Zitto Kabwe: Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa ambayo hamjawahi kuyaona, tusipoteze hii fursa jamani

Zitto Kabwe: Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa ambayo hamjawahi kuyaona, tusipoteze hii fursa jamani

Kumbe bado hujafahamu shida ipo wapi,
Jisome hii
2
Lessons from Sri Lanka on China's 'debt-trap diplomacy'
China's 'tied aid' for infrastructure usually benefits Chinese companies, while its loans are in many cases backed by natural resources.




www.nytimes.com
How China Got Sri Lanka to Cough Up a Port (Published 2018)
25 Jun 2018 — Yes, though Sri Lanka's debt was ballooning rapidly under Mr. Rajapaksa. ... The case is one of the most vivid examples of China's ambitious use of loans and ...
Nadhani wewe ndio unachanganya mambo hapa, mimi naelewa vizuri. Hawa waliingia katika matatizo kwa ajili ya kukopa pesa nyingi China haikuwa uwekezaji wa kibiashara. Sisi issue ya Port ni uwekezaji wa makubaliano ya kibiashara. nikupe mfano miwili sisi na hao Srilanka. chukuwa wewe una kiwanja Kariakoo anakuja mfanya biashara anakwambia nipe kiwanja nijenge gorofa ikiisha nakupa maduka 4 mimi nachukuwa 10 baada ya miaka 20 nikiwa nimerudisha pesa zangu nitakupa wewe 10 na mimi 4 baadaya muda nyumba yote yako, huu uwekezaji wa kibishara na makubaliano ndio yetu Bagamoyo. Hao wengine ni kuwa walikuwa na kiwanja wakaenda Bank kukopa pesa nyingi biashara imekataa kurudisha hawawezi Bank inachukuwa nyumba. msichange mikopo na investment kama kukopa tumekopa kipande cha mwisho cha SGR toka Mwanza huo ni mkopo na lazima urudishwe, tulikopa Gas line toka Mtwara ndio mikopo. Ukisoma zote ulizonitumia ni kuwa walichukuwa mikopo
 
🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾 Ahsante sana hawa wahuni nchi imewashinda na wanajua hivyo sasa wamebaki kulazimisha kung’ang’ania madarakani kwa kutumia njia haramu. Zitto ni mnafiki na mroho wa madaraka watu wenye tabia hizi ni watu hatari sana kwa mustakabali wa Taifa. Sasa kaamua kujiegemeza kwa Mama akitegemea kupata ulaji.
Hii nchi ina viongozi wa ajabu sana
Zitto haeleweki ni sawa na debe tupu... anapuyanga hatari
Bandari hahahahh ya nini wakati iliyopo inawashinda, sheria za uwekezaji zimekimbiza wawekezaji, kuna miradi lukuki haijakamilika.
Hawa wanatumia ujinga sijui upole au udhaifu wa WaTz kujinufaisha
Mchina si muwekezaji ni mnyonyaji tuelewe hivyo
Tango Mama kaingia madarakani Zitto amekuwa msemaji Mkuu
Huyu dogo ana udhaifu fulani hivi wengi hawajauona bado na ni hatari kwa Taifa
ACT mlengo wake ni wa.........
Tutakumbushana mbeleni
Keleleeee nyiiiiingi lakini si kwa nia inayofanana na wengi wa wananchi
 
Tatizo lenu hamtaki kusikiliza!

Mngekuwa mnasikiliza hoja na kizipima badala ya kupinga tu kwa kuwa mtoa hoja humpendi.

Mradi wa Bandari ya Bagamoyo,ulikuwa ujengwe kwa makubaliano ya uwekezaji wa pande tatu,Tanzania,Oman na China. Wawekezaji wangejenga miundo mbinu ya bandari na industrial parks kwa ajili ya viwanda zaidi ya 800 na kuchukua port charges kwa kipindi cha miaka 50. Serikali haikuyakiwa kutoa hata sumuni! Katika kipindi hicho serikali itachukua kodi zingine mbalimbali kama ushauri wa forodha kama kawaida. Baada ya miaka hiyo, bandari inakuwa mali ya serikali 100%

Utaratibu huu ndio unaotumika hata sasa kwenye bandari ya Dar. Wapo TICTS wanaendesha bandari hiyo.

Mradi wa Bandari ya Bagamoyo unamanufaa makubwa katika uchumi wa Tanzania. Pamoja na kuifanya Tanzania kuwa lango juu la bidhaa kwa zaidi ya nchi 8 za Afrika,unaifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda vya kisasa ambavyo vitahudumia soko la ndani na nchi nyingine za Afrika.

Mradi huu utazalisha ajira nyingi mno katika sekta mbalimbali kama mahoteli, usafirishaji nk.

Hayo maelezo yako umeyatoa wapi? Mbona ni tofauti na Hayati, Pia aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa TPA Kakoko.
 
Tatizo bandari mnayotaka kuijenga haipo Chatial... hapa ndipo tatizo lilipo msitafute mchawi.
 
Eti mameli makubwa ndiyo fahari yake kuona mameli makubwa bila faida yoyote
 
KC wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe amesema kitu ambacho wabunge wengi hawakijui ni kwamba Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa makubwa kutoka huko duniani ambazo hatujawahi kuziona hapa Tanzania

Kisha hizi meli tunazoziona zikileta mizigo Dar port ndio zitakuwa zinabeba miizigo kutoka Bagamoyo na kusambaza sehemu mbalimbali duniani amesisitiza Zitto

Tusiiache fursa hii jamani na siyo kweli kwamba kila mradi ulioanzishwa awamu ya Kikwete ulikuwa mbaya kwani hata reli ya SGR mradi uliasisiwa vizuri na serikali ya JK lakini serikali ya awamu ya tano imekuja kuutekeleza kwa namna tofauti, amemalizia Zitto.

Chanzo: Clouds 360
Nadhani kila mradi unatakiwa uwe kwenye mpango wa Maendeleo.Hatuwezi kuwa tunafuta miradi bila kufuata utaratibu wala kuirudisha miradi kwenye mpango kwa kutumia njia za Mkato.
 
ni kweli tatizo watatuendesha wao kwa mashati yao ukoloni mambo leo. bora tutafute vyakwetu tu tuwe huru.
 
Nadhani wewe ndio unachanganya mambo hapa, mimi naelewa vizuri. Hawa waliingia katika matatizo kwa ajili ya kukopa pesa nyingi China haikuwa uwekezaji wa kibiashara. Sisi issue ya Port ni uwekezaji wa makubaliano ya kibiashara. nikupe mfano miwili sisi na hao Srilanka. chukuwa wewe una kiwanja Kariakoo anakuja mfanya biashara anakwambia nipe kiwanja nijenge gorofa ikiisha nakupa maduka 4 mimi nachukuwa 10 baada ya miaka 20 nikiwa nimerudisha pesa zangu nitakupa wewe 10 na mimi 4 baadaya muda nyumba yote yako, huu uwekezaji wa kibishara na makubaliano ndio yetu Bagamoyo. Hao wengine ni kuwa walikuwa na kiwanja wakaenda Bank kukopa pesa nyingi biashara imekataa kurudisha hawawezi Bank inachukuwa nyumba. msichange mikopo na investment kama kukopa tumekopa kipande cha mwisho cha SGR toka Mwanza huo ni mkopo na lazima urudishwe, tulikopa Gas line toka Mtwara ndio mikopo. Ukisoma zote ulizonitumia ni kuwa walichukuwa mikopo
Sasa hapo hapo kwenye mfano wako nani ana control cost za investment , pili nani ana control rent, na kwa ujumla revenue wakati wewe huhusishwi ktk hiyo biashara, halafu risk nyingine ikiwa biashara isiende vizuri hivyo wasirudishe hela yao ktk kipindi walicho sema inakuwaje.
Mwisho kuna kitu kinaitwa substance over form.
Kimsingi mtu anapoweka sharti la kurudisha pesa yake na faida ni mkopo. Usidanganyike na haya maneno mengine ya uwekezaji wa kibiashara.

Another example is the situation where a company short of cash sells its machinery to the bank and then leases the same property from the bank. ... Under the substance-over-form principle, the sale and subsequent leaseback are considered one transaction.
Hapa zimechukuliwa kwamba umekopa na sio umeuza hiyo machinery , na hela ya ku lease zimechukuliwa kama ni ya kulipa mkopo interest na principal

Ndio maana kwenye mambo kama haya tunatakiwa kuwatumia wataalamu na sio wanasiasa,
Hapa mwana siasa atakwambia huyu anatujengea sio anatukopesha na masharti yake ni nafuu kulinganisha na nini hakwambi,
Ndio tukaishia kujenga jengo la umoja wa vijana, uwt n.k n.k
 
KC wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe amesema kitu ambacho wabunge wengi hawakijui ni kwamba Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa makubwa kutoka huko duniani ambazo hatujawahi kuziona hapa Tanzania
Halafu tuwape kwa miaka 99 sio ?

Ushenzi na umangimeza uliokubuhu. Kwa hili Zitto nakukatalia kwa herufi kubwa HAPANA
 
Halafu tuwape kwa miaka 99 sio ?

Uhsenzi na umangimeza uliokubuhu. Kwa hili Zitto nakukatalia kwa herufi kubwa HAPANA
Sasa wanjanja watu kuwekea miaka 33 wakati kuna kifungu kingine wanaficha kwamba mkataba utaendelea ikiwa hawajarudisha fedha zao huku fedha zingine wanachukua kwa ununuzi vipuri na mngt fees
 
Ngoja tukashangae mameli Bagamoyo.
Bwana eh tuandae makameraaa makubwa kabisa
Ila ipo siku watamkumbuka jpm kwenye hili
Maana naona nguvu kubwa ya kutuaminisha inatumika ili wafanikishe azma yao

Ova
 
KC wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe amesema kitu ambacho wabunge wengi hawakijui ni kwamba Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa makubwa kutoka huko duniani ambazo hatujawahi kuziona hapa Tanzania

Kisha hizi meli tunazoziona zikileta mizigo Dar port ndio zitakuwa zinabeba miizigo kutoka Bagamoyo na kusambaza sehemu mbalimbali duniani amesisitiza Zitto

Tusiiache fursa hii jamani na siyo kweli kwamba kila mradi ulioanzishwa awamu ya Kikwete ulikuwa mbaya kwani hata reli ya SGR mradi uliasisiwa vizuri na serikali ya JK lakini serikali ya awamu ya tano imekuja kuutekeleza kwa namna tofauti, amemalizia Zitto.

Chanzo: Clouds 360
Hatautatki hayo mameli yasiyo faida na wananmchi. Waambie wachina waende Kenya hatutaki Bandari Bagamoyo na mlogwe muipitishe patachimbika!
 
Sasa wanjanja watu kuwekea miaka 33 wakati kuna kifungu kingine wanaficha kwamba mkataba utaendelea ikiwa hawajarudisha fedha zao huku fedha zingine wanachukua kwa ununuzi vipuri na mngt fees
Khaa . . management fees ? Pumbavu kabisa
 
Bwana eh tuandae makameraaa makubwa kabisa
Ila ipo siku watamkumbuka jpm kwenye hili
Maana naona nguvu kubwa ya kutuaminisha inatumika ili wafanikishe azma yao

Ova
Hahahaaaa...... !

Mchina akitimba Bagamoyo wazaramo wote watasukumiziwa Msata na Pangani.
 
Back
Top Bottom