Zitto akosoa wasifu wa Membe kuacha uanachama wake ACT-Wazalendo. Alaani walioshiriki kumchafua kupitia magazeti

Inaonekana Zitto ana uchungu sana na alimpenda sana mwendazake, huko nyuma aliwahi kusema wanaompenda mwendazake wakazikwe nae huko na sasa nae zamu yake imefika, aach porojo aonyeshe mfano wa kupenda kwa vitendo.
 
Kumbe wewe humjui huyu Mrundi, anajua sana kujipendekeza kwa wakubwachuki kwa mwendazake ilianza pale alipojitoa ufahamu wakati wenzake walisusia ufunguzi wa bunge yeye akabaki mjengoni na akapongeza sana na mwendazake, yeye alidhani mwendazake atampa uwaziri wa nishati na madini lakini mwendazake akamshiti wakati yeye alijua ataukwaa uwaziri aikiweka historia kama waziri kutoka upinzani, maono na ndoto zake zikafa kibudu na hapo ndipo chuki ikaanza.Huyu jamaa alitolewa kwenye kamati ya bunge ya mashirika ya umma baada ya kubainika kuwa alifanya mtaji wa kujipatia mlungura, na kuna wakati alitiahidi kuwataja walioficha pesa Uswisi lengo ilikuwa awa blackmail hao wenye vijisenti. huyu jamaa amebaki kusafiria nyota ya matukio, ni mjanja tu wa mjini.
 
Kwani uongo, hao tiss sio kutumika tu kutukana viongozi, bali ndio walitumika kuharibu chaguzi za nchi hii kipindi chote cha dhalimu. Huo ni ukweli ulio wazi na Zito kausema tu kukazia ukweli huo.
Vipi uchaguzi wa 2010 ulikua halali?
 
Kwamba Zittow hakumsikia membe akikana kuwa hakuwahi kuwa mwanachama WA ACT?
 
Ulikuwa na afadhali kuliko ule uhayawani wa dhalimu wa 2020.
Tunaongelea uhalali, Nyeusi ni nyeusi na nyeupe ni nyeupe. Uchaguzi ulikua halali au si halali?Nilishuhudia akina mahanga wakiwa na mabox ya kura.Sasa kwanini ujitoe ufahamu na kufanya jambo la wizi wa kura kaleta Magufuli?CCM ndio wanaamua nani awe Rais,mbunge au diwani na wapi.Hata uchaguzi ujao wataamua hivohivo, Wakitaka mbeya yote iwe ccm wanafanya na hakuna wa kupinga, Wakitaka Sugu apewe nusu mkate wanafanya. 2025 kuna majimbo upinzani watachukua na hii itakua hisani ya ccm,si umemsikia boss wako Lisu?
 

Magufuli hakuiba kura usichanganye boss, Magufuli alinajisi uchaguzi. Nakupa mfano mmoja, huwa kuna ajali za meli ziwani, lakini huwezi kusema ajali ya MV Bukoba ilikuwa ni kawaida eti kisa huwa kunatokea ajali nyingine huko ziwani.

Ni kweli CCM kwa kushirikiana na vyombo vya dola inaweza kupora uchaguzi, na kuamua nani atangazwe mshindi. Lakini hii sio sifa bali ni upuuzi, nashangaa unapoiongelea kama ni sifa.
 
Haijachafuliwa Bali ilijichafua yenyewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…