Nikiwa darasa la tatu(Njombe huko) masikini hatujui hata kubalehe ni nini basi classmate wetu mvulana alikuwa mchokozi akagombana na rafiki yangu msichana akamwambia ndio maana una "mavu zi" bila kujua "mavu zi" ni nini nikamwambia "mavu zi" mwenyewe ghafla na mwalimu akawa anaingia akatoa kisago maana alilisikia lile neno akatuchukua mimi, rafiki yangu, na yule mvulana akatupeleka ofisini...... kufika ofisini akawaambia walimu nimewakuta wanagombana tena wanatukanana wanambiana mavu zi sasa nataka waniambile mbele ya walimu wenzangu eti mavu zi ni nini?
Mwalimu mmoja akadakia akasema mwalimu kwani wewe hujui"Mavu zi" ni nini, si ni matunda ya Uwemba hahaha walimu wote waliangua kicheko ila tulikula mboko tatu tatu kila mmoja kisha tukarudi darasani na nilikuwa sijui mavu zi ni nini mpaka nilipokua muda wote nilikuwa na lile jibu kuwa ni matunda ya Uwemba.