Zitto Kabwe: Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa ambayo hamjawahi kuyaona, tusipoteze hii fursa jamani

Zitto Kabwe: Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa ambayo hamjawahi kuyaona, tusipoteze hii fursa jamani

Hivi Tanzania ni Bagamoyo tu? kuuza nchi maana yake nini? kwani ulisikia tunakopa sisi, huu ni uwekezaji sio mkopo sisi kama nchi hatuna uwezo wa kujenga port kubwa ya kisasa najuwa watu wanasema tunayo port Dar ya nini hii, Port ya Dar ina limitation na ya kizamani ni sawa na Airports tulikuwa na Term-1, tukaja 2 na sasa 3 kwa sababu Tech inabadilika. Hizi propaganda tunauza nchi hazina mashiko dunia ni biashara kutoa ki ardhi kijisehemu tu Bagamoyo ndio imekuwa tunauza nchi? tuwe serious kidogo na kujiongeza
Wekeni hadharani vipegele vya mkataba. Hatubishanii umuhimu wa bandari. Mkataba. Mwendake alituambia mkataba ule ni mbovu. Uleteni bungeni, wabunge wauone na waujadili. Hatutaki kina Chifu Mangungo wafufuke! Karl Peters wa leo (Wachina) ni wajanja mno.
 
KC wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe amesema kitu ambacho wabunge wengi hawakijui ni kwamba Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa makubwa kutoka huko duniani ambazo hatujawahi kuziona hapa Tanzania

Kisha hizi meli tunazoziona zikileta mizigo Dar port ndio zitakuwa zinabeba miizigo kutoka Bagamoyo na kusambaza sehemu mbalimbali duniani amesisitiza Zitto

Tusiiache fursa hii jamani na siyo kweli kwamba kila mradi ulioanzishwa awamu ya Kikwete ulikuwa mbaya kwani hata reli ya SGR mradi uliasisiwa vizuri na serikali ya JK lakini serikali ya awamu ya tano imekuja kuutekeleza kwa namna tofauti, amemalizia Zitto.

Chanzo: Clouds 360
Kwa nini iwe Bagamoyo na isiwe Kilwa au Mafia? Tuache uzuzu hii ni project ya JK ila anatumia wapambe wake na mmojawapo ni Zitto. Huyu ni suhuba wa JK mkubwa sana.
 
Wekeni hadharani vipegele vya mkataba. Hatubishanii umuhimu wa bandari. Mkataba. Mwendake alituambia mkataba ule ni mbovu. Uleteni bungeni, wabunge wauone na waujadili. Hatutaki kina Chifu Mangungo wafufuke! Karl Peters wa leo (Wachina) ni wajanja mno.
Sasa mimi nitautoa wapi huo mkataba? hiyo ni kazi ya bunge. sidhani kama kuna mkataba labda majadiliano maana mkataba unakuwa umeshawa kuwa sign na unakuwa kisheria mimi sijui kama kuna mkataba wa lisign. Ni kazi ya watunga sheria kutaka kuona hayo majadiliano na kuweka wazi kwa wananchi wote. mashaka yangu tu aina ya wabunge waliopo wana upeo wa kujadilia mambo labda wachache. lazima zipimwe hasara na faida zake mwisho wa siku uzito una beba maamuzi. Mimi sina mkataba na wala sijui kilichopo hata aliyeongea hakuweka ushahidi kama karatasi wenye masharti hayo yalikuwa maneno tu kama sisi hapa tunavyoongea.
 
Sasa mimi nitautoa wapi huo mkataba? hiyo ni kazi ya bunge. sidhani kama kuna mkataba labda majadiliano maana mkataba unakuwa umeshawa kuwa sign na unakuwa kisheria mimi sijui kama kuna mkataba wa lisign. Ni kazi ya watunga sheria kutaka kuona hayo majadiliano na kuweka wazi kwa wananchi wote. mashaka yangu tu aina ya wabunge waliopo wana upeo wa kujadilia mambo labda wachache. lazima zipimwe hasara na faida zake mwisho wa siku uzito una beba maamuzi. Mimi sina mkataba na wala sijui kilichopo hata aliyeongea hakuweka ushahidi kama karatasi wenye masharti hayo yalikuwa maneno tu kama sisi hapa tunavyoongea.
Nimekupata. Tunajadili kwa muktadha wa Muheshimiwa sana Ndugai anayetetea sana kila anachosema mwendazake alishauriwa vibaya. Alete proof hiyo bungeni wabunge waone nani kamdanganya nani.
 
kwanini wasitoe mkataba tukauona? wanabaki tu tujenge wengine wanasema tusijenge. bora hoja za JPM zilijikita kwenye mkataba
 
Nimekupata. Tunajadili kwa muktadha wa Muheshimiwa sana Ndugai anayetetea sana kila anachosema mwendazake alishauriwa vibaya. Alete proof hiyo bungeni wabunge waone nani kamdanganya nani.
Mimi nilichosikia kwa Ndungai ni kuwa port Bagamoyo inahitajika sasa kama wa China hamuwezi kuafikiana nao tafuteni wawekezaji wengine yoyote aje ajenge yeye kasema mradi unahitajika. Hayati yeye kasema wanataka kutuibia basi yakaishia hapohapo, ndio maana yanaitwa majadiliano na PSA inataka watu wenye kujuwa kujadiliana wale ni wafanya biashara hawaji kutoa misaada lazima watuvuta upande wao. Mimi na uhakika port itajengwa sasa itajengwa na nani hilo sijui. Bunge wako busy kujadili Legacy ya marehemu badala ya maendeleo.
 
KC wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe amesema kitu ambacho wabunge wengi hawakijui ni kwamba Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa makubwa kutoka huko duniani ambazo hatujawahi kuziona hapa Tanzania

Kisha hizi meli tunazoziona zikileta mizigo Dar port ndio zitakuwa zinabeba miizigo kutoka Bagamoyo na kusambaza sehemu mbalimbali duniani amesisitiza Zitto

Tusiiache fursa hii jamani na siyo kweli kwamba kila mradi ulioanzishwa awamu ya Kikwete ulikuwa mbaya kwani hata reli ya SGR mradi uliasisiwa vizuri na serikali ya JK lakini serikali ya awamu ya tano imekuja kuutekeleza kwa namna tofauti, amemalizia Zitto.

Chanzo: Clouds 360
Kwa asimia ngapi Bandari zetu za Tanga na Mtwara zinatumika? Kuna tofauti gani za gharama kati ya kuzipanua na kuziimarisha Bandari za Tanga na Mtwara na ujenzi wa Bandari mpya ya Bagamoyo. Ni faida zipi zitakazoletwa na Bandari ya Bagamoyo ambazo hatuzipati katika Bandari za Tanga na Mtwara? Majibu ya Maswali haya ndio yatakayo halalisha au kutohalalisha ujenzi wa Bandari Mpya ya Bagamoyo. Lakini pia uwezekano wa upanuzi wa Bandari ya Dar Es Salaam.
 
Unanikumbusha Tulivyoandamana udsm enzi izo tukipinga mkataba wa miaka 50 wa mlimani city na ndugu yetu Adong Odwaa alierudishwa kwao Uganda...tulipewa stories km hizi ila uliza udsm inapata how much kwa mwaka, unaweza kutoa chozi...ila siku zote ukweli unatabia ya ku surface ht km utachelewa...sema ndo hua unatoka while madhara yashajitokeza na hakuna namna inabidi tu mvumilie maumivu...
Haya mambo ya mwekezaji ana collect kila kitu then anatoa gawiwo itamfanya mwekezaji kila mwaka ana diclear loss or small profit ili atoe gawiwo kubwa...
SGR ya kenya mpaka leo mwaka wa 4 ina make loss kutokana na uendeshaji wa kichina..
Kifupi chinese are the colonizers...be aware
Alafu muda wao ukiisha wanakuachia magofu na ardhi yako isiyo na faida tena maana imekua turned into desert
 
Ingawa umeandika analyitically lakini unaupigia debe mradi wa bandari ya Bagamoyo utekelezwe kinyume na maamuzi ya JPM kuwa usitekelezwe. Nami naona nikujibu kiuchambuzi kwa nini usijengwe. Katika uchambuzi huu nitatumia pia hoja za wengine wenye mawazo kama yako.

Kwanza, Ndugai mwanzoni kabisa alisema kuwa Magufuli alishauriwa vibaya. Wote tunamfahamu Magufuli kama mtu makini sana katika kusoma document hata iwe kubwa kiasi gani si rahisi kumchomekea kitu asikione, pili kati ya Ndugai na JPM ambaye anaweza asiwe na access ya document ni Ndugai lakini sio JPM kwa kuzingatia nafasi yake hivyo hoja ya Ndugai kuwa Magufuli alishauriwa vibaya haina mantiki kabisa ila Ndugai aliitumia kama gia ya kutaka kujenga uhalali wa kureverse maamuzi ya Magufuli kuhusu kukataa kujengwa kwa bandari hiyo.

Mnaoupigia debe mradi huo mnadai kuwa bandari ya Bagamoyo ina kina kirefu maji hayajai na kupwa hivyo ndio sehemu inayofaa kujengwa bandari ya kupokea meli hizo kubwa na kuwa bandari ya DSM haiwezi kupanuliwa kuchukua meli kubwa za mita mia tatu au mia nne. Sasa kwa nini mkataba ukataze kujenga bandari ya DSM au nyingine yeyote kuanzia Tanga hadi Mtwara? Hao wawekezaji na nyinyi mnaogopa nini hiyo bandari ya Bagamoyo kushindana na bandari zingine za Tanzania? kwa nini mnaikingia kifua dhidi ya bandari zingine? Busara ya kawaida hapa ni kuwa wao kama wangewekeza (japo mimi napinga) basi wangekuwa tayari kwa ushindani na sio kutaka upendeleo wa kipekee.

Mnadai meli kubwa ndizo zitakuwa zinatia nanga bandari ya Bagamoyo sasa kwanini hamtaki hizo meli mnazoziita ndogo ziendelee kutia nanga katika bandari ya Dsm, Tanga na Mtwara? Kwa nini mnataka kuziua bandari zingine ikiwa lengo ni bandari ya Bagamoyo kuhudumia meli kubwa za mita mia tatu au mia nne?

Pia mnadai kuwa meli kubwa zitaleta mizigo Bagamoyo kisha baada ya kupakuliwa mizigo hiyo itabebwa na meli ndogo kupelekwa sehemu zingine! Uongo ulioje! Hizo sehemu ni zipi? Jiografia ya Tanzania ni kuwa sisi tumezungukwa na nchi sita zisizo na bandari ambazo ni Malawi, Zambia, Congo Mashariki (ingawa atlantic ocean wanayo), Rwanda, Burundi na Uganda. Nchi tatu za mwisho huwa tunashindana na Kenya katika kugombania mizigo yao hivyo wanaotutegemea kabisa ni nchi tatu za mwanzo. Pia hata kwa Zambia huwa tunashindana na bandari ya Durban. Mizigo inapoletwa katika bandari zilizopo hubebwa kwa reli na malori kupelekwa huko katika nchi hizo hivyo suala la meli ndogo ndogo kuichukua mizigo na kuisambaza haina mantiki kabisa, Pia jiografia ya Africa, mizigo inayokwenda Africa kaskazini au Magharibi kutoka Asia ni rahisi kupita Suez canal, mediteranian kisha kwenda huko hivyo haiwezekani mizigo yao ije huku East Africa kisha irudi huku North au west Africa. Hali kadhalika kwa mizigo inayotoka bara la America haiwezi kuletwa huku kwetu kisha ipakiwe tena kwenda West Africa au hata South Africa. Pia mizigo ya Africa Kusini inayotoka Asia haiwezi kuletwa Bagamoyo kisha ipakiwe tena kwenda Africa Kusini. Ni wazi mizigo ya Africa Kusini kutoka Asia moja kwa moja inapelekwa bandari ya Durban ambayo ni bandari kubwa. Hivyo hoja kuwa sisi tutakuwa tunahudumia mizigo ya nchi zenye bahari kama sisi ni hoja mufilisi isiyo na mashiko. Sisi urefu wa Kamba yetu utaendelea kuwa nchi zisizo na bandari zinazotuzunguka tu na ambazo zinahudumiwa vyema na bandari za DSM, Tanga na Mtwara vizuri na kwa ufanisi.

Reli ya kutoka bandari ya Mtwara hadi Mbababay ikikamilika, tutakuwa na uhakika wa kuihudumia Malawi kwa ufanisi zaidi kuliko bandari ya Bagamoyo. Hali kadhalika bandari ya Tanga imepanuliwa na SGR ikikamilika mizigo ya Congo Mashariki, Rwanda, Burundi, Uganda itahudumiwa kwa ufanisi zaidi.

MAPATO

Serikali kupitia mamlaka ya bandari inapata pesa za handling na storage ya mizigo pamoja na kodi/tozo mbali mbali za forodha zinazokusanywa na TRA kutokana na meli zinazotia nanga katika bandari ya DSM, Tanga na Mtwara; lakini bandari ya Bagamoyo ikijengwa mamlaka hizo hazitakusanya mapato huko na wakati huo huo bandari hizo zitakuwa zimeminywa meli zisitie nanga huko, badala yake mapato hayo na mengine ambayo projections zinaonyesha yataendelea kukua yatakuwa yanachukuliwa na wawekezaji hao toka China na Oman kutokana na meli kutia nanga bandari ya Bagamoyo, ujinga ulioje. Tuwe wakweli hata bandari hiyo ya Bagamoyo ikijengwa asilimia kubwa ya meli zitakazokuwa zinatia nanga ni hizi hizi zinazoitwa meli ndogo ambazo kwa sasa zinatia nanga bandari za Dsm, Tanga na Mtwara. Wakina Ndugai wanapigia debe hata haya mapato tunayoyapata sasa kupitia bandari zetu tuyakose badala yake yakusanywe na kuchukuliwa na wachina kwa kisingizio mradi una manufaa. Mbona hawatauambii quantifiable revenue amount ambayo tutakuwa tunapata bandari ya Bagamoyo ikifanya kazi badala yake wamekalia kusema mradi una manufaa sana lakini hawatupi figure?



UJENZI WA VIWANDA

Hoja nyngine ambayo inapigiwa debe na kufungamanishwa na ujenzi wa bandari ni ujenzi wa viwanda katika ukanda huo wa Bagamoyo. Swali rahisi hivi ni lazima mtu akitaka kujenga viwanda lazima ajenge na bandari? Kama hao wawekezaji wana nia ya kujenga hvyo viwanda hawajakatazwa kwani eneo la Bagamoyo ni moja ya meneo yaliyoainishwa kama EPZ, Hivyo wanaweza kuja kupitia TIC na kupewa ruhusa ya kujenga viwanda. Jambo la msingi wajenge viwanda kwa terms zilizo sawa na wawekezaji wengine katika EPZs zingine na wasipewe upendeleo wa kipekee kuliko wawekezaji wengine wanaojenga viwanda. Ukipita barabara ya Kilwa kuelekea Mkuranga, njia ya Chalinze na Tanga, utaona kuna viwanda vya wachina vimejengwa/vinaendelea kujengwa; mbona hao hawakufungamanisha ujenzi wa hivyo viwanda na ujenzi wa bandari ya Bagamoyo?

Ujenzi wa viwanda na ujenzi wa bandari ni vitu viwili tofauti ambavyo mwekezaji hana uhalali wa kulazimisha kuwa lazima afanye vyote. Amekataliwa bandari ajenge hivyo viwanda. Kama atahitaji bandari za kuimport raw materials au export ya bidhaa zake atatumia bandari zilizopo. Hoja kuwa bandari ya Bagamoyo ikijengwa na viwanda 700 vitajengwa haina mashiko kwa sababu hayo mambo mawili siyo lazima yafanyike pamoja.

Hoja yako kuwa China inaitambua Bagamoyo katikampango wake wa Belt and Road sisi haituhusu kwani hiyo ni mikakati yao ya kuitawala na kuinyonya dunia. Kwani hata kama tungeamua kujenga bandari ya Bagamoyo ni lazima wajenge wachina? Hatuwezi kujenga kwa nguvu zetu?

Watu wanapopata nafasi za uongozi wajifunze kuiga uzalendo kama ambavyo viongozi wa mataifa ya Uchina na mengine yaliyoendelea wanavyoweka maslahi ya nchi zao mbele hata kama ni kwa kunyonya nchi zingine.

Bandari ya Baagamoyo ikifanikiwa kujengwa basi itakuwa ni ufisadi kama ufisadi mwingine uliokuwa unafanyika huko nyuma hususan awamu ya nne.

kwenye hili nafikiri mchina anataka njia ya uhakika ya kuchukua malighafi kutoka DRC , Zambia na hata Tanzania. Kufanikisha hili wanataka bandari watakayo iendesha wao na reli. Bandari ndio hiyo ya Bwagamoyo na reli wanaitaka TAZARA. Nafikiria pia wanataka njia hiyohiyo itumike kuleta bidhaa kutoka kwao kwa mauzo huku wanakokuita bara jeusi.
 
KC wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe amesema kitu ambacho wabunge wengi hawakijui ni kwamba Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa makubwa kutoka huko duniani ambazo hatujawahi kuziona hapa Tanzania

Kisha hizi meli tunazoziona zikileta mizigo Dar port ndio zitakuwa zinabeba miizigo kutoka Bagamoyo na kusambaza sehemu mbalimbali duniani amesisitiza Zitto

Tusiiache fursa hii jamani na siyo kweli kwamba kila mradi ulioanzishwa awamu ya Kikwete ulikuwa mbaya kwani hata reli ya SGR mradi uliasisiwa vizuri na serikali ya JK lakini serikali ya awamu ya tano imekuja kuutekeleza kwa namna tofauti, amemalizia Zitto.

Chanzo: Clouds 360
Sawa mameli makubwa makubwa tunayataka lakini kwanini hawataki TRA yetu ikusanye kodi kwa miaka zaidi ya 30? Tupe sababu
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Alafu muda wao ukiisha wanakuachia magofu na ardhi yako isiyo na faida tena maana imekua turned into desert
Udsm wataachiwa magofu pale mlimani city km sio majengo yaliyopoteza mvuto baada ya hio miaka 50...wasomi ila hamna kitu, watu wanaingia mikataba kwa maslai binafsi
 
Back
Top Bottom