Zijue Mbinu Hizi za Kuwa Tajiri("Milionea")

Zijue Mbinu Hizi za Kuwa Tajiri("Milionea")

7. Ukianza kupata utajiri, wafundishe wengine mbinu ulizotumia
Andika vitabu, uza. Wafundishe wengine masuala ya kifedha kwenye semina, warsha, makongamano, kwa malipo.
Bahati Mbaya sana Wanaofundisha kwenye hizo Semina na Warsha na wao hawana hela wanategemea kiingilio unacholipa ndio wale ugali dagaa watoto waende chooni.

Mi nadhani Utajiri una mbinu nyingjne kuliko hizi bla bla za vitabuni

Watu tumesoma Hadi Rich Dady Poor Dady lakini bado
 
Kwani we ni tajiri?!...labda tuanzie hapo...
  1. Kocha wa timu ya mpira si lazima awe mchezaji bora, lakini anaweza kufundisha wachezaji wakawa mabingwa. Hii inaonyesha kuwa mtu anaweza kufundisha mbinu za kupata utajiri hata kama yeye hajaupata utajiri.
  2. Daktari wa afya hajawahi kuugua magonjwa yote anayoyatibu, lakini bado anawasaidia wagonjwa kupona. Hii inadhihirisha kuwa kufundisha hakuhitaji mtu awe na uzoefu wa hali halisi.
  3. Na mimi najifunza ku-apply mbinu hizi. Naamini baada ya muda fulani "nitatoboa".
  4. Utajiri huanza na maarifa. Nimeamua kuwa tajiri wa maarifa kwanza, ili mapesa yafuate baadaye.
Waswahili wanasema: "kizuri kula na mwenzio." Kwakuwa mbinu nilizozieleza zina ukweli kwanini niwe mchoyo nisiwasaidie wengine wanaotamani kuwa matajiri. Nikiwa tajiri peke yangu, watu wengi watakuja kuniomba msaada. Tukiwa matajiri wengi................ jazia...
 
Watu wengi wana ndoto za kuwa matajiri. Wanafanya kazi kwa bidii usiku na mchana ili wawe matajiri. Hata hivyo ni wachache wanaofanikiwa kuupata utajiri. Leo nakutajia baadhi ya mbinu muhimu za kupata utajiri au kuwa milionea/bilionea – sizungumzii utajiri unaopatikana kwa bahati au kwa kurithi.

Utajiri unapatikana kwa kutumia mbinu sahihi, nidhamu, na uthabiti. Kama kweli unataka kuwa tajiri, tumia mbinu hizi:

1. Anza kuwa na mtazamo(mindset) wa utajiri
Utajiri huanzia kwenye mawazo. Watu matajiri huifikiria pesa tofauti na watu wa kawaida. Ili kujenga mtazamo wa utajiri fanya hivi:
  • Matumizi yako ya pesa yawe ya chini kuliko kipato chako(spend less than you earn)
  • Weka malengo ya kifedha ya muda mrefu.
  • Kaa katikati ya watu wenye mafanikio na maarifa ya kifedha.
2. Weka pesa benki na wekeza kwa hekima
Kuweka pesa benki peke yake hakutakufanya uwe tajiri, lakini ukiwekeza utafanikiwa. Kwahiyo badala ya kuweka pesa zako zote benki:
  • Wekeza kwenye hisa, dhamana, au mifuko ya pamoja. Kabla ya kuwekeza fanya utafiti.
  • Anzisha biashara yenye uwezo wa kukua.
  • Wekeza kwenye mali isiyohamishika(real estate) au mali nyingine zenye thamani inayoongezeka.
3. Uwe na vyanzo vingi vya mapato
Chanzo kimoja tu cha mapato hakitoshi sana kama unataka kupata utajiri mkubwa na wa kudumu. Watu matajiri hupata pesa kutoka kwenye vyanzo vingi vya mapato kama vile nyumba za kupangisha, gawio(dividents), au mirahaba(royalties), biashara za mtandaoni nk.

4. Dhibiti fedha zako vizuri
Huwezi kuwa tajiri kama utashindwa kudhibiti au kusimamia fedha zako. Kwahiyo:
  • Uwe na bajeti na ufuatilie(track) matumizi yako.
  • Epuka madeni yasiyo ya lazima na tumia pesa kwa busara.
  • Uwe na akiba ya dharura(emergency fund) ili uweze kuyakabili matukio au hali zisizotarajiwa.
5. Elimu haina mwisho. Jifunze tena na tena masuala ya kifedha
Dunia ya kifedha inabadilika kila wakati. Watu matajiri huendelea kujifunza kwa:
  • Kusoma vitabu kuhusu utajiri na usimamizi wa fedha.
  • Kuhudhuria semina za biashara na uwekezaji.
  • Kujifunza kutoka kwa washauri na wataalamu wa fedha.
6. Uwe mvumilivu (be patient and persistent)
Utajiri hauoti kama uyoga. Wajasiriliamali wengi walichukua miaka kadhaa kuwa matajiri. Hivyo uwe mvumilivu, na usikate tamaa unapokutana na changamoto.

7. Ukianza kupata utajiri, wafundishe wengine mbinu ulizotumia
Andika vitabu, uza. Wafundishe wengine masuala ya kifedha kwenye semina, warsha, makongamano, kwa malipo.

Ukishakuwa tajiri usimsahau Mungu.
Nawe utakula ushibe, utamshukuru BWANA, Mungu wako... jihadhari, usije ukamsahau BWANA, Mungu wako, kwa kutozishika amri zake, na hukumu zake, na sheria zake...( Kum 8:10-11).

Ukimsahau Mungu Maandiko haya yanaweza kukuhusu:
“Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo. Akawaambia mfano, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana; akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje?

Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu. Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu. Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi. Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanaitaka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani? Ndivyo alivyo mtu anayejirundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu.”( Luka 12:15-21)

View attachment 3236711
Asante sana kwa maarifa haya.
Hakika watakaoyaamini watavuka,lakini wanaoamini kuwa huwezi kutajirika bila kutokea familia ya kitajiri watayapita tuu.
 
Ukitaka kuwa Tajiri pamoja na yoteee MGANGA
Mganga.jpg

Waganga wa kienyeji ni maajenti wa shetani. Wanapokuambia watakupa utajiri lengo lao ni ili umwabudu shetani. Na ukimwabudu shetani maana yake tayari umejiingiza katika kundi la watakaotupwa katika moto wa milele. Shetani alimwambia pia Yesu amuabudu ili ampe fahari ya ulimwengu.
Mt 4:8-10
Kisha Ibilisi akamchukua mpaka juu ya mlima mrefu, akamwonesha falme zote za ulimwengu na fahari zake, akamwambia, “Hivi vyote nitakupa kama ukipiga magoti na kuniabudu.” Hapo, Yesu akamwambia, “Nenda zako Shetani! Imeandikwa: ‘Utamwabudu Bwana Mungu wako
na kumtumikia yeye peke yake.’”

cc: Mahondaw Kiranga Mshana Jr Infropreneur Demi FaizaFoxy
 
View attachment 3236975
Waganga wa kienyeji ni maajenti wa shetani. Wanapokuambia watakupa utajiri lengo lao ni ili umwabudu shetani. Na ukimwabudu shetani maana yake tayari umejiingiza katika kundi la watakaotupwa katika moto wa milele. Shetani alimwambia pia Yesu amuabudu ili ampe fahari ya ulimwengu.
Mt 4:8-10
Kisha Ibilisi akamchukua mpaka juu ya mlima mrefu, akamwonesha falme zote za ulimwengu na fahari zake, akamwambia, “Hivi vyote nitakupa kama ukipiga magoti na kuniabudu.” Hapo, Yesu akamwambia, “Nenda zako Shetani! Imeandikwa: ‘Utamwabudu Bwana Mungu wako
na kumtumikia yeye peke yake.’”

cc: Mahondaw Kiranga Mshana Jr Infropreneur Demi FaizaFoxy
Unaweza kuthibitisha kuwa shetani yupo kweli na hizo habari za shetani kuwapo si hadithi za ujinga za mapokeo tu?
 
Kwa Afrika, utajiri halali uko shambani na kwenye mifugo
 
View attachment 3236975
Waganga wa kienyeji ni maajenti wa shetani. Wanapokuambia watakupa utajiri lengo lao ni ili umwabudu shetani. Na ukimwabudu shetani maana yake tayari umejiingiza katika kundi la watakaotupwa katika moto wa milele. Shetani alimwambia pia Yesu amuabudu ili ampe fahari ya ulimwengu.
Mt 4:8-10
Kisha Ibilisi akamchukua mpaka juu ya mlima mrefu, akamwonesha falme zote za ulimwengu na fahari zake, akamwambia, “Hivi vyote nitakupa kama ukipiga magoti na kuniabudu.” Hapo, Yesu akamwambia, “Nenda zako Shetani! Imeandikwa: ‘Utamwabudu Bwana Mungu wako
na kumtumikia yeye peke yake.’”

cc: Mahondaw Kiranga Mshana Jr Infropreneur Demi FaizaFoxy
Sijakuelewa kabisaaa
Tunazungumzia MOTO au PESA??.

#YNWA
#YANGA_BINGWA
 
Back
Top Bottom