Zitto ataka wanaoikosoa ACT-Wazalendo waanzishe chama chao

Zitto ataka wanaoikosoa ACT-Wazalendo waanzishe chama chao

They will never get peace kwa kusaliti big course

Yaani hawa jamaa wameiondolea serikali ya CCM pressure kubwa ya ndani ya nchi na hata ya nje ambayo ingewaminya wafanye reforms fulanifulani za msingi.

Yaani ACT wamewazawadia CCM zawadi ya uaminifu kwa mchakato haramu na feki wa uchaguzi na kwa kufanya hivyo wameihakikishia CCM kuwa hakuna consequences zozote watakazozipata hata wakirudia michezo yao hiyo kwenye chaguzi zijazo!. Kwa kweli hakuna usaliti mbaya kama huu kwa future ya demokrasia ya nchi hii!.

Yaani kacheo kisicho na kichwa wala miguu cha Maalim na pengine "behind the scene deals ikiwemo hongo" vimesababisha hawa watu wasaliti movement nzima ya kuiminya CCM ifanye reforms za maana kwenye tume ya uchaguzi

Inasikitisha sana.
Imenichukua takriban wiki moja kusoma malalamiko ya wote dhidi ya maamuzi ya ACT kujiunga SUK.

Nilichokuwa nasubiri ni kuona hao watu wanakuja na solution/mapendekezo juu ya nini ACT wazalendo wangekifanya baada ya hapo kama wasingejiunga na SUK! Well kuna baadhi ya wanachadema wamekimbia nchi- Sijui kama hilo ndio jibu! Lakini ni hatua mojawapo, muda utatuonyesha. Kuna covid-19 ikaamua kuapishwa na spika- nayo ni hatua mojawapo ambayo kikundi fulani kimeona ni dawa ya kubadili mtazamo wa CCM. Mimi naamini kuwa yote haya yanafanyika kwa nia njema sana ya kubadili mbinu za CCM mbele ya wapinzani.

Ni ukweli usiofichika kuwa mbinu ya kuwaingiza wananchi barabarani ilishindikana, kwa vile watawala walitumia nguvu za ziada za kukabiliana na wananchi. Swali linabaki pale pale, tunafanya nini katika hatua ijayo. Sijasikia lolote toka kwa CHADEMA zaidi ya kudeal na covid-19 na waliokimbia nchi.

Binafsi sikilaumu chama chochote kile kwani yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi ni mshtuko mkubwa kwa kila chama. Hakuna aliyejua watawala wangeenda mbali namna hii bila aibu mbele ya macho ya waangalizi wa nje na ndani. Hakukuwa na haiba kabisa, ni ubabe wa aina yake.

Katika wakati kama huu, ili kuwaunganisha wanachama wa kila chama kunahitajika kurudi nyuma kwanza hatua kadhaa ili kujipanga upya. Ni strategy muhimu sana hii katika uwanja wa vita, vinginevyo mtamalizwa wote na msiwe na askari hata wa kupiga kelele. Hivyo kwangu alichokifanya ACT ni kurudi nyuma na kujipanga upya. Tunasubiri move ya CHADEMA, kwani sijaisikia!

Hata hivyo nyie mnaolaumu bado mna nafasi ya kueleza ACT wangefanya nini? Tiririkeni!
 
Unaijuia na kuilewa dolla Milioni 1 US kwanza au unataja tu namba ? Ungeanza na kuilewa US Dola laki moja kwanza , Zito kabwe alipwe 5 million USD halafu aendelee kuganga njaa kwenye Siasa zisizo na mbele wala nyuma ? Unajua chadema walikuwa wanalipwa ruzuku kiasi gani na Serikali kwa mwezi ? Anzia hapo halafu labda utapata idea ya 5 million USD ni nini, labda kwa kukusaidiatu kama chadema walilipwa shilingi milioni 300/mwezi hiyo hiyo haifiki hata dola laki moja na nusu achilia mbali dola laki tano na wala sijagusia dola laki 7, 8, 9 mpaka 1 million USD, ...
Zito kiasilia ni bahili isitoshe hizo pesa wanagawana na viongozi wenzao wengi na zitazosalia zitaimarisha chama, ukumbuke hiyo ni Rushwa lazima matumizi yake yanafanyika kwa siri kukwepa ushahidi wa mali kuonekana , Zito shamba lake ni Siasa amevuna pesa nyingi kupitia Siasa tokea utawala wa mkapa kikwete hata awe na pesa nyingi huwezi kumjua kwani mda wote hujidai Masikini saa 24
 
Zito kiasilia ni bahili isitoshe hizo pesa wanagawana na viongozi wenzao wengi na zitazosalia zitaimarisha chama, ukumbuke hiyo ni Rushwa lazima matumizi yake yanafanyika kwa siri kukwepa ushahidi wa mali kuonekana , Zito shamba lake ni Siasa amevuna pesa nyingi kupitia Siasa tokea utawala wa mkapa kikwete hata awe na pesa nyingi huwezi kumjua kwani mda wote hujidai Masikini saa 24

Kwa hiyo unaamini ruzuku aliyolipwa CHADEMA kwa karibia miaka 5 apewe Zitto Kabwe kama sadaka mara moja tu? Na kwa lipi haswa hadi alipwe hela zote hizo ?
 
Hata wewe haulewi maana ya dola milion 5 USD unataja tu namba, laiti ungeelewa usingeamini kirahisi hivyo kwamba Serikali inaweza kumpa Zito Kabwe hela zote hizo, for what ?
Serikali ina pesa nyingi mno vipesa kama dola milion 5 kwao ni vipesa kidogo mno
 
Serikali ina pesa nyingi mno vipesa kama dola milion 5 kwao ni vipesa kidogo mno

Ndo maana nasema unarusha tu namba lkn hauelewi maana yake nini, labda hauelewi unaweza kufanya nini dola US milioni 5, vinginevyo usingeamini kirahisi hivyo, ...
 
Kwa hiyo unaamini ruzuku aliyolipwa chadema kwa karibia miaka 5 apewe Zito Kabwe kama sadaka mara moja tu ? Na kwa lipi haswa hadi alipwe hela zote hizo ?
CHADEMA ina watumishi wengi gharama za kuendesha chama ni kubwa isitoshe CHADEMA hutumia gharama kubwa kujihami dhidi ya hujuma za CCM ikiwemo utitiri wa kesi za kubambikiwa na mambo mengineyo ya hovyo tokea CCM, CHADEMA inatumia pesa nyingi kuzuia dhahama za CCM na mengineyo mengi ya ajabu tokea CCM ikiwemo chaguzi za marudio
 
Sasa Ndugu yangu Wewe wa kumfundisha Siasa Maalim Seif Sharif Hamad hasa hasa siasa za Upinzani Tanzania?

Seif katumia options zote mnazomshauri na bado hazijazaa matunda

1. 1980s Seif katumia uongo na uzushi na fitna kutaka kumchomoa Sheilkh Jumbe kwa kumchonganisha na Nyerere , akafanikiwa kumkosesha Urais Jumbe lakin hakufanikiwa kupata Urais wa Znz

2.1985-1990 Seif Katumia Siasa za kumchonganisha Idrisa Abdul wakeel na Wananchi Unguja 1985-1990 akafanikisha kumstaafisha Urais Hayati Mzee Wakeel lakin hakuupata Urais
3. 1995 Seif akafanikiwa kuichonganisha Znz na Jumuiya ya Kimataifa hadi ikawekewa vikwazo lakin haikumfanya kupata Urais
4.2000 Seif akafanikiwa kuitisha Maandamano ya vurugu watu wakauawa lakin hakufanikisha azma yake ya Urais

5. 2010 akaridhia maridhiano ili apate fursa ya kuwa ndani ya Serikal akidhan ni shortcut ya kumfanya kupata Urais lakin hakufanikiwa
6.2016 Akasusia Uchaguzo, uchaguzi ukafanyika lakin hakuna alicho gain


So Options zote za Kisiasa kuanzia Fitna za kuchonganisha Watu ndan ya Serikal, kufungwa, kuhama vyama, kuitisha maandamano hadi watu kufa,kususa, kuchongea jumuia ya kimataifa hadi kuwekwa vikwazo, kote huko kamaliza

So only option iliyopo ni kushirikiana na Walinzi wa Mapinduzi matukufu ya 1964

Naifahamu vizuri historia ya Maalim Seif na Znz, nashukuru kwa mtiririko wako mzuri kuhusu safari ya kisiasa ya Maalim Seif. Ila uliponiquote sina popote nilipomtaja Maalim Seif, maana najua Maalim Seif ni tofauti na ACT ambayo iko chini ya Zito. Nimemtaja Zito maana ndio mwenye chama cha ACT. Maalim Seif ni taasisi yenye kama yeye, popote au chama chochote atakachoenda Wapemba wenzake watamfuata. Kwa maneno marahisi, Maalim Seif hahitaji chama chochote kufanya siasa za huko Znz, maana tayari ana wafuasi wa rohoni, ila ni wachache sana unapoitaja Tanzania.Rejea anguko la CUF baada ya Seif kuondoka kudhibitisha Seif ni taasisi ndani ya Taasisi.

Namzungumzia Zito maana ndio mwenye chama cha ACT, ili ACT ikue hasa huku bara ilipaswa kutembea pembeni ya bega la cdm, hapo ingepata imani kubwa sana ya wapinzani. Ukweli usioacha shaka ni kuwa cdm ndio yenye wafuasi wa upinzani wengi hasa vijana, na ccm tayari ni chama kilichopitwa na wakati, ila ina mwenyekiti mwenye kiburi cha madaraka kwa kofia ya urais. Matumizi haya mabaya ya madaraka, kwa makusudi au kwa bahati mbaya inasemwa kuwa ni uimara wa ccm jambo ambalo si kweli. Mwenyekiti huyu akitoka madarakani, ni nadra mwenyekiti ajaye wa ccm kuwa na misimamo yake, kwani tayari nchi ipo kwenye mahusiano mabaya kimataifa, na sehemu yenye tatizo ni demokrasia na Utawala bora kwa sababu ya rais huyu. Mbinyo atakaoupata mwenyekiti ajaye wa ccm ni kuheshimu utawala bora na demokrasia, hivyo uwanja wa siasa utarudi kama inavyopaswa ikiwemo uhuru wa vyombo vya habari , kwa vyovyote vile ccm tayari itakuwa imelamaa kwenye ushindani kwani inategemea zaidi kubebwa, hivyo cdm itaonekana tena maana ina wafuasi watiifu, wakati huo ACT itakuwa imepoteza imani kwa watu wenye imani ya upinzani, na eneo dogo la Znz ambapo Maalim Seif yupo, atakuwa amezeeka hivyo kushindwa kwenda na changamoto za wakati huo. Je ni nani atavaa viatu vya Seif na awe na ushawishi kama Seif? Je Zito huku Bara atatoboa kutokana na maamuzi ya chama chake kwa sasa?
 
Ndo maana nasema unarusha tu namba lkn hauelewi maana yake nini, labda hauelewi unaweza kufanya nini dola US milioni 5, vinginevyo usingeamini kirahisi hivyo, ...
Kwako binafsi unaona ni pesa nyingi lakini kwa Serikali ni pesa kidogo sana kwani utulivu wa Serikali ya Zanzibar utapelekea kupata misaada mingi tokea nje na hiyo pesa unarudi ndani ya mda mchache sana
 
Mbona wakati anahamasisha watanzania wajiunge na chama cha Act wazalendo hakusema waanzishe chama chao ?au ndio upimbi unamsumbua baada ya kuusaliti umma wa watanzania yeye na Maalim Seif ?
Pesa waliyochukua imemtia kiburi
 
Kilichowazuia kutoka barabarani ni nini wakati mlitakiwa kuidai hiyo haki na hamkutoka?
Zitto kachanganya na za kwake baada ya kuona mmemterekeza siku ya kuandamana.
Sasa wenye hasira na hiyo SUK anzisheni chama nanyi mkapinge kujiunga nayo.
Kuandama kwenye serikali dhalimu siyo rahisi maana unaweza kosa viungo vyako vyote
 
Nimeshangazwa na majibu ya mkuu wa chama cha ACT Wazalendo ndugu Zitto Kabwe aliyoyatoa kwenye mtandao wa twitter.

Zitto alikuwa akimjibu mwananchi mmoja aliyekuwa akionyesha frustrations zake juu ya uamuzi wa chama cha ACT kujiunga na Serikali ya CCM huko Zanzibar katika kile kinachoitwa serikali ya umoja wa kitaifa. Mwananchi huyo anaonyesha kuwa kuingia kwa ACT katika hiyo serikali hakuwezi kusaidia wananchi kupata uhuru mpana waliokuwa wakitamani kuwa nao.

Katika hali isiyo ya kawaida, isiyo ya uungwana na isiyo ya kiuongozi mkuu wa chama cha ACT ndugu Zitto badala ya kutumia fursa hiyo kumuelewesha au atleast akae kimya wananchi watumie haki yao ya kutoa maoni, yeye anamjibu kwa ufedhuli na jeuri kuwa "Kama unaona tumekosea basi anzisha chama chako".

Kwa kweli sikutegemea kiongozi haswa wa upinzani kutoa majibu ya nyodo kama haya kwa wananchi wanapouliza maswali ya msingi juu ya mienendo ya kisiasa nchini.

Labda Zitto afahamu tu kuwa sababu mojawapo ya leo ACT kuwa hapa ni haohao wananchi ambao leo anawajibu kwa nyodo kuwa "anzisheni chama chenu"

Lakini pia Zitto akumbuke kuwa kuna watu wamekifia hicho chama, Wakati akijibu kwa majibu ya "Anzisheni chama chenu" Je amelifikiria hili kuwa kuna watu wame-pay ultimate price kwa hicho chama au kwa course yake waliyoinadi kwao na kwa hiyo ndugu, jamaa, marafiki na wananchi wana haki ya kuhoji ukinyongakinyonga wa misimamo iliyowafanya hapo awali wawe tayari kukipigania hicho chama?

Lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida, Viongozi wa ACT sasa hivi wameacha kujibu maswali magumu ya wananchi juu ya hatua yao ya kuingia kwenye SUK wakati waliitangazia dunia na nchi kiujumla kuwa uchaguzi uliopita ulikuwa haramu, Zitto mwenyewe akaweka saini tamko la pamoja la Upinzani kuwa hawautambui uchaguzi ule pamoja na natunda yake, Sasa leo wananchi wakihoji wanaambiwa jamani eeh kama hamtaki tulichokifanya basi nendeni CCM, au NCCR yaani ni majibu ya kifedhuli uliopitiliza!. Sasa wameacha kutoa majibu kwa wananchi, wameanza kublackmail wanachama wa ACT na kutoa kauli za nyodo kwa wananchi, kuwa "ACT ina wenyewe na nyie kaanzisheni chama chenu"

Sasa leo tunaona kwa macho yetu, watu tuliodhani ni wakomavu wa kisiasa, tuliodhani kuwa mashambulizi yao kwa CCM basi wao labda wana ngozi ngumu na kwamba labda wao wakipewa nchi basi watakuwa humble, watakuwa na humility, watajibu hoja kwa hoja kumbe hawa jamaa ni arrogant(wenye viburi), intolerant(wasio wavumilivu) na wanajiona wao ni wamiliki wa taasisi kwa kuwa walizianzisha na si wahudumu tu wa taasisi ambazo wao ni wanachama.

Hawa wapinzani hawana blank cheque ya kutuletea jeuri sisi wananchi, Kwa miaka mingi tumekuwa tukiishabumbulia CCM, lakini na wenyewe hawana impunity, tutawaekeza ukweli maana hivyo vyama kwa namba moja au nyingine vinanufaika kwa jasho la wananchi iwe kwa ruzuku au wanasiasa wao kulipwa kwa kodi za wananchi n.k

Zitto acha jeuri kwa wananchi, Jibu hoja na frustrations zao kwa hekima, utulivu, nidhamu na utu. Bila wananchi usingekuwa hapa kuwa na humility.

View attachment 1648516

Na mahali pengine anamjibu mwananchi hivi:

View attachment 1648775
Safi sana maswali yamekuwa mengi, unapokuwa na kiongozi kama Zitto Kabwe na Maalim Seif pamoja hutakiwi kuwa na mashaka nao kuhusu maamuzi yoyote, maalim siku zote amekuwa muaminifu na husimama upande wa wananchi ni suala la kuwapa muda tu kwa kile walichokiamua kwenye Kamati tukaona impact yake
 
We kamanda unajilopokeaga tu.. Hivi unajua dola milion 5 ni kitu gani katika uhalisia?
Ni bilion 10 tu, kwa mfano yeye akiweka kibindoni bilion 2, halafu nane zilizobaki akawagawia genge lake ili wamuunge mkono watulie wewe huoni kuwa inawezekana kabisa?

Jiwe anafahamika kuwa ni mwepesi wa kupenyeza rupia ili kutuliza upinzani mkali mfano mmojawapo ni jinsi alivyomtuliza Mange kwa mpunga mrefu
 
Back
Top Bottom