Zanzibar ni nchi huru au ni sehemu ya Tanzania?

Zanzibar ni nchi huru au ni sehemu ya Tanzania?

Ukinambia ni sehemu ya Tanzania nitakuuliza maswali yafuatayo:

1. Kwanini Watanganyika hawaruhusiwi kumiliki ardhi Zanzibar?

2. Kwanini ni ngumu ajira za Zanzibar kuhusisha Watanganyika?

3. Kwanini wana rais wao na bendera yao?

4. Kwanini wana taasisi zao zinazojitegemea kama mahakama, bunge, tume ya uchaguzi nk?

5. Kwanini timu za Zanzibar zinaiwakilisha Zanzibar kama nchi kwenye mashindano mbalimbali ya CAF kwa ngazi ya vilabu?

6. Kwanini taasisi zao zinaendeshwa tofauti kabisa na Tanzania, mfano kule watu wanatibiwa bure kwa hospitali za serikali, gharama za umeme ni nafuu sana nk?

Ukinambia Zanzibar ni nchi huru nitakuuliza maswali yafuatayo:

1. Kwanini haina amiri jeshi mkuu kwa maana ya kwamba haina jeshi linalojitegemea?

2. Kwanini Tanzania ikikopa Zanzibar wanapata fungu lao tena kwa uwiano usio sawa (Zanzibar inapata ratio kubwa) huku ikiwa mlipaji wa mkopo akiwa Tanzania bara pekee.

3. Kwanini haina sarafu yake yenyewe?

Mtazamo wangu: Muungano una mapungufu mengi.

Huwezi kuwa na Nchi ambayo kuna wakati inakuwa nchi kamili na kuna wakati inakuwa sehemu ya nchi nyingine.

Nadhani ni muda sahihi Zanzibar kuwa mkoa wa Tanzania, ama tuwaachie nchi yao wajitegemee.

Inavyoonekana ni kuwa Nyerere alitaka kuwalaghai Wazanzibari mwisho wa siku akajikuta anatengeneza muungano usioeleweka na sasa madhara yake yapo dhahiri.

Hoja ya usalama kwangu haina mashiko! Kama tumeweza kuilinda mipaka yetu yote dhidi ya nchi korofi zinazotuzunguka tutashindwaje kujilinda dhidi ya Zanzibar?
Kabla ya mama kero za muungano zilikuwa zinaikera Zanzibar, mama alipoingia kero za muungano akazimaliza kimya kimya ndani ya dakika sifuri na hapo hapo zikaibuka kero za muungano kwa upande wa Tanganyika!! Ni nani mwenye ubavu wa kuzisemea kero za muungano kwa upande wa Tanganyika!! Wengi waliopo hata wanaona aibu au wanaogopa kujiita watanganyika!!
 
Mimi sijasema jina lakini inaonyesha wewe unajua zaidi
Top manyota ni yeye mwenyewe hakuna cha uremote wala nini ! Labda huwa anaomba ushauri ushauri tu maana hilo likazi nalo ni gumu linahitaji uzowefu na ujasiri mkubwa !!
 
Kabla ya mama kero za muungano zilikuwa zinaikera Zanzibar, mama alipoingia kero za muungano akazimaliza kimya kimya ndani ya dakika sifuri na hapo hapo zikaibuka kero za muungano kwa upande wa Tanganyika!! Ni nani mwenye ubavu wa kuzisemea kero za muungano kwa upande wa Tanganyika!! Wengi waliopo hata wanaona aibu au wanaogopa kujiita watanganyika!!
Mkubwa huwa anaogopa kuchekwa akisema anaonewa na mdogo wake !!
 
Kabla ya mama kero za muungano zilikuwa zinaikera Zanzibar, mama alipoingia kero za muungano akazimaliza kimya kimya ndani ya dakika sifuri na hapo hapo zikaibuka kero za muungano kwa upande wa Tanganyika!! Ni nani mwenye ubavu wa kuzisemea kero za muungano kwa upande wa Tanganyika!! Wengi waliopo hata wanaona aibu au wanaogopa kujiita watanganyika!!

Kero
Za muungano haziwezi kuisha kwa Zanzibar kwani hiyo Zanzibar yenyewe ipo ipo Tu kifigisu figisu.
Msikilize
 
Top manyota ni yeye mwenyewe hakuna cha uremote wala nini ! Labda huwa anaomba ushauri ushauri tu maana hilo likazi nalo ni gumu linahitaji uzowefu na ujasiri mkubwa !!
Mbona unajaribu kukimbia Na ulishatumwagia punje Za mtama kidogo
 
Kabla ya mama kero za muungano zilikuwa zinaikera Zanzibar, mama alipoingia kero za muungano akazimaliza kimya kimya ndani ya dakika sifuri na hapo hapo zikaibuka kero za muungano kwa upande wa Tanganyika!! Ni nani mwenye ubavu wa kuzisemea kero za muungano kwa upande wa Tanganyika!! Wengi waliopo hata wanaona aibu au wanaogopa kujiita watanganyika!!

 
Mbona unajaribu kukimbia Na ulishatumwagia punje Za mtama kidogo
Zile ni speculations tu sidhani kama zina ukweli !! Lakini pia inawezekana ! Ila mimi sijui !! Lakini kama itakuwa kweli ni yeye mwenyewe amependa iwe hivyo! Maana katiba inampa madaraka yote yeye sio mtu mwingine yeyote !! Na wala sio kwa hisani ya mtu au taasisi yeyote !! Yeye ni Top kwa mujibu wa katiba ya Nchi na si vinginevyo !!
 
Zile ni speculations tu sidhani kama zina ukweli !! Lakini pia inawezekana ! Ila mimi sijui !! Lakini kama itakuwa kweli ni yeye mwenyewe amependa iwe hivyo! Maana katiba inampa madaraka yote yeye sio mtu mwingine yeyote !! Na wala sio kwa hisani ya mtu au taasisi yeyote !! Yeye ni Top kwa mujibu wa katiba ya Nchi na si vinginevyo !!
Katiba Si inafuatwa kwa vile vitu vinavyopendwa Na Wazee wa CCM vyenginevyo mambo mengi yanafanywa kinyume Na katiba
 
Zanzibar ni mkoa mmojawapo wa Tanzania, sema umepewa heshima ya kipekee kwasababu umezungukwa na bahari halafu Kuna waislamu wengi.
 
Zanzibar ni mkoa mmojawapo wa Tanzania, sema umepewa heshima ya kipekee kwasababu umezungukwa na bahari halafu Kuna waislamu wengi.
Huo uislamu ndio lengo tokea kuja wazungu, ingalikuwa ZNZ ni nchi ya kikristo isingalivamiwa Na Tanganyika chini ya msaada wa Waingereza
 
Ndivyo älivyokuambia?
Basi angegoma mapema..mbona alikubali hadi umauti umemkuta akiwa makamu...na nzuri zaidi ndiye aliyeomba watanganyika waje kumsaidia dhidi ya utawala ma kisultani usirudi tena zenji.

#MaendeleoHayanaChama
 
Basi angegoma mapema..mbona alikubali hadi umauti umemkuta akiwa makamu...na nzuri zaidi ndiye aliyeomba watanganyika waje kumsaidia dhidi ya utawala ma kisultani usirudi tena zenji.

#MaendeleoHayanaChama

Kumbe umeelewa ila unatafuta ligi , hivi alipoomba ulikuwepo au alikuambia wewe tu?
 
Katiba Si inafuatwa kwa vile vitu vinavyopendwa Na Wazee wa CCM vyenginevyo mambo mengi yanafanywa kinyume Na katiba
Labda kwa mambo madogo madogo sio kwa jambo kubwa kama hilo !
 
Back
Top Bottom