Zanzibar: Kanisa la T.A.G pamoja na makazi ya Mchungaji wake Daudi Suna, yamebomolewa na wanaodaiwa ni wakazi wa eneo hilo

Zanzibar: Kanisa la T.A.G pamoja na makazi ya Mchungaji wake Daudi Suna, yamebomolewa na wanaodaiwa ni wakazi wa eneo hilo

misikitini hakufanyiki utapeli
Mkuu Mimi ni muislam,
Lakini kinachofanyika kwa dini zingine ni upuuzi.

Hata kuna Aya zinasema.
Surat kafiroon.
--Enyi makafiri

--Ninacho abudu Mimi.
Sicho mnachoabudu nyie..

--Kila mtu anaabudu anachokiamini.
--nyie mna dini yenu na Sisi tuna dini yetu.

Sasa ya nini kuvunja nyumba za ibada ya Imani zingine?.

Ndy mafundisho ya mtume wetu Muhammad ( SAW)?
 
Una uhakika gani watakua wamebomoa waislamu!!! Ujerumani makanisa yanabomolewa inajengwa misikiti, so watu washaona ukweli na kuhamia upande wa pili.

Naheshimu sana imani ya wengine, lakini linapokuja suala la kulalamikiwa misikiti, misikiti ya Mwenyezi Mungu mara adhana, aisee hatutaelewana mzee.

Viongozi waliopita wa kikafiri kama wangelikuwa na jeuri ya kuzuia adhana wangekipata cha [emoji91][emoji91][emoji91] lakini jeuri hiyo hawana.
Tangu kanisa linajengwa kulikuwa na katazo la kujenga kanisa.

Kila mtu ana Imani na ana abudu kwa Mungu wake.

Mambo ya kuvunjiana makanisa na kuchomeana misikiti ya nn?


Hili ni tukio baya kuliko lile la zamuradi.

Tuone whts comes next kwenye mkono wa Sheria.
 
matapeli wako kila mahali kuna yule maalim alisema kiongozi mmoja marehem ni zaidi ya allah? sio utapeli huo
Sheikh wa mchongo Alhad, kwa namna yeyote Ile ningekuwa muislam nisingekubali yule jamaa asalishe nikiwepo.

Amekaa kitapeli sana Kama gwajiboy
 
Niliiona jana hii habari, sema Wahusika wametulia kwa sababu wanajua walichokuwa wakifanya sio sahihi

Huwezi ukaejenga makanisa na kwenye makazi ya watu na kuwapigia kelele usiku kucha kwa miujiza ya kitapeli

Zanzibar hawapendi ujinga
Ila kujenga msikiti ni sawa? Mbona misikiti tunayokila mahala tena ipo katikati ya watu, kila mara wanapiga hadhana sijui inaandikwa hivyo, usiku saa 10 kila siku wanatuamsha, sema ni ubaguzi wa dini tu ubnafsi.
 
Mm Ni mkiristo sioni sababu huyo mtumishi kwenda kufanya ujenzi ktk maeneo ya wanao ishi waislmu yaani unakwenda uarabuni kufungua kanisa hapan aise. usijaribu Imani za watu haondoke Hapo kbsa Tena ashukuru ajapigwa kipigo kikali mnk hvyo yey ndie mchokozi ..watu wasitafute usaw wa kidini hapa
Kenya umewahi sikia muslami kaw rais au hata kiongoz mkuu hkn hvyo vitu sas na huku iwe Hvyo uwez kwenda kufanya ibada Zanzibar Tena siku hz wamestarabika zamani waliwamwagia tindikali .....
Halafu Kristo huwa anajipigania mwenyewe
 
Mkuu Mimi ni muislam,
Lakini kinachofanyika kwa dini zingine ni upuuzi.

Hata kuna Aya zinasema.
Surat kafiroon.
--Enyi makafiri

--Ninacho abudu Mimi.
Sicho mnachoabudu nyie..

--Kila mtu anaabudu anachokiamini.
--nyie mna dini yenu na Sisi tuna dini yetu.

Sasa ya nini kuvunja nyumba za ibada ya Imani zingine?.
Ndy mafundisho ya mtume wetu SAW?
Wewe muislamu jina
 
Mm Ni mkiristo sioni sababu huyo mtumishi kwenda kufanya ujenzi ktk maeneo ya wanao ishi waislmu yaani unakwenda uarabuni kufungua kanisa hapan aise. usijaribu Imani za watu haondoke Hapo kbsa Tena ashukuru ajapigwa kipigo kikali mnk hvyo yey ndie mchokozi ..watu wasitafute usaw wa kidini hapa
Kenya umewahi sikia muslami kaw rais au hata kiongoz mkuu hkn hvyo vitu sas na huku iwe Hvyo uwez kwenda kufanya ibada Zanzibar Tena siku hz wamestarabika zamani waliwamwagia tindikali .....
Utakuwa mkristo wakubumba, umehamia sehemu hakuna kanisa kwahiyo usifanye ibada kisa hapa nikwa waslamu? Ulitaka ahamie msikitini? Wewe si mkristo!
 
Wewe muislamu jina
Kila mtu ana anachoabudu..
Kwa Imani yake.

Nini kufatana fatana?

--Wewe baki na imani yako kwamba Yesu ni Mungu jr ..

--waislam wabaki na Imani yao kwamba Nabii Muhammad (SAW) Mtume wa Mungu.

Na Allah ndy mmiliki wa mbinu/ardhi na vilivyomo..

Yanini malumbano ya kuvunjiana makanisa?
 
Kanisa la T.A.G pamoja na makazi ya Mchungaji wake Daudi Suna yamebomolewa na wanaodaiwa ni wakazi wa eneo hilo wakishinikiza kuwa hawataki Kanisa katika eneo lao.

Hii ni kunyume kabisa na sheria za nchi zinazoruhusu Uhuru wa Kuabudu. Kama jambo halitafanyika basi ni wazi kuna kiongozi mbaguzi wa dini anaewalinda wabomoaji na pia hii itachochea sehemu nyingine makanisa na makazi ya wachungaji kubomolewa.

Pia miezi michache ijayo kipindi cha mfungo kikianza huwa ni marufuku kwa wakristo kula sehemu za wazi, ukikutwa unafungwa mpaka mfungo uishe, wengine huwa wanapigwa sana, sasa hapa ni kwamba mtu kama umeamua kufunga kwa imani yako iwaje hutaki kuona wenzako hawali, ni kwamba imani yako no nyepesi sana kuisimamia, kama ni hivyo kuna haja gani ya kufunga.

View attachment 2146530

View attachment 2146523

============================================

Taarifa uhakika juu ya tukio hilo ni kuwa Mchungaji David Victor Suna ni mzaliwa wa Sumbawanga, lakini kwa miaka mingi amekuwa akiishi Zanzibar baada ya familia yake kuhamia huko. Kaka yake naye ni mtu wa kanisani lakini anafanya shughuli zake Dar es Salaam.

Alipoanza harakati za kutafuta eneo kwa ajili ya kanisa alipata wakati mgumu kwa kuwa walikuwa wanamkatalia, baadaye akabadili gia na kutafuta eneo la kununua la kwake binafsi na siyo kwa ajili ya kanisa.

Baada ya kutafuta eneo lake binafsi ndipo akapata eneo hilo lililopo Sebleni, Unguja. Akanunua kwa Sh 16,000,000 (milioni 16) akalipa fedha taslimu, akasaini mkataba rasmi wa mauziano (tazama picha), japokuwa katika eneo hilo alikuta mmiliki tayari amejenga banda ambalo nalo lilikuwa sehemu ya mkataba wa manunuzi.

Baada ya kununua akajenga ukuta kuzungushia eneo husika kisha akaanza shughuli zake za ibada, baada ya majirani kubaini kuwa mnunuzi ameanzisha kanisa eneo hilo ndipo mgogoro ulipoanzia.

Wakamwabia hatakiwi kuwa na kanisa eneo husika lakini David Victor Suna akashikilia msimamo wake kuwa ataendelea na shughuli zake za kanisa.

Mhusika ambaye aliuza eneo hilo naye akamvaa David Victor Suna na kumtaka arejeshe eneo hilo kwa kuwa hakuuza kwa ajili ya kanisa bali kwa ajili ya kujenga makazi, bado David Victor Suna akagoma kubadilisha matumizi wala kurudisha eneo.

David Victor Suna akawa asisistiza kuwa yeyote mwenye malalamiko aende Mahakamani ambapo haki itatendeka, hata waliposhirikisha Serikali za mtaa nao wakawa wanamshawishi ama kubadili matumizi au kurejesha eneo, msimamo ukawa ni uleule.

Ndipo siku ya tukio, lilikuka bulldoza likaanza kuvunja eneo husika wakati wahusika wakiwepo wachache wakiendelea na ibada kama kawaida, kanisa likavunjwa na baadhi ya vitu vikiwemo viti vikaharibiwa na gari hilo.

Mamlaka za Serikali za mtaa hazijawa tayari kuzungumzia tukio hilo, naye David Victor Suna amekuwa mgumu kuzungumzia kinachoendelea kwa kile kinachodaiwa hajatulia hadi sasa.

SERIKALI YAINGILIA
Taarifa zinaelezwa kuwa Mkuu wa Wilaya wa eneo husika anatarajiwa kutolea ufafanuzi suala hilo mchana wa leo Machi 11, 2022.

Nitarudi kuwapa kilichoendelea kuhusu tamko la Serikali.

ITAENDELEA...
View attachment 2146667
View attachment 2146668
View attachment 2146670
View attachment 2146671 View attachment 2146672
Nitafute ili nitoe mchango wangu hadi haki ipatikane, inauma sana
 
Kwann dini ya kiislamu huwa inaogopa Sana competition ya kiimani. Je ni dhaifu dhidi ya imani zingine?
Maana ni nature imani yeyeto dhaifu huwa inamezwa na imani imara.
Mfano dini za weupe zilikuwa na nguvu zaidi hadi zikazimeza dini za asili.
Huez kijenga nyumba ya ibada mahala popote unapojisikia,dini ya islam ilikuja miaka mingi mbele ya dini mnayoita ukristo ingekuwa inaogopa competition isingezaliwa,tumia akili ktk kufikiri!!
 
Marko 6:3 “HUYU SI YULE SEREMALA, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda, na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake”.
Kwani ufundi selemala na fundi mjenzi nikitu kimoja?
 
Hii iko kwa pande zote hata wakristo huwa tunapiga vita uislam baadhi ya maeneo.

Mimi ni mwenyeji wa kibosho Moshi, walitokea waislam katika kijiji kimoja kinaitwa Mweka ambapo kuna taasisi kama Chuo cha wanyamapori, geti la kushukia watalii kutoka Mt kilimanjaro, mashule nk, hivyo wakataka kujenga misikiti ili waweze kuswali karibu maana misikiti upo moshi mjini.

Waliponunua eneo na kumwaga tofali na mchanga, fitna zikaanza na padre akasema kanisani mnakubalije misikiti hapa, kilichotokea ni vita mpaka mradi ukafa.

Nafikiri Watu wa dini zote wanahitaji kustaarabika na kuelewa kwamba tunatakiwa tuishi wote kwa kuchukuliana.
Lakini kesi hizo ni nyingi kama za wenzetu?
 
Back
Top Bottom