Zitto Kabwe: Membe alitupigania dhidi ya tabia Mbaya ya Watu wenye Mamkala kutumia Wahuni kutukana Viongozi wenzao

Zitto Kabwe: Membe alitupigania dhidi ya tabia Mbaya ya Watu wenye Mamkala kutumia Wahuni kutukana Viongozi wenzao

Msipo wasamehe watu makosayao hata baba yenu wambinguni hata wasamehe.

Put it in your mind.
Maisha ya mwanadamu ni fumbo. Huwezi kujua ni nani anasamehe, na nani anasamehe.
 
Huyo ni narcissist,yeye kila event atahakikisha anaigeuza inakuwa it's all about him.Sasa hivi utakuta hana habari na kinachoendelea kwenye tukio,yupo anaranda randa mitandaoni kuona watu wame react vipi kwa speech yake.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mnaofatilia msiba wa Membe nafikiri mnamsikiliza sasa Zitto akimuelezea marehemu Membe.

Zitto badala ya kumuongelea Membe anaushambulia utawala wa Magufuli mpaka kumuita JPM mpuuzi.

Na kwanini wenzake wamepewa dakika mbili ila Zitto kapewa dakika zaidi. Zitto anachafua hali ya hewa...
Weka na ka clip
 
CCM ukweli upo wazi na haupingiki mmemfanya vibaya kwenye historia ya marehemu Benard Membe kipengele cha siasa ,mmeshindwa kuelezea alihama CCM na kugombea Urais kupitia Act wazalendo, hivyo hivyo pia kwa msemaji wa familia

Zitto kabwe umefanya vizuri kuwakumbusha waweke record vizuri ya historia ya marehemu kupitia siasa , lakini kwangu mimi Zitto kabwe atabaki kuwa mwanasiasa mnafiki.
Alikuwa mgombea wa CCM kupitia ATC WAZALENDO.
Alikuwa planted tu kule msijitoe ufahamu.
 
Huyo Zitto kutoa maneno hayo vepee?? Si aungane nae wakafukiwe wote huko Rondo km ana mkubali sana huyo marehemu.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Mkuu kwa hiyo kuguswa na msiba ni kutaka kuthubutu kuzikwa na marehemu?!!!
 
Lolote limhusulo Muumba wetu, hakuna wa kumpangia maana hekima ya Mungu si hekima ya mwanadamu.

Tunaweza kuona tunanena vyema sana, kumbe ikawa ni takataka mbele zake. Tunaweza kumwona mtu akinena takataka, lakini ikawa ni hekima mbele za Mungu.

Lakini pa.oja na hizo hali zote, hatuwezi kuacha kunena, ila yeye ndiye mwamuzi.
[emoji2956][emoji2956]
 
Zitto Kabwe amewaponda wote walioshabikia upuuzi aliofanyiwa Membe wakati Ule huku wengine wakimchafua kwa magazeti yaliyochapishwa na Mitambo " Vyombo"

Zitto anesema ana Imani wale wote waliomchafua Membe na kumtendea Uovu watajuta na wataenda kuomba radhi kaburini kwake

Source: ITV
Ayatolla Zitto ni idiot kabisa. Rais Dkt Samia kaongea vizuri mno. Ila kwa hii hotuba nahisi Ayatolla kaingia 18 za Mama, sijui, huwezi dharau mamlaka kiasi kile
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki ibada ya kuaga Mwili wa Marehemu Mhe. Bernard Kamillius Membe, Waziri Mstaafu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika Viwanja vya Karimjee - Dares Salaam leo tarehe 14 Mei, 2023



Saa 4:00 Asubuhi
Viongozi Mbalimbali wa Kiserikali wakiongozwa na Waziri Mkuu wameanza kuwasili

Saa 5:45 Asubuhi
Mwili wa Marehemu Bernard Membe umewasili Karimjee ukiwa umebebwa kwenye gari Maalum la kubebea Maiti.

Saa 6:00 Mchana
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan anawasili.

Rais Samia amekwenda moja kwa moja kusaini kitabu cha Maombolezo kilichoandaliwa, kisha kusalimia na kuwapa pole wafiwa.

Saa 6:05 Mchana
Dua na Sala kutoka kwa viongozi mbalimbali wa Dini kisha salamu za viongozi wa Kiserikali na Kisiasa wamekaribishwa kutoa salamu zao.

Zitto Kabwe anazungumza; Amemuelezea Bernard Membe kama Mwanasiasa mkomavu aliyepambana kulinda heshima yake dhidi ya watu waoga walioshindwa kumkabili kwa hoja, ambapo baadhi ya viongozi na Watu wenye Mamkala walitumia Wahuni kutukana Viongozi wenzao.

Amesema Ushindi wake katika kesi ile utazika utamaduni huu mbaya wa kushambulia na kuchafua watu.

“Wewe sio tu ulizuia na kukemea upuuzi ule, bali ulihakikisha unatoa mfano kwa mpuuzi aliyebebeshwa upuuzi ule ili kuwa funzo kwa wapuuzi wengine wote”

Amesema kuwa anataraji wale wote waliohusika na mambo yale watamuomba radhi akiwa kwenye umauti.

View attachment 2621369
Zitto Kabwe
Aidha, amemsifu kwa kusimama imara katika nyakati ngumu ambazo taifa lilipitia, nyakati ambazo watu wengi waliogopa kuisimamia kweli.

Amemshukuru kwa kujiunga na Chama cha ACT Wazalendo ambapo aliwapa mafunzo na kuamsha ari ya kufanya kazi kwa bidii.

“Umetimiza wajibu, upumzike pema Membe… Tangulia BM, umeacha simanzi kubwa kwa watanzania. Bwana ametoa, Bwana ametwaa. Upumzike pema mzee wangu Membe” Zitto Kabwe

Daniel Chongolo (Katibu Mkuu CCM) anazungumza; Amesema Chama cha Mapinduzi kimepokea kwa Masikitiko na Mshituko mkubwa kifo chake.

View attachment 2621375

Daniel Chongolo, Katibu Mkuu CCM

Amesema CCM imepoteza kada wake mkubwa, na amewaomba watanzania na wana CCM kuenzi mema yake kwa kusimamia maslahi ya watanzania ndani na nje ya nchi.

Stergomena Lawrence Tax, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anazungumza; Ametoa pole kwa mjane wa Marehemu pamoja na watoto kwa kuondokewa mpendwa wao.

Amesema wakati wa uhai wake alitekeleza kazi zake kwa weledi mkubwa hasa katika kukuza uhusiano mwema kati ya Tanzania na mataifa mengine ambao nchi imenufaika sana na kazi zake.

View attachment 2621403
Stergomena Lawrence Tax, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Alichangia katika kujenga mipango mizuri kwenye sera za nje.

Amemshukuru Membe kwa kumtia Moyo wakati alipoteuliwa kugombea ngazi ya kimataifa ambapo alikuwa nae bega kwa bega kuanzia hatua za mwanzo na muda wote wa kazi.

Rais Samia Suhulu Hassan anazungumza; Amesema kifo ni jambo lisiloepulika kwa binadamu, na wote tumepokea kwa huzuni taarifa hizo za kifo cha Membe.

Serikali, Familia ya Rais na watanzania wote tunaungana kwa pamoja kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na wanalindi wote kwa kumpoteza mpendwa wao.

View attachment 2621413
Samia Suhulu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Rais amemsifu kwa kuwa mtu muungwana na kaka wa karibu aliyekuwa tayari kusadia wengine. Amesema maamuzi ya Mungu huwa hayalaumiwi bali hushukuriwa.

Amemalizia kwa kuwaomba watanzania kumuombea Membe roho yake ipumzike kwa amani.

Nape Nnauye anazungumza; Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye akizungumza kwa niaba ya familia amemshukuru Rais Samia kwa kusimama bega kwa bega na familia ya Marehemu katika wakati huu mgumu ambapo gharama nyingi za msiba huu ikiwemo usafiri zimebebwa na Rais mwenyewe.

View attachment 2621415
Nape Nnauye anazungumza; Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
Ameishukuru Wizara ya Mambo ya nje kwa kuwabeba, kwa moyo wa upendo walioonesha. Heshima hii hawataisahau.

Amewashukuru viongozi wote wa Serikali na Mkoa, Madaktari wa Hospitali ya Kairuki, majirani, waombolezaji, ndugu, jamaa na marafiki wote kwa umoja walioonesha.

Saa 7:30 Mchana:
Jeneza linafunguliwa ili waombolezaji watoe heshima za mwisho. Rais Samia anawaongoza waombolezaji

 
Pole Mama Samia kwa kuondokewa na mtu wa karibu.

Pole JK kwa kuondokewa na rafiki yako.

Pole kwa Watanzania wote

Apumzike salama jasusi mbobevu. Ni safari yetu binadamu wote. Zingine zote mbwembwe tu zetu wanadamu...
Kama ni mtu wao wa karibu wakazikwe nae waandae makaburi manne…! Hakuna ujasusi hapo….utapeli mtupu…jasusi si alipata chanjo? Kwa hiyo kakorona kamemuua jasusi?
 
Salamu za Zito kabwe zimelenga kumsimanga hayati Magufuli na kuonyesha kwamba,Membe alikuwa bora kuliko Magufuli ikiwemo kuendekeza mtifuano kwenye taifa hili ,inahitaji akili kubwa kulitambua hilo alilifanya Zito kabwe
Ayatolla Zitto ni idiot. Huwezi linganisha Dkt Magufuli na Membe. Dkt Magufuli kalifanyia makubwa hili taifa na aligusa maisha ya kila mtanzania. Ila wezi na mafisadi ndiyo walikona cha moto.
 
"Mungu tunaomba umlaze ndugu yetu pahala pale ambapo wewe utaridhia", hayo ni maneno ya Sheikh Walid. Hakunaga unafki wa "mlaze mahali pema peponi".
Safi sana…tunaomba awaombee na wale wanaotaka kuzikwa nae…..
 
Back
Top Bottom