Zamani watoto walitafuta wazazi wao waliowatelekeza, zama hizi wazazi ndiyo wanatafuta watoto wao

Zamani watoto walitafuta wazazi wao waliowatelekeza, zama hizi wazazi ndiyo wanatafuta watoto wao

Watoto na wazazi wote kwa pamoja mue na adabu...
 
Usidanganyike!! Baba mzazi amebeba baraka kwa ajili ya wanawe!! Ukijiona umefanikiwa japo huna mahusiano mazuri na wazazi au umewatelekeza kwa makusudi ni kwamba arobaini zako ziko njiani zinakuja!! Kuna watu wana pesa lakini wanaishi maisha chini ya laana.

Magonjwa yasiyoponyeka!! hasara za mara kwa mara kwenye biashara! kudhulumiwa makazini au kwenye biashara, kuibiwa, watoto kukuasi pia, mahusiano mabaya kwenye ndoa na mambo mengine ya hovyo kukuandama.

Wanaokutazama wanaweza kudhani una raha na maisha mazuri lakini wewe mwenyewe unajua huna raha wala amani yoyote katika maisha yako!! Usicheze na wazazi!! Ukifanya hivyo usitafute mchawi!! wewe ndo mchawi wa maisha yako mwenyewe.

Nadhani atakuwa kakuelewa asijijaze ujinga
 
Mimi ni wa zamani pia, mzee aliingia mitini tangu nikiwa kichanga, lakini hata siku moja sikuwahi kumuulizia licha ya mama kutaka kufanya juhudi nionane nae lakini moyo wangu haukuwa tayari, niliwahi kupewa simu siku moja nimsalimie ila sikufanikiwa kumaliza hata sekunde 30 kuzungumza nae.

Sijawahi kulishwa sumu juu yake ila ni vile tu nahisi nilishamtoa kwenye maisha yangu. Kwenye nyaraka zangu zote muhimu zinazohitaji taarifa za wazazi upande wa baba huwa naandika amefariki.

Hata nikisema nikutane nae katika umri huu huwa naona ni suala la kinafiki tu nitazungumza nae kitu gani??. Hakuna bond.

Muda utafika utamtafuta utatuletea mrejesho hapa
 
Kati ya Baba na Mtoto ni nani anapaswa kujua umuhimu wa mwenzake?

Ikiwa Baba katelekeza familia na hajui umuhimu wa familia na watoto iweje useme watoto hawajui umuhimu wa Baba?
Mtoto hajui kitu, vile unavyomlea ndivyo anavyokua.
Watoto wengi wa 2000 mfano wao ni daimond PLATENUM /ommy dimpoz etc ,,kwamba hata bila kuwa na baba unatoboa maisha.

Kwamba mama ndy kila kitu.

Kumbe wanajidanganya sn.

Singel mothers wa zamani walikuwa wanawaeleza watoto wao umuhimu wa kuwa na baba hata kama hajakulea,
Mama atakueleza kwamba yule ni baba yako na unapaswa umuheshimu na kumpenda kama unipendavyo mimi mama yako,
Single mothers wa zamani hawakuwa wabinafsi wala chuki kwa baba watoto wao.
Na hata watoto walijivunia kuwa na baba hata kama ni baba jina tu.

Wanawake wa sasa ni wabinafsi na wamejawa na tamaa na chuki dhidi ya mwanaume aliyezaa nae watoto.


mwanamke (single mother) ndy chanzo kikubwa cha watoto kuwakataa baba zao.
90% ya watoto wanaowakataa baba zao ukiangalia kwa makini ni chuki zilizopandikizwa na mama zao.sababu ya chuki zao binafsi kwa baba watoto wake.

Hakuna baba asiyetaka kulea family yake lazima kuna sababu nzito ambazo zimesababishwa na single mothers..
 
Sema mitoto ya ckuiz Ni ya hovyo kbsa haina adabu kwa wazazi wao
 
Watoto wengi wa 2000 mfano wao ni daimond PLATENUM /ommy dimpoz etc ,,kwamba hata bila kuwa na baba unatoboa maisha.

Kwamba mama ndy kila kitu.

Kumbe wanajidanganya sn.

Singel mothers wa zamani walikuwa wanawaeleza watoto wao umuhimu wa kuwa na baba hata kama hajakulea,
Mama atakueleza kwamba yule ni baba yako na unapaswa umuheshimu na kumpenda kama unipendavyo mimi mama yako,
Single mothers wa zamani hawakuwa wabinafsi wala chuki kwa baba watoto wao.
Na hata watoto walijivunia kuwa na baba hata kama ni baba jina tu.

Wanawake wa sasa ni wabinafsi na wamejawa na tamaa na chuki dhidi ya mwanaume aliyezaa nae watoto.


mwanamke (single mother) ndy chanzo kikubwa cha watoto kuwakataa baba zao.
90% ya watoto wanaowakataa baba zao ukiangalia kwa makini ni chuki zilizopandikizwa na mama zao.sababu ya chuki zao binafsi kwa baba watoto wake.

Hakuna baba asiyetaka kulea family yake lazima kuna sababu nzito ambazo zimesababishwa na single mothers..

Wakati mama anamlisha sumu mtoto baba unakuwa upo wapi?
 
Usidanganyike!! Baba mzazi amebeba baraka kwa ajili ya wanawe!! Ukijiona umefanikiwa japo huna mahusiano mazuri na wazazi au umewatelekeza kwa makusudi ni kwamba arobaini zako ziko njiani zinakuja!! Kuna watu wana pesa lakini wanaishi maisha chini ya laana.

Magonjwa yasiyoponyeka!! hasara za mara kwa mara kwenye biashara! kudhulumiwa makazini au kwenye biashara, kuibiwa, watoto kukuasi pia, mahusiano mabaya kwenye ndoa na mambo mengine ya hovyo kukuandama.

Wanaokutazama wanaweza kudhani una raha na maisha mazuri lakini wewe mwenyewe unajua huna raha wala amani yoyote katika maisha yako!! Usicheze na wazazi!! Ukifanya hivyo usitafute mchawi!! wewe ndo mchawi wa maisha yako mwenyewe.

Yaani baba atekeleze familia yake alafu yeye akitelekezwa mtoto anapata yote hayo?
Kama unafikiri kwa namna hii basi hukupaswa kuwa katika karne hii.

Upo katika karne hii kimakosa sana kama utakuwa na mitazamo hiyo ya karne za 20 kurudi nyuma.
 
Kizazi cha miaka ya 2000 ni kizazi ambacho hakina maadili.

Ni kizazi cha singel mothers 60%..

Hawajuwi umuhimu wa baba ktk family..

Dawa ni baba kutafuta pesa kwa bidii ili mtoto ajute yeye na mama yake single mother..

Baba aliyekimbia familia ndio anajua umuhimu wake ndani familià?
Yaani Baba ukimbie familia alafu wewe ndio ujitie unajua umuhimu wa Baba kwenye familia na kuanza kulaumu Mwanamke na watoto kuwa hawajui umuhimu wa Baba ndani ya familia?
 
Usidanganyike!! Baba mzazi amebeba baraka kwa ajili ya wanawe!! Ukijiona umefanikiwa japo huna mahusiano mazuri na wazazi au umewatelekeza kwa makusudi ni kwamba arobaini zako ziko njiani zinakuja!! Kuna watu wana pesa lakini wanaishi maisha chini ya laana.

Magonjwa yasiyoponyeka!! hasara za mara kwa mara kwenye biashara! kudhulumiwa makazini au kwenye biashara, kuibiwa, watoto kukuasi pia, mahusiano mabaya kwenye ndoa na mambo mengine ya hovyo kukuandama.

Wanaokutazama wanaweza kudhani una raha na maisha mazuri lakini wewe mwenyewe unajua huna raha wala amani yoyote katika maisha yako!! Usicheze na wazazi!! Ukifanya hivyo usitafute mchawi!! wewe ndo mchawi wa maisha yako mwenyewe.
Ukiwa na mahusiano mazuri na baba yako aliyekutelekeza hutapeliwi?

Wote wenye mahusiano mabaya ya ndoa hawana radhi za baba zao?

Wanaofirisika wote waligombana na baba zao?

Wagonjwa wote hospitali na majumbani waligombana na baba zao?

Yatima ambaye hakulelewa na baba au mama (assume alilelewa kituoni) huyo hawezi kuachwa, kutapeliwa, kufirisika, kuibiwa na kuumwa?

Yani shida za binadamu zote unadai ni kutozungumza na wazazi.
 
Ukiwa na mahusiano mazuri na baba yako aliyekutelekeza hutapeliwi?

Wote wenye mahusiano mabaya ya ndoa hawana radhi za baba zao?

Wanaofirisika wote waligombana na baba zao?

Wagonjwa wote hospitali na majumbani waligombana na baba zao?

Yatima ambaye hakulelewa na baba au mama (assume alilelewa kituoni) huyo hawezi kuachwa, kutapeliwa, kufirisika, kuibiwa na kuumwa?

Yani shida za binadamu zote unadai ni kutozungumza na wazazi.

Kama Baraka zingekuwa zinatoka kwa Wazazi pasingekuwa na binadamu mwenye shida au umaskini katika dunia hii.

Hizo kauli wanazosema ni kauli za kizamani sana ambazo kwa sasa ni kama hadithi za sungura na Fisi.

Ni kweli tunapaswa kuwaheshimu wazazi wetu ili wafurahi na kujiona wanathaminiwa lakini hiyo haitabadilisha chochote kwenye maisha yetu kwa upande wa mafanikio.

Hivi kuna Watu wenye heshima kwa wazazi wao kama Makabila ya Afrika. Au kuna Watu wanaomheshimu Baba kama makabila ya Afrika ikiwemo Wamasai, Wasukuma, Wakurya n.k. embu akaangalie maisha wanayoishi ya Mateso.
Afu aende Ulaya akaone mtoto akimpeleka mzazi asiyewajibika mahakamani alafu hukohuko wanakula Maisha.

Watakuja na kisingizio kuwa furaha ipo moyoni. Sasa huko moyoni mwa mtu kunatuhusu nini sisi wa nje. Hata asiye na furaha moyoni anaweza kusema anayo na usiweze kumbishia kwa sababu humuoni.
 
nilicho gundua humu kuna watoto wengi wa singo mama

humu kuna watoto wengi wana jidanganya watafanikiwa na baba atakuja omba msaada

ila ukienda kwenye jamii, bado watoto lukuki wana watafuta baba zao ili kujua asili yao na ndugu zao pia

ukija huku ukikutana na watoto wa single mama wanajidanganya kwamba watatafutwa wao

kwenye magazeti, redio na mitandao ya kijamii mingi watoto wana tafuta wazazi
 
nilicho gundua humu kuna watoto wengi wa singo mama

humu kuna watoto wengi wana jidanganya watafanikiwa na baba atakuja omba msaada

ila ukienda kwenye jamii, bado watoto lukuki wana watafuta baba zao ili kujua asili yao na ndugu zao pia

ukija huku ukikutana na watoto wa single mama wanajidanganya kwamba watatafutwa wao

kwenye magazeti, redio na mitandao ya kijamii mingi watoto wana tafuta wazazi

Sio kwamba ulichogundua kuwa watoto wengi humu Baba zao waliwatoroka na kuwatelekeza?
 
Inanikumbusha tajiri wa dunia Jeff Bezos wa kampuni ya Amazon baba yake na mama yake walioana wakiwa bado wadogo wakiwa chuoni mama akiwa na umri wa miaka 17 na baba miaka 19 alivyozaliwa baba yake mzazi alikuwa mlevi sana alimtelekeza mama yake na kumpa talaka.Yote shauri ya wote kuwa na akili za kitoto
Mama yake akaondoka na mtoto wake akarudi kwao baadae akapata mwanaume mwingine Mmarekani mwenye asili ya Cuba.Wakati anazaliwa aliitwa Jeff Preston Jorgensen lakini baada ya mama yake kupata mme mwingine akaridhi jina la ubin wa baba wa kambo akaitwa Jeff Bezos.

Kwa maana hiyo alilelewa na baba wa kambo na kumsomesha baba yake wa kibayolojia akaoa mwanamke mwingine.
Katika hali yake ya umasikini baba yake mzazi aliugua sana na ukata mwandishi mmoja akaja kumuambia una habari mwanao wa kibayolojia ni billionea wa dunia? akashtuka sana akasema hivi kumbe huyu kijana bado yupo?.

Akafanya majaribio ya kumuandikia barua mwanawe kumuomba msamaha kwa yaliyopita Jeff Bezos wala hata hakuijibu hiyo barua akaja kufariki mwaka 2015 kwa ugonjwa wa mapafu na majuto mwakubwa mno
 
Inanikumbusha tajiri wa dunia Jeff Bezos tajiari wa dunia wa Amazon alivyozaliwa baba yake mzazi alikuwa mlevi sana alimtelekeza mama yake na kumpa talaka.
Mama yake akaondoka na mtoto wake akarudi kwao baadae akapata mwanaume mwingine Mmarekani mwenye asili ya Cuba.Wakati anazaliwa aliitwa Jeff Preston Jorgensen lakini baada ya mama yake kupata mme mwingine akaridhi jina la ubin wa baba wa kambo akaitwa Jeff Bezos.

Kwa maana hiyo alilelewa na baba wa kambo na kumsomesha baba yake wa kibayolojia akaoa mwanamke mwingine.
Katika hali yake ya umasikini baba yake mzazi aliugua sana na ukata mwandishi mmoja akaja kumuambia una habari mwanao wa kibayolojia ni billionea wa dunia? akashtuka sana akasema hivi kumbe huyu kijana bado yupo?.

Akafanya majaribio ya kumuandikia barua mwanawe kumuomba msamaha kwa yaliyopita Jeff Bezos wala hata hakuijibu hiyo barua akaja kufariki mwaka 2015 kwa ugonjwa wa mapafu na majuto mwakubwa mno

Sio pouwa
 
Back
Top Bottom