Zitto Kabwe awa mbogo, awashukia vikali wanaodai Makamu wa Rais, Dkt. Mpango ni Mrundi

Zitto Kabwe awa mbogo, awashukia vikali wanaodai Makamu wa Rais, Dkt. Mpango ni Mrundi

Ila hizi propaganda kwamba Dr. Mpango ni Mrundi kwa kuwa tu ameonekana akicheza wimbo wa kiha ni utoto na kukosa hoja.

Kigogo sometimes anakuwa na mambo ya kipuuzi sana. These days yupo off target kwa kila jambo na frustrations zake zinamfunua na kuonyesha ni mtu wa aina gani

Niliwaambia kuwa huyu KIGOGO yumo humu humu nchini sio kama MUSIBA na genge lake walitaka kutuaminisha kuwa yuko UINGEREZA!! Hili ni kundi la hawa watu waliokuwa wanauwania umakamu wa RAIS na kuukosa hivyo sasa wanaleta propaganda zao za ukabila!!
 
Zito nae anatafuta kiki tu. Toka lini Burundi wakavaa sare za CCM? Ukiangalia ile ngoma wamama wanaocheza na Dr.Mpanga wanaonekana dhahiri ni CCM na nguo zao za kijani. Sema Zito ni mzuri sana kwenye kutumia fursa.
Ngoma ilichezewa Burundi? Warundi hawawezi kuvaa sare?
 
Kigogo ni mku.ndu tu yule, serikali na vyombo vyake vyote wameshindwa hata kumbaini kweli? Wambaini anaishi wapi watoe mpunga wa maana hata kama anaishi nje ya nchi sie wengine hata kujitoa mhanga siyo tatizo.Unamfumua mtu hata nikifia jela nchi nyingine poa tu
 
Watu wa mikoa ya pembezoni huwa wananyanyapaliwa sana kwa kubambikiwa uraia wa nchi jirani.
Zitto yuko sahihi kukasirika
Hilo ni tatizo la ccm, walianza enzi za Mkapa kutumia fimbo ya uraia kuwapiga wanaowakosoa. Basi. Yaani mtu anayeikosoa serkali ya ccm atazushiwa siyo raia. Alianza Jenerali Ulimwengu ambaye aliikosoa sana serikali ya ccm enzi ya Mkapa, kwa ubinafsishaji wa kifisadi, na mikataba ya kifisadi ya madini.

Ulimwengu akatangazwa siyo raia. Kwa wale wasiofahamu, Jenerali Ulimwengu ni msomi mahiri. Alisoma sheria chuo kikuu cha Dar enzi hizo siasa za ukombozi zimepamba moto. Yeye na wenzake, walidiriki kushiriki vita mstari wa mbele kule Msumbiji, kuiunga mkono FRELIMO.

Baada ya masomo nadhani alifanya kazi Daily News, chini ya Mkapa, na kuna wakati alikuwa Algeria, kama coordinator wa umoja wa vijana Afrika. Baada ya hapo alirudi Tanzania na akawa DC nadhani hapa Dar. Nakumbuka alikuwa mmoja wabunge (G. 55?) Waliounga mkono serikali tatu enzi hizo. Baadaye aliachana na active politics akarudia fani ya magazeti, akiwa na gazeti la Rai, baadae Dimba na Mtanzania. Baada ya Nyerere kuachana na urais, akiwa kwenye Tume ya mataifavya kusino, South Commission, alimtumia sana Ulimwengu kama mkalimani katika lugha ya Kifaransa, wakati akiwa mpatanishi katika mataifa mbalimbali

Uchaguzi Mkuu wa 1995 alitumia gazeti lake la Rai kumpigia kampeni kali Mkapa, akiwa na wenzake kina Johnson Mbwambo. Nakumbuka siku anatangaza kuingia kinyan'ganyiro cha Urais, Mkapa alizungukwa na watu wawili. Upande mmoja Mark Bomani (kama sikosei) na upande wa pili Jenerali Ulimwengu.

Baada ya kushinda, Ulimwengu alipewa fursa kadhaa kuiwakilisha nchi katika forum kadhaa za kimataifa. Lakini mara Mkapa alipoanza sera za ubinafsishaji holela, wakasigana na Ulimwengu, ambaye alitumia tena magazeti yaleyale yaliyomsifia mwanzo, Mr. Ben, Mr. Clean, sasa akaanza kumkosoa.
Wakati huo Ulimwengu alikuwa na cheo fulani Baraza la Michezo la Taifa, BMT, na nyadhifa kadhaa zingine. Alipotangazwa tu siyo raia, vyote vikaporomoka.

Hiyo ilimchanganya sana Jenerali.
Tokea hapo rungu la uraia limetumiwa sana na serikali za ccm kupambana na wanaowakosoa kwa hoja. Siku zote ccm hawajui kujibu hoja. Kama siyo uraia, watatumia Polisi kukutuhumu uchochezi, uhujumu uchumi, utakatishaji fedha, au hata kukupima mkojo, wakubambikizie madawa ya kulevya. Ndio yalitaka kumkuta Tundu Lissu, bahati njema alikataa kutoa mkojo.

Shida ya Lissu ni mtu wa Singida, katikativya nchi. Unambambikizaje kuwa siyo raia?

Kwa hiyo Magufuli naye hakusita kutumia karata hiyo. Na kwakuwa ni mbabe, yeye sasa akaenda mbali hadi kuitumia kwa maaskofu.

Kwa hiyo nikisikia wengine wakimtaja Waziri Mpango, nachekelea tu, ni kejeli kwa ccm na silaha yake feki.

Nashangaa kuna watu wanamtaja Magufuli kama Mwanamajumui (Pan Africanist) eti shujaa wa Afrika . Hiyo si kweli. Mwanamajumui wa kweli anaamini katika Afrika moja, sio mipaka iliyowekwa na wakoloni. Nyerere ndio, huyo ni Mwanamajumui. Kaipigania Afrika . Hakuwahi hata mara moja kutenda dhambivya ubaguzi, kusema fulani siyo raia. Huo ni ujinga.
 
Mbona Zitto hakupanic hivi wakati Magu anaitwa mhutu?

Hii tabia ya kuanza kupekenyua uraia wa viongozi wetu ikome sasa!


Mtu ametoa hadi historia ya tangu anazaliwa lakini zwazwa moja linakuja linasema huyo ni wakutoka nchi flani
 
Ila hizi propaganda kwamba Dr. Mpango ni Mrundi kwa kuwa tu ameonekana akicheza wimbo wa kiha ni utoto na kukosa hoja.

Kigogo sometimes anakuwa na mambo ya kipuuzi sana. These days yupo off target kwa kila jambo na frustrations zake zinamfunua na kuonyesha ni mtu wa aina gani
Amekosa taarifa + hoja za msingi

Hata yale ya kuvuja hayaonekani tena.

Anataka kumaintain followers wake.
 
Baba wa taifa aliwai kukili kuwa tumepambana na ukabila sana lakini ukabila bado upo, ukiwaminya sehemu utasikia maweeee!
 
Huyu si Mwanasiasa wa kwanza kutuhumiwa kwamba si raia wa Tanzania , wako wengine kadhaa walishatuhumiwa akiwemo aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala Generali Ulimwengu , wamo akina Eyakuze wa Twaweza pamoja na Maaskofu kadhaa wa Makanisa .

Walichokifanya ni kutoa nyaraka zao kuthibitisha uraia wao , wako ambao pia walithibitisha hata uraia wa babu zao baada ya kutakiwa kufanya hivyo , kwahiyo tuhuma za uraia wala si jambo geni , Nyalandu alidaiwa kuwa na uraia wa nchi mbili mbona hatukusikia akitetewa ?

Makamu wa Rais kama walivyo Watanzania wengine hana kinga dhidi ya shutuma zozote juu yake , anatakiwa ajitokeze hadharani kukanusha tuhuma hizo na kuthibitisha uraia wake , huo ndio Uzalendo , Kabudi na Mwandosya wamewahi kushutumiwa kuhusu vyeti feki lakini walijitokeza hadharani na kutoa ufafanuzi na wazushi wakashindwa , hiki ndicho anachopaswa kukifanya Dr Mpango ili kuweka mambo sawa kabla wadau hawajazusha mengine .

Hakuna haja ya wanasiasa kujivika utetezi wakati Mpango mwenyewe yupo , ajitokeze tu .
 
Kwani ni nani anayemtuhumu? kuna jibu moja Nyerere aliwahi kulitoa pale Hoteli ya Kilimanjaro baada ya mwandishi mmoja kuda "amesikia"... Wanaodai siyo raia ndio wanajukumu la kutoa uthibitisho wao. Wao watuambie kwanini wanasema siyo rais; kucheza ngoma haiwezekani kuwa ni ushahidi au uthibitisho...
 
Back
Top Bottom