Ziara ya Raisi Mbona hawa wananchi hawaelezi kero zao

Ziara ya Raisi Mbona hawa wananchi hawaelezi kero zao

Wandugu nawashangaa hawa wananchi wanaotembelewa na Raisi Samia siwasikii wakieleza kero zao wamesimama tu kama makatuni flani hivi,hawajielewi au wametishwa.View attachment 2316818
 
Ile hotuba wakati wa uzinduzi wa barabara ya Chunya makongorosi watu walikua wamekaa kimya wanasubiri kusikia jambo flani hivi yaani ukiwatazama sura zao utawaelewa.

Huwa nacheka sana kusikia eti rais ataongea na wananchi, kisha kinachofanyika ni yeye kuwahutubia, na ikitokea mtu akauliza jambo unakuta ni wa mchongo!

Sasa huwa najiuliza kwanini kutumia fedha nyingi, na vitisho vya chama dola ili watu wajae kwa lengo la kuhadaa umma kuwa unakubalika, huku huna uwezo wa kutimiza mahitaji ya watu?
 
Alipojaribu kumpa nafasi kijana wa kike kuuliza swali akapigwa swali umeme kuunganisha bei kubwa ya laki 3 wanataka elfu 27 .........,,
 
Back
Top Bottom