Zamani nilikuwa namshangaa mtu aliyefanikiwa kimaisha na hasaidii ndugu zake, Leo mimi natamani hata kuwapiga Risasi

Zegota Msaada una hatarisha uhuru wa mtu, mimi ningekuwa ndugu yako ningekuroga hasa ufilie kwa mbali, ndugu zako wako sahihi kukuumiza, kukuombea mabaya!

kwa nini unawasaidia? kwani wao vilema? hawana mikono? akili, na utashi? au Mazezeta pa kutoa misaada hupajui? Ndugu zake Matonya, Mayatima! shule ya viziwi Buguruni Malapa, hupajui? peleka misaada huko!

Misaada hatari kwa uhuru, kwa nini ulihatarisha uhuru wao kwa misaada yako? na ulijuaje ulicho wapa kinakidhi mahitaji yao? wewe ndiyo una roho mbaya! unachuki ambayo huijui, unawaroga kisaikolojia kwa kile unachoona binafsi ni Misaada! umtatulie ndugu yako matatizo usiyo yajua?

Ndugu zangu wa Damu, popote mlipo Diasporas na kwingineko ole wenu mnisaidie mimi Nyarusare, naanza nanyi kuwamaliza! wengine wanajipendekeza kupenyeza vijimisaada maksudi sababu Baba ya mtu ni tajiri, ili wamsimange baadaye! na ku gain popularity! kupitia mgongo wangu!

Ndugu Mpe njia yatosha, usimuonyeshe njia, bali Mpe njia ya mafanikio halafu mtupe nje ya Mawanda yako, Mtukane on the spot! atajiju hiyo safi sana, atarudi kukushukuru! na mtakuwa kitu kimoja!

Na ndugu mpenda vya kupewa toka hapo kwa bro! wako, anza hivo ulivo! kalale chini sokoni kariakoo! kashinde stendi, kula kwa ma ntilie, osha vyombo/suuza, atakulipa, Malori ya Mkoa yakija usiku jichanganye na Matingo piga kazi upate msingi. Msaidie wewe huyo anaye penda kukupa misaada wewe.

Weye ndiyo uwe tegemeo la misaada kwao, siyo wewe ndiyo upewe kataa vya kupewa hata ukilala njaa! ikibidi watie Bakora seriously wale watoa misaada kwako wote! then watupie hela zao usoni, japo huna kitu! hii itawachanganya, soon watakuiga mwenendo wako wa maisha!

Mleta Mada wewe ni Hatari sana! kuliko siraha za maangamizi au Bomu la Nuclear! Msaada haujawahi kuiletea jamii yeyote Maendeleo Duniani! Leo miaka zaidi ya hamsini bado Tanzania mnatega Bakuri chanzo humuhumu yaani ni watu km wewe!
 
Uache kazi kisa ndugu? Acha umama, achana nao
 
Wewe ni ndugu yake!!? Au mnapenda zogo tu.

Haya kasaidika nini sasa!?
kwani ameomba msaada? au ametoa mawazo yake tu. hata hivyo wewe huoni msaada wa mawazo ya wengine humu,huoni maoni kinzani humu?au ulitegemea msaada wa chakula
 
Mimi Bora nihonge hela kwa Demu angalau najua naweza kupata "return to investment" kuliko nisaidie ndugu
 
Kama unaniongelea mimi vileeee.........



Dah
Ni hatari sana
 
Kwani huwezi kumsaidia mtu wakati huo huo ukaweka mipaka ya mazoea ya kijinga jinga?? Kitu tunachokosea wabongo ni kuleta mazoea yasiyo na msingi na ile dhana ya polygamy family, unakuta mtoto wa shangazi sijui mama mdogo, mtoto wa dada wote wanakaa kwako.. Hapa lazima kuna lawama..

Mzee Mkapa alikuwa na ndugu wengi tu na alikuwa akiwasaidia sana sana pasipo kuwa na mazoea yaliyovuka mipaka na ki ukweli hao ambao aliweka nao mipaka waliupokea msaada na wakautumia vizuri. Sasa cha kushangaza Kuna binti mtoto wa dada yake aliyemchukua na kuishi nae, huyo ndiye akaja kuwa sifuri na wa ajabu kabisa.

Tujifunze kusaidia wengine na kuweka mipaka ya mazoea, ndugu wana lawama lakini kuacha kuwasaidia eti kuogopa hizo lawama hiyo nayo ni roho mbaya iliyovuka mipaka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…