Zakazakazi: Yanga sio Mabingwa mara 29 na Simba sio Mabingwa mara 22

Zakazakazi: Yanga sio Mabingwa mara 29 na Simba sio Mabingwa mara 22

Mkuu kaangalie list ya Club kongwe Ulaya kabla hata ligi KUU kuanza ndio utaelewa ninachokiandika.

Kipindi ambacho Simba na Yanga zimeanzishwa kulikuwa na mashindano local tu ambayo hayana hadhi ya kua ligi kuu.

Ni sawa na mashindano yanayochezwa na timu za mtaani tu
Kama kombe la Abiora?
 
TFF waoga sana wanajua hii kitu itavyokuja kuleta ugomvi
Unajua kwenye masuala ya takwimu ukiwa mjanja unaweza kuzitumia unavyotaka wewe kwa manufaa yako na kwa kiasi fulani ukawa sahihi ingawa ndani yake umefanya udanganyifu kwa kuacha data fulani.

Kipindi kile Yanga wanajigamba kwa rekodi za unbeaten, walipokumbushwa mbona mmefungwa mashindnao ya CAF, piw na Vipers, wakasema ooh tunahesabu mashindano ya ndani tu.

Kuna msemo mmoja kuhusu takwimu nikiukumbuka nitauleta.
 
Wewe na huyo Zaka Zakazi kuna kitu mmeshindwa kuelewa. Kuna ligi ya muungano na ligi ya Tanzania bara. 29 kwa Yanga na 22 kwa Simba ambazo zinahesabiwa ni kwa makombe ya ligi ya Tanzania bara. Kuna wakati ligi ilikuwa inahusisha timu kutoka Zanzibar na kuitwa ligi ya muungano. Kuna timu zilikuwa zinachukua ubingwa wa Tanzania bara pekee na zingine zilikuwa zinachukua yote mawili kwa pamoja (Muungano na bara)
Tupe mfano.

Mwaka upi kulikuwa kunachezwa ligi mbili kwa wakati mmoja?

Yaani Ligi ya Bara na Muungano.
 
Hapo kwenye list ya mabingwa ya Zakazakazi kuna Tukuyu stars na Mtibwa ambao wamesahaulika
Coastal Union pia hayupo.
Hivyo Zakazakazi hana data kamili.
Ushindi unaotajwa hauhusishi timu za Zenji.
Wakati ule mabingwa wa bara walikuwa wakicheza na mabingwa wa Zenj Sidhani kama ilikuwa ligi.
Nikumbusheni.
 
1907 ni kombe gani?
Soma juu kabisa.
IMG_20230615_105308.jpg
 
Ndio ujue anaokoteza tu ili kuwafanya mikia angalau mupate cha kuegemea na kushangilia mwaka huu
The more we get, the more you lose.

Kadri tunavyozidi kuwakumbuka mabingwa wengine ambao tuliwasahau kwenye list ndivyo inavyozidi kupungua nafasi ya Yanga kumiliki makombe mengi
 
Unajua kwenye masuala ya takwimu ukiwa mjanja unaweza kuzitumia unavyotaka wewe kwa manufaa yako na kwa kiasi fulani ukawa sahihi ingawa ndani yake umefanya udanganyifu kwa kuacha data fulani.

Kipindi kile Yanga wanajigamba kwa rekodi za unbeaten, walipokumbushwa mbona mmefungwa mashindnao ya CAF, piw na Vipers, wakasema ooh tunahesabu mashindano ya ndani tu.

Kuna msemo mmoja kuhusu takwimu nikiukumbuka nitauleta.
Tatizo lako hua haujui na hauja gungua haujui ile unbeaten ilikua domestically ndio maana hata Arsenal , Benifica, AC Milan records zao zipo sababu unakuaga pimbi tunaku zoom tu
 
Anaandika Zakazakazi,

YANGA SIYO MABINGWA MARA 29 NA SIMBA SIYO MABINGWA MARA 22

Hii ni changamoto kwa wadau wote wa soka nchini Tanzania; wachambuzi, waandishi wa habari, mamlaka za soka na serikali kwa maana ya wizara ya michezo na baraza la michezo.

Fanyeni utafiti na mje na majibu sahihi maana siku zinavyozidi kwenda, uongo unakuwa ukweli kwa sababu watu wanaamini yasiyo sahihi.

Ligi ya Tanzania ilianza mwaka 1965 ikiitwa Klabu Bingwa ya Taifa. Hadi mwaka huu, 2023, ni miaka 58. Maana yake kuna mabingwa 58 wanatakiwa kuwepo.

Sasa kama Yanga ni mabingwa mara 29, Simba mara 22 maana yake hawa wawili peke yao wamechukua ubingwa mara 51.

Katika misimu 58, imebaki misimu 7 pekee ambayo wamechukua wengine.

Hao wengine ni wafuatao.

Cosmopolitan -1 (1967)
Mseto -1 (1975)
Pan African - 1 (1982)
KMKM - 1 (1984)
Majimaji - 3 (1985, 1986 na 1998)
African Sports - 1 (1988)
Malindi - 2 (1989 na 1992)
Pamba - 1 (1990)
TZ Prisons - 1 (1999)
Azam FC - 1 (2014)

Jumla 13

Ukijumlisha na zile 51 za Yanga na Simba, unapata 64...inawezekanaje?

Ligi iliyochezwa miaka 58 inakuwaje na mabingwa 64...hesabu za wapi hizo?

Timu zilizotajwa hapo ndiyo mabingwa wa Tanzania wanaotambuliwa na CAF na FIFA, na ndiyo walioshiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika katika miaka husika.

Ndiyo maana nilianza kwa kutoa changamoto kwa wadau.

Tembeleeni tovuti za CAF na FIFA muone ni timu zipi ziliiwakilisha Tanzania kwenye Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika kuanzia 1965.

UKWELI
Yanga ni mabingwa mara 22 na Simba mara 21.

22+21= 43 - Yanga na Simba
43+13=56 - Jumla (kati ya 58)

NB: Kuna misimu miwili (1970 na 2003) Tanzania hakukuwa na bingwa.

Ndiyo maana unapata mabingwa 56 katika misimu 58.

Itaendelea...
Huyu jamaa anawaita wenzake Changamoto wakati yeye mwenyewe ni changamoto.
Nimepita kwa sekunde 4 tu kaba sijaanza kuisoma tayari nimeona data ambazo sizo, naamini nikipata muda wa kusoma huenda nikaona zaidi taarifa ambazo zisizo.
Mwaka 1986 bingwa hakuwa Majimaji bali Tukuyu Stars.
 
MISIMU MIWILI HAKUKUWA NA BINGWA

Kuna misimu miwili Tanzania haikuwa na bingwa rasmi kutokana na sababu tofauti...mwaka 1970 na mwaka 2003.

1970

Mwaka 1970 ligi haikufanyika kabisa kwa sababu timu nyingi ziligomea kushiriki, zikiongozwa na Yanga na Sunderland (Simba).

Mwaka huo FAT iliruhusu timu nyingi za mashirika kushiriki ligi. Wachezaji wa Yanga na Sunderland walikuwa wanafanya kazi kwenye hayo mashirika(ikiwemo Bandari na Cargo).

Kwa hiyo hayo mashirika yakazuia wafanyakazi wao kuchezea timu za mtaani ili wachezee timu zao za kazini.

Yanga na Sunderland zikakosa wachezaji, zikajitoa kwenye ligi...na ligi haikufanyika.

FAT ikaichagua Yanga ishiriki klabu bingwa Afrika mwaka 1971, kwa sababu walikuwa mabingwa wa msimu uliopita. Yanga wakajihesabia kupewa na ubingwa...lakini walipewa tiketi tu!

2003

Mwaka huu Ligi ya Muungano ambayo ndiyo ilikuwa ligi kuu ya Tanzania, haikumalizika baada ya Yanga kufungua kesi mahakama ya Ilala kupinga ligi kuchezwa kwa mtoano.

Yanga walipangwa kucheza na Jamhuri ya Pemba, na wakatoka Dar Es Salaam kuelekea Pemba. Kufika Unguja wakagoma kwenda Pemba wakisema wamegundua ligi huwa haichezwi kwa mtoano.

FAT na ZFA kama waandaaji wa ligi ya Muungano wakaitoa Yanga na kuipa ushindi Jamhuri. Yanga wakaenda mahakamani kupinga kutolewa.

Mahakama ikasimamisha ligi na kupanga kusikiliza kesi Februari 2004.

Ligi ikasimama na FAT na ZFA wakaipa Simba tiketi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa mwaka 2004.

Simba wakajitangazia kupewa na ubingwa...lakini haikuwa hivyo, walipewa tiketi tu.

Mara hizo mbili, ndizo zinafanya hesabu iwe 58 lakini mabingwa halisi ni 56.

Itaendelea...
 
MISIMU MIWILI HAKUKUWA NA BINGWA

Kuna misimu miwili Tanzania haikuwa na bingwa rasmi kutokana na sababu tofauti...mwaka 1970 na mwaka 2003.

1970

Mwaka 1970 ligi haikufanyika kabisa kwa sababu timu nyingi ziligomea kushiriki, zikiongozwa na Yanga na Sunderland (Simba).

Mwaka huo FAT iliruhusu timu nyingi za mashirika kushiriki ligi. Wachezaji wa Yanga na Sunderland walikuwa wanafanya kazi kwenye hayo mashirika(ikiwemo Bandari na Cargo).

Kwa hiyo hayo mashirika yakazuia wafanyakazi wao kuchezea timu za mtaani ili wachezee timu zao za kazini.

Yanga na Sunderland zikakosa wachezaji, zikajitoa kwenye ligi...na ligi haikufanyika.

FAT ikaichagua Yanga ishiriki klabu bingwa Afrika mwaka 1971, kwa sababu walikuwa mabingwa wa msimu uliopita. Yanga wakajihesabia kupewa na ubingwa...lakini walipewa tiketi tu!

2003

Mwaka huu Ligi ya Muungano ambayo ndiyo ilikuwa ligi kuu ya Tanzania, haikumalizika baada ya Yanga kufungua kesi mahakama ya Ilala kupinga ligi kuchezwa kwa mtoano.

Yanga walipangwa kucheza na Jamhuri ya Pemba, na wakatoka Dar Es Salaam kuelekea Pemba. Kufika Unguja wakagoma kwenda Pemba wakisema wamegundua ligi huwa haichezwi kwa mtoano.

FAT na ZFA kama waandaaji wa ligi ya Muungano wakaitoa Yanga na kuipa ushindi Jamhuri. Yanga wakaenda mahakamani kupinga kutolewa.

Mahakama ikasimamisha ligi na kupanga kusikiliza kesi Februari 2004.

Ligi ikasimama na FAT na ZFA wakaipa Simba tiketi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa mwaka 2004.

Simba wakajitangazia kupewa na ubingwa...lakini haikuwa hivyo, walipewa tiketi tu.

Mara hizo mbili, ndizo zinafanya hesabu iwe 58 lakini mabingwa halisi ni 56.

Itaendelea...
Nenda CAS Mwanasheria
 
Tatizo lako hua haujui na hauja gungua haujui ile unbeaten ilikua domestically ndio maana hata Arsenal , Benifica, AC Milan records zao zipo sababu unakuaga pimbi tunaku zoom tu
Mara nyingi na ignore replies zako ili nijilindie heshima ila leo nakublock rasmi, usihangaike kujibu post zangu maku wee.

Kama mnafuata standard za Ulaya, na hiyo treble ya juzi mliyofanyia gwaride na tamasha nayo inafuata standard za Ulaya?
 
Mkuu kaangalie list ya Club kongwe Ulaya kabla hata ligi KUU kuanza ndio utaelewa ninachokiandika.

Kipindi ambacho Simba na Yanga zimeanzishwa kulikuwa na mashindano local tu ambayo hayana hadhi ya kua ligi kuu.

Ni sawa na mashindano yanayochezwa na timu za mtaani tu
MFANO KUTOKA ULAYA

Una maanisha msimu wa 1990-91 wa First League Division wa nchini Uingereza ni sawa na Ndondo za mtaani?


Hii hapa ni team squad ya Liverpool ya msimu 1990-91 kabla ya Ligi kuitwa EPL.
1dffdf.JPG
 
Mara nyingi na ignore replies zako ili nijilindie heshima ila leo nakublock rasmi, usihangaike kujibu post zangu maku wee.

Kama mnafuata standard za Ulaya, na hiyo treble ya juzi mliyofanyia gwaride na tamasha nayo inafuata standard za Ulaya?
Maku mwenyewe
 
Ni kweli ila swali lingine, je ni sahihi kuweka pembeni takwimu za waliochukua Muungano au na zenyewe inabidi tuzijumuishe pale timu inapojigamba kuwa imechukua ubingwa mara kadhaa?

Kwa nini Yanga hawajumuishi takwimu za Kombe la Muungano?
Yanga imechukua kombe la muungano mara 6 na katika hizo mara sita ni mara moja pekee ndio kawa bingwa wa kombe la muungano pasipo kuchukua kombe la Tanzania bara (mwaka 2000) ila mara tano zote kabeba makombe mawili kwa pamoja. Hivyo kwenye takwimu zao zina makombe mawili kwa pamoja pia
 
Back
Top Bottom