Zaka ya 10% unatoa kwenye faida au kwenye utajiri wako?

Zaka ya 10% unatoa kwenye faida au kwenye utajiri wako?

Kwenye hizi mambo ya imani kumejaa utapeli mtupu, mtu anachukua mkopo benki baba yake wa kiroho anamwambia toa fungu la kumi kwa ajili ya ulinzi wa huo mkopo[emoji1664]
Sasa mkopo ni pesa yako [emoji1787][emoji1787][emoji1787] zaka ilikuwa inatolewa kwa vile vilivyo vyako.kutoa mkopo zaka ni sawa sawa na umeajiliwa kuchunga ng'ombe mia wa tajiri yako wewe uchukue ng'ombe 10 wa tajiri na kuwatoa zaka kisha unasema hiyo ni zaka yako[emoji23][emoji23]
 
Kwenye hizi mambo ya imani kumejaa utapeli mtupu, mtu anachukua mkopo benki baba yake wa kiroho anamwambia toa fungu la kumi kwa ajili ya ulinzi wa huo mkopo🦍
Hiyo tayari imeshakuwa hasara. Kisa baba wa kiroho,tena hapo hapo nyumbani unga unabaki robo. Jama anakata tena kidogo anampa. Tena waliomuombea kupata huo mkopo,anaambiwa lazima washikwe mkono. Sasa kwenye kurudisha ameshindwa,nyumba yake(kama anayo),inapigwa mnada,baba wa kiroho anamuombea ajikaze tu kiume,kwamba yeye si wa kwanza wala wa mwisho.
 
Kama ni mtumishi serikali imkate PAYE, makato ya mifuko ya kijamii (NSSF n.k.), makato ya mikopo, makato ya uanachama wa vyama vya wafanyakazi, bima ya afya kisha mtumishi huyo huyo atoe matoleo, malimbuko, zaka, sadaka, nadhiri n.k. mbona atakuwa na maisha magumu sana huyo mtumishi wajameni?
Hahhaaha huo ni utapeli mkuu Kumnyang'anya mtu
 
Sauli kuna kisa alishika vazi la samweli likapasuka katikati akaambiwa ufalme wako umepasuliwa kwa maana umekataliwa ...wapumbavu wa makanisani wa leo wanabisha kuwa hekalu alipo tena mungu kalikataa katika kanuni aliyo sema yesu kuwa ...mara ngapi nimekukusanya kama vifaranga lakini umekataa basi nyumba yako umeachiwa ukiwa .....pia wasome uzinduzi wa hekalu mungu alisema nini juu ya Israel kuhusu hekalu kuwa kama wana wa Israel watamuasi yeye basi atalipiga hilo hekalu hata watu wa mataifa watashangaa kakisema hawa walimfanya nini mungu wao ....kitendo cha yesu kukuta wahuni hekaluni ndiyo ushuhuda kuwa hekalu lilikataliwa kwa kupasuka kwa pazia vipande viwili.
Safi sana! Mkuu itoshe kusema Kuna baadhi ya maeneo nakubaliana na wewe kabisa
 
Kanisa limechukua nafasi ya hekalu.
Hahaha kanisani haliwezi kuchukua nafasi ya hekalu...
Labda kama ungeniambia Kanisa limechukua Nafasi ya Sinagogi...
Mkuu nenda kwanza kasome nini maana ya Hekalu na kazi zake na nini maana ya Synagogue na kazi zake..
Vinginevyo utakuwa unatumia hisia kujibu..
 
Peleka kwenye Kanisa linalohubiri sana habari za dhambi na kuishi maisha mema. Ukiona kanisa sijui inahubiri upate gari au nyumba, achana nalo
Vipi kule wanatangaza kiasi kinachokusanywa kila jumapili?
Vipi waumini huwa wanajulishwa matumizi ya Zaka hizo?
 
Malaki alikuwa nabii wa Mungu wa miungu yote duniani.
Mahali hapo ulipo, mchungaji wako anasema, Hatutoi zaka ili tubarikiwe bali tunalipa!
Vipi unalinganishaje hiyo Malaki na anachosema Mchungaji wako?
 
PAYE, HESLB, NSSF na makato mengine halafu church nako wanataka 10% ya huo mshahara? Mbinguni wataenda wachache sana kwa hali hii. Kanisani nitatoa tu mchango wa ujenzi na mambo mengine muhimu ila kuhusu Zaka na sadaka nitatoa kulingana na ninavyoguswa. Ile kauli kwamba wachungaji wanakula madhabahuni naiheshimu ila nao wapambane kujiongezea vyanzo vya mapato.
Mkuu uko sawa!
Mtume Paulo alifanyakazi za mikono ili ajikimu! Alikuwa Fundi wa kushona Mahema.
Lakini Wachungaji wa Nyakati zetu ni kubanana waumini.
Achilia mbali muumini anatoa zaka, lakini ataambiwa atoe sadaka ya kumtegemeza Mchungaji!
 
Hata Hekalu ni Mwili wa Kristo ambao ni sisi Wakristo,(1Wakorintho6:18-19)
Kwa hiyo Hekalu na Kanisa tafsiri yake ni moja.
Kuna Jengo la Hekalu au Jengo la Kanisa, lakini kuna Hekalu au Kanisa ambalo ni sisi Wakristo, Matendo2:47
Hekalu ni Jengo na Kanisa ni mwili wa Kristo
 
Kanisa ni mwili wa Kristo maana yake ni sawa na kusema Kanisa ndiye Kristo.

Kama Kichwa kinavyokuwa na mwili ili mtu akamilike.

Hivyo Kristo ni Kichwa na kanisa ni mwili ili Kristo akamilike.

Ndio maana mtu anapookoka na kumpokea Kristo, Kristo ndiye anayeishi ndani yake kupitia roho wake.

Hata sehemu/jengo tunalokutanika kufanya ibada kwenye ulimwengu wa mwili ni Kanisa pia, hivyo fungu la kumi ni sahihi kabisa kupeleka kanisani.

Rejea kanisa la mwanzo, wale waliouza mali zao walipeleka fedha zao Kanisani.

Matendo ya mitume 4:34-35
Yesu Kristo alishajitoa Sadaka hivyo mambo ya Zaka, Fungu la 10 nk alishazitamatisha

Fungu la 10 wanatoa Majamatini kwa wahindi
 
Tofautisha msaada na fungu la 10%.

Pia elewa msaada hauchagui wa kunugaika lakini fungu la 10%,zaka,sadaka,harambee,nk ni wizi na wanaonufaika ni maaskofu na wachungaji kwa kula vzr,magari,ndege,pombe,majumba,nk

Hili haliondoi muongozo wa fungu la 10,hutolewa madhabahuni tu na si kwengineko,tafuta kanisa imara upeleke zaka.
 
Mkuu uko sawa!
Mtume Paulo alifanyakazi za mikono ili ajikimu! Alikuwa Fundi wa kushona Mahema.
Lakini Wachungaji wa Nyakati zetu ni kubanana waumini.
Achilia mbali muumini anatoa zaka, lakini ataambiwa atoe sadaka ya kumtegemeza Mchungaji!
Yesu mwenyewe hakuwa na hayo mambo ya kubana watu. Yeye ndo alilisha watu 5000 lakini siku hizi watu 5000 wanamlisha mtu mmoja. Kwa wasiojua ni kuwa wachungaji wa sasa wanapiga dili nyingi sana chafu na safi.
 
Hahaha kanisani haliwezi kuchukua nafasi ya hekalu...
Labda kama ungeniambia Kanisa limechukua Nafasi ya Sinagogi...
Mkuu nenda kwanza kasome nini maana ya Hekalu na kazi zake na nini maana ya Synagogue na kazi zake..
Vinginevyo utakuwa unatumia hisia kujibu..
Tatizo lako unatumia tafsiri za kale za Kiyahudi ndio maana hatuelewani.

Isitoshe 'kiroho' hata mwili wa mtu pia ni hekalu.

Agano la kale hekalu lilikuwa ni jengo ila kwa sasa hekalu linaweza kuwa jengo (Kanisa) au mwili.

1 Wakorintho 3:16
Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
 
Unataka kusema mtaji Mungu hakuwezeshi au?
Maandiko yote uliyoyatoa ukiyaangalia kwa kina yanagusia vyote mfano angalia maneno haya " fungu la kumi la vitu vyote" Je? mtaji haupo kwenye vitu vyote?...

Kama fungu la kumi ni ulinzi wa mapato yetu je? tunapaswa kulinda faida tu na siyo mtaji?.. Haya masuala yanahitaji uelewa mpana sana kiroho siyo kiuchumi tu. Je? faida tu ndiyo inayohitaji baraka za Mungu na ulinzi na siyo mtaji?.
Kuna mahali hatujaelewa



Faida ni kile Mungu alichokuwezesha kukipata baada ya wewe kuwekeza mtaji, hicho ndicho unachopaswa kukitolea zaka ya asilimia 10 au zaidi ukiamua hivyo.

Mwanzo 14:16
Naye akarudisha mali zote, akamrudisha na Lutu nduguye na mali zake, na wanawake pia, na watu.

Mwanzo 14:20
Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.

Abraham alimpa kuhani Melikizedeki fungu la kumi la vitu vyote alivyovitwaa kutoka kwa wale wavamizi (asilimia kumi ya faida aliyopata).

Kumbukumbu la Torati 14:22
Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi katika maongeo yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka.

Toa fungu la kumi la 'maongeo: yote ya mbegu zako......(faida inayotokana na mbegu zako kwenye shamba mwaka baada ya mwaka).



Kumbukumbu la Torati 14 28
Kila mwaka wa tatu, mwisho wake, toa fungu la kumi lote la maongeo yako ya mwaka huo, uliweke ndani ya malango yako;

Toa fungu la kumi la maongeo (mapato,maongezeko) yako ya mwaka huo ndani ya malango yakk.
 
Ukitaka kujua ukweli tumia hata haya niliyo yasema kisha yapime kwa kusoma upya injili ...utagundua ni kwanini yesu alipo kuwa hai alisema atakufa na siku ya 3 atafufuka ila alipo kuwa msalabani anamwambia yule aliye sulibiwa naye kuwa leo hii utakuwa pamoja nami peponi ....mtu mpumbavu ataona hapo ni lugha gongana ila mimi kwa kuwa naijua injili ya kweli nijua ni nini alicho kuwa ana maanisha Yesu wala siyo lugha gongana .....pia ukitumia haya niliyo kuambia utajua kuwa Yesu alipo ulizwa swali na wanafunzi wake kuhusu kiama kitakuwa lini ...utagundua kuwa yesu alisema yeye anajua siku ya kihama ...tofauti na wakristo wanavyo fundishwa kuwa yesu alisema hajui ...ila ukweli ni kwamba alicho jibu yesu kilikuwa ni kukili kuwa anajua wala siyo kukataa ina logic sawa na kufufuka siku ya tatu ila ana mwambia yule mtu msalabani leo hii tutakuwa pamoja pema peponi.
Tuambie sasa alichomaanisha Yesu na tuonyeshe kwa andiko Yesu alipokiri anaijua siku ya kiama.
 
Ukitaka kujua ukweli tumia hata haya niliyo yasema kisha yapime kwa kusoma upya injili ...utagundua ni kwanini yesu alipo kuwa hai alisema atakufa na siku ya 3 atafufuka ila alipo kuwa msalabani anamwambia yule aliye sulibiwa naye kuwa leo hii utakuwa pamoja nami peponi ....mtu mpumbavu ataona hapo ni lugha gongana ila mimi kwa kuwa naijua injili ya kweli nijua ni nini alicho kuwa ana maanisha Yesu wala siyo lugha gongana .....pia ukitumia haya niliyo kuambia utajua kuwa Yesu alipo ulizwa swali na wanafunzi wake kuhusu kiama kitakuwa lini ...utagundua kuwa yesu alisema yeye anajua siku ya kihama ...tofauti na wakristo wanavyo fundishwa kuwa yesu alisema hajui ...ila ukweli ni kwamba alicho jibu yesu kilikuwa ni kukili kuwa anajua wala siyo kukataa ina logic sawa na kufufuka siku ya tatu ila ana mwambia yule mtu msalabani leo hii tutakuwa pamoja pema peponi.
Tuambie sasa alichomaanisha Yesu na tuonyeshe kwa andiko Yesu alipokiri anaijua siku ya kiama.
 
Back
Top Bottom