Zanzibar: Serikali yalaani vitendo vya unyanyasaji wa kidini vinavyoendelea visiwani

Zanzibar: Serikali yalaani vitendo vya unyanyasaji wa kidini vinavyoendelea visiwani

Hatupaswi kubaguana; sisi ni wamoja na Muungano ni Tunu yetu.

Upande wa pili wanashindwa kuwa wavumilivu.
Hakuna asiyejua kuna imbalance kwenye Muungano. 1). Ni Watanganyika kukubali kupoteza Utanganyika wao mithili ya mwanamke aliyeolewa anavyopoteza utambulisho wa ukoo wao. 2). Sheria za umiliki wa ardhi ambapo Mzanzibari anaruhusiwa kumiliki ardhi kama mtanganyika tu ila si hivyo kwa mtanganyika akiwa Zanzibar. 3). Sheria za forodha pia kuna shida; 4). Marejesho ya mikopo na matumizi ya mikopo ya nchi; nk.
Mambo yote yanaipendelea Zanzibar.

Sasa inapotokea Mtanzania wa upande wa Tanganyika kuwa mistreated inatuuma na kutufanya tuoji huu Muungano. Mbona Wazanzubar waishio Tanganyika hawana hiyo kasumba ya kunyanyasa Watanganyika?

Hii haitokei kwa bahati mbaya. Tunaomba rais wa Zanzibar ambaye kiutawala ni kama mkuu wa mkoa akemee kwa sauti kubwa hivi vitendo vya uvunjifu wa Amani.

Tunamuomba pia rais wa JMT, ambaye ndiye Amiri Jeshi Mkuu, Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama wa Tanzania akemee pia hivi vitendo viovu vinavofanyika Zanzibar vikalenga Watanganyika.

Tunaupenda Muungano, yatupasa tuendeleze upendo.
 
imeandikwa kimchongo!

ingekataza upande mmojaa kuonea wengine! mfano ingesema muislam akimuona mkristu anakula hadharani amuonyeshe mahali pa kujificha ale! na akikataa basi hakuna haja ya kumlazimisha! hii ni kuonyesha ukomavu wa uislam!
Kwanza kula haijawai kuwa dhambi, siyo kosa kisheria na Wakristu waishio Tanzania hawapashwi kujificha wanapokula. Mbona Tanganyika hatuna hizo na mifungo inaendelea tu?
 
Ndiyo ajabu hiyo wanajifanya wacha Mungu huku vinyeo viko wazi kwa luingiliana kinyume cha maumbile.
Juzi katikati ya jan kuna wale walikamatwa wanapigana vipande vya nyama ngumu kwenye mapagale wakapelekwa polisi usiku wakaendeleza mchezo huo wakiwa mule mule selo.

Hao jamaa ni wa kipekee sana
 
Ukisikia mtu anaandika kitu, ila ukisoma ni kama hajaandikaa kitu. Yaani inakuwa kama (1- 6 + 5 -7 + 3 + 4) = 0
Hapa alikuwa anaandika anafuta, anaandika tena anafuta. Akaona amechoka ila kuna shinikizo ya kuandika ikabidi aiachie hivyo hivyo 🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kuzibuana mitaro ruksa na si dhambi! Dhambi ni kula hadharani kwa asiyemwislamu wakati mmefunga mfungo wenu! Swaini!
 
Walishatuona na wananchi ni watoto?

Sasa hapo kutoa tamko walikua wapi? Je waliokamata hao watu watachukuliwa hatua?
 
Juzi katikati ya jan kuna wale walikamatwa wanapigana vipande vya nyama ngumu kwenye mapagale wakapelekwa polisi usiku wakaendeleza mchezo huo wakiwa mule mule selo.

Hao jamaa ni wa kipekee sana
Wachafu sana hawa wala urojo. Hata yule askari FFU ambaye video zake alifukuliwa mtaro zilivuja aliachiwa na kurudishwa kazini.
 
View attachment 2949080

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imehimiza katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan kutenda mema na kudumisha amani, umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi.

Zanzibar ni nchi yenye historia kongwe ya uvumilivu wa kidini ambapo Uislamu na Ukristo uliingia mapema kuwa sehemu muhimu ya utamaduni uliodumu kwa karne nyingi. Hii inatufundisha kuhusu ustaarabu wa Wazanzibari kuvumiliana kidini na ndio msingi wa mshikamano miongoni mwetu.

Serikali inalaani vitendo vya unyanyasaji vinavyoendelea kufanyika sehemu mbalimbali Zanzibar, kadhia hiyo ni kinyume na misingi ya kuvumiliana katika imani za kidini.

Aidha, Serikali inawahimiza wananchi kujizuia kwa namna yoyote ile kuingilia uhuru wa mtu binafsi katika kuabudu.

Ikumbukwe Zanzibar inaongozwa kwa Katiba, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ina mamlaka ya kullinda Katiba ya nchi na watu wake, hivyo hatua yoyote ile yenye kuhatarisha Umoja, Amani na Mshikamano haitavumiliwa.

Serikali itaendelea kulinda haki na uhuru wa mtu kuabudu kama ilivyoelezwa katika Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

Hivyo, tuendelee kudumisha amani na upendo kama mafundisho ya dini zetu yanavyotutaka, tofauti zetu za kidini zisiwe chanzo cha kuvuruga amani, umoja na mshikamano.
Huu ni ushahidi kuwa masuala ya imani huchangia sana kuua fikra tunduizi. Na kukosa fikra tunduizi kuna gharama kubwa. Paul na Elder(2009) waliwahi kusema "Shoddy thinking is costly,both in money and in quality of life." Inasikitisha sana.
 

Attachments

  • inbound6030463211047220982.jpg
    inbound6030463211047220982.jpg
    212.7 KB · Views: 1
kimsboy jitahidi uwe unatumia akili. Hakuna Katiba ambayo mla hadharani anavunja.

Mkiruhusu watu waishi kama wanyama kujiamua sheria mkononi ni hatari hata kwa dini yenyewe.

Mimi jana nimeshinda sehemu na mafundi. Wamefunga lakini wanatukana kuanzia asubuhi mpaka jioni. Kisha wanaitisha futari wanafuturu.
Shetani hajawahi kuwa mwema..
 
Back
Top Bottom