Zitto Kabwe: Sitagombea tena Uongozi ndani ya ACT WAZALENDO, najikita kwenye Ubunge. Malengo yangu ni kuwa Rais wa Tanzania

Zitto Kabwe: Sitagombea tena Uongozi ndani ya ACT WAZALENDO, najikita kwenye Ubunge. Malengo yangu ni kuwa Rais wa Tanzania

Kichaa peke yake ndio anaweza mchagua mtu mdini kama zitto, na kuhusu urais hilo asahau

Ninakazia:

Kujikita kwenye udini hakumlipi yeyote si Zitto wala yeyote ukiwamo wewe.

"Mada nzima haina popote Zitto alipotamka neno dini, kutaja dini wala kiashiria."

Hoja ya udini ni mfu na mahsusi kwa mafukara wa hoja.
 
Ninakazia:

Kujikita kwenye udini hakumlipi yeyote si Zitto wala yeyote ukiwamo wewe.

"Mada nzima haina popote Zitto alipotamka neno dini, kutaja dini wala kiashiria."

Hoja ya udini ni mfu na mahsusi kwa mafukara wa hoja.
Huwezi kumtenga zitto na udini popote pale
 
Hivi kung'atuka Kwake mbona imekuw hoja ya kila siku au ndiyo mafanikio ya chama?

Hata ukitoka uongozini chama chenyewe kinafanya kazi Tunduru-Kigoma mjini-Magomeni na Pemba tu. Kina life circle ya Mende.
Jamaa ni lichawi... hapo linaroga ili CDM ife na halijafanikiwa!! Sura baya roho mbaya jitu la hovyo sana hilo.
 
Akiongea na redio hiyo ya kimataifa jana mchana, mwanasiasa huyo amefunguka:

View attachment 2933149

Kwamba:

1. Ameamua kunga'atuka kwa mujibu wa katiba akikiacha chama kikiwa katika hali bora zaidi kuliko wakati wowote.
2. Hatarejea kwenye uongozi wa chama hicho kama katiba inavyotaka, kwani muda wake umekwisha; bali atasalia kuwa mwanachama.
3. Anayo imani kubwa na waliochukua hatamu za uongozi na kuwa hana shaka, chama kipo katika mikono salama.
4. Mzee Duni kujitoa katika kinyang'anyiro cha uchaguzi, hakukuwa na shinikizo lolote.
5. Malalamiko yao kwenye "serikali yao ya nusu mkate Zanzibar" karidhika na alipofikia na yaliyopo ya nini kitafuata.
6. Kuwa anapanga kurejea bungeni agombee 2025.
7. Chama kikimhitaji kwa ushauri au kushiriki vikao yuko radhi.
8. Anazo ndoto za urais wakati wake ukifika, na hasa 2030 na huko mbele lakini si 2025.
9. Anaamini kwenye siasa za kuleta mabadiliko; kuwa hizo ziko bungeni.
10. Anatambua mbunge aliyepo Kigoma ni aliyetangazwa tu, lakini siyo aliyeshinda.
11. Kuhusu uchaguzi 2025 kuwa huru na haki; anaamini mazingira yatakuwa bora zaidi 2025, kwani 2020 yalikuwa mabaya mno na kuwa heri tungerejea hata kwa yaliyokuwa 2015.
12. Mabadiliko yaliyopo sasa kuwa hakuna kupita bila kupingwa, wenyeviti na makamu watapatikana tokea kwenye mchakato wenye usaili wa waombaji, nk yanatia moyo.
13. Kuhusu madai ya u CCM B wake; hajawahi kuwa CCM, amekuwa upinzani muda wote, hajawahi kuunga mkono juhudi. Hata hivyo anatambua siasa zake ni tofauti na za wengine, ambalo hilo ni suala binafsi.

Maneno kuntu kabisa kutoka kwake Zitto Zuberi Kabwe.

Kwa hakika kama asemavyo Prof. Lwaitama adui yetu ni mmoja:

Lwaitama: Kwenye maslahi ya nchi, adui yetu ni CCM
Chama kilimshinda ,je anaweza kua RAIS wa nchi?

Sorry,I dont believe that
 
Xi

ZItto sijaanza kumjua leo.
kama umekwenda shule vizuri nadhani utakuwa unafahamu kitu kinachoitwa tathmini. Matendo, kauli, mienendo na misimamo ya mtu over time inakuwa basis ya evaluation. Niliyoyasena kuhusu Zitto ni matokeo ya tathmini yangu ambayo sio lazima wewe ukubaliane nayo. Only time will tell.

Zitto kutokana na kuutaka sana urais wakati akiwa hajafikisha miaka 40 ambayo ndio umri kikatiba mtu anaruhusiwa kugombea urais hapa TZ. aliwahi kuomba umri wa kugombea urais upunguzwe ili tu aweze kuqualify ; leo hii amefikisha 40 lakini hana kiu ya kugombea urais hadi 2030. Kwa tabia ya CCM mwaka 2030 most likely mgombea wake atakuwa mkristo ndio maana Zitto atagombea mwaka huo. Zitto ni kama Lipumba.

Rejea ukosoaji wa zitto wakati wa Magufuli na Mkapa halafu revisit wakati wa KIikwete na sasa.

Pitia michango yangu yote humu jf, mimi huwa naanalyse hoja objectively tofauti na wewe ambaye uko subjectively.

Nimeweka wazi kuwa siipendi CHADEMA lakini nikakiri ukweli kuwa vyama ni viwili tu CCM na CHADEMA.

Tusubiri next moves za Zitto.
Nimesoma bandiko lako vzur lakini nimefikia hitimisho kwamba wakati wa harakati za Zitto ama ulikuwa shule ama ulikuwa underbed na hivyo hukupata kujua kilichoendelea..
Hoja yako ya kumjua Zitto labda niseme kati yako na Saed Kubenea jipime nnan anayeweza kuwa alimjua/anamjua Zitto.Mwaka 2019 Saed Kubenea alikuwa mhariri wa Mwanahalisi nadhan alikuwa kinara wa kurusha mawe kwa Zitto kwa makala na kiujumla gazeti lake loote.Unajua baadae Saed Kubenea alijoin kwa Zitto.Hapa itoshe kusema zile makala hukuwah kuzisoma huenda ulikuwa shule..
Hoja ya kuupigania umri wa urais kushushwa,hapa napo uko shallow sana mzee.Zitto kiasili ni mwanamabadiliko kama haujui nikupe taarifa ndio mtu pekee aliyeanzisha au kupambania vijana kuwa bungeni,mwenyew alikuwa kijana mdogo tu kuingia bungeni na aliwapa morale vijana wengine kuingia bungeni.So alijua ujana sio kikwazo cha kushika hatamu,thats y.Kwanini hataki kugombea Urais sasa hivi(!)hilo halikuhusu coz kwenye siasa utakuwa mtu mjinga kufanya jambo bila kutazama mazingira kama yapo favourable.Naomba nikupe mfano ili ujue kuwa ni vzuri kutazama mazingira kabla ya kufanya maamuzi.Wakati wa Magufuli Chadema hamkuandamana kwanini(wakati katiba inaruhusu,mliogopa nn)?..Jibu hapo ni mazingira ya kisiasa..
Hoja ya ukosoaji wa Zitto wakati wa Magufuli,Kikwete na sasa.Kwanza unaonekana haujui chochote kumhusu Zitto na ama haumfuatilii aina ya siasa zake.Kwani ukosoaji wa CHADEMA dhidi ya viongozi hao tofautitofauti unafanana?In every action there must equal and opposite reaction.Ukosoaji unaendana na nguvu ya utendaji wa Serikali!
Umeweka waz kwamba huipendi CHADEMA lakini umeficha kwamba UNAIPENDA CCM.Infact ACT huielewi and thats ok.Mtu asiyeelewa jambo huwa ni mjinga katika jambo hilo.Bado unamuda wa kutosha unaeza kujieleimisha au laa huwez wapigie Simu DR.Slaa,Saed Kubenea na wengine weengi watakwambia whos Zitto is.😅
 
Kwanza ni uwongo kuwa ameng'atuka. Yeye amemaliza muda wake wa uongozi kwa mujibu wa katiba ya ACT.

Watu wengi wana akili ndogo. Wanakuza jambo dogo lionekane la ajabu!

Nyerere alinga'atuka. Mwinyi, Mkapa na Kikwete walimaliza muda wao kwa mujibu wa katiba, na wala halikuwahi kuwa jambo la ajabu kiasi cha kuongelea kila siku.

Huwezi kusema kuwa Mwinyi, Mkapa au Kikwete waling'atuka. Labda kama hujui Kiswahili wala maana ya neno kung'atuka.

Umewahi kumsikia Kikwete akisema kuwa aling'atuka? Halafu ikawa hadithi ya kila siku? Kama katiba ya ACT ina muda maalum wa kiongozi kuwa kwenye nafasi fulani, kuna nini cha ajabu?
Hiki chama huwa tunakiita CCM- mazambarao. Ngoja nikuonyeshe walivyo wanafiki. Mwaka 2020 waliingia kwenye kile walichokiita serikali ya umoja wa kitaifa. Hii ni baada ya kudhulumiwa uchaguzi, baadhi ya viongozi wake na pia wananchi kupigwa na polisi na kuumizwa, na wengine kuuawa. Walipoingia kwenye serikali ya umoja wa kitaifa, kuna makubaliano walifanya na CCM-kijani ili kuhakikisha makovu ya uchaguzi yameponywa. Baada ya viongozi wake kupewa magari yenye ving'ora na kina Zitto kuingizwa kwenye kamati zisizo na maana, walisahau kabisa kabisa yale makubaliano waliopanga na CCM-kijani ili waingie kwenye serikali. Muda wote wa 2020 mpaka 2024, wako kimya, mwaka huu wameona uchaguzi unakaribia, wanajifanya kusema watajitoa kwenye serikali ya umoja. Yaani kipindi chote kilichopita walikuwa kimya, wameona uchaguzi unakaribia, wakaanza kuhofu watawaambia nini wananchi, hasa wale walioumizwa, ndiyo wamekumbuka shuka.
 
Akiongea na redio hiyo ya kimataifa jana mchana, mwanasiasa huyo amefunguka:

View attachment 2933149

Kwamba:

1. Ameamua kunga'atuka kwa mujibu wa katiba akikiacha chama kikiwa katika hali bora zaidi kuliko wakati wowote.
2. Hatarejea kwenye uongozi wa chama hicho kama katiba inavyotaka, kwani muda wake umekwisha; bali atasalia kuwa mwanachama.
3. Anayo imani kubwa na waliochukua hatamu za uongozi na kuwa hana shaka, chama kipo katika mikono salama.
4. Mzee Duni kujitoa katika kinyang'anyiro cha uchaguzi, hakukuwa na shinikizo lolote.
5. Malalamiko yao kwenye "serikali yao ya nusu mkate Zanzibar" karidhika na alipofikia na yaliyopo ya nini kitafuata.
6. Kuwa anapanga kurejea bungeni agombee 2025.
7. Chama kikimhitaji kwa ushauri au kushiriki vikao yuko radhi.
8. Anazo ndoto za urais wakati wake ukifika, na hasa 2030 na huko mbele lakini si 2025.
9. Anaamini kwenye siasa za kuleta mabadiliko; kuwa hizo ziko bungeni.
10. Anatambua mbunge aliyepo Kigoma ni aliyetangazwa tu, lakini siyo aliyeshinda.
11. Kuhusu uchaguzi 2025 kuwa huru na haki; anaamini mazingira yatakuwa bora zaidi 2025, kwani 2020 yalikuwa mabaya mno na kuwa heri tungerejea hata kwa yaliyokuwa 2015.
12. Mabadiliko yaliyopo sasa kuwa hakuna kupita bila kupingwa, wenyeviti na makamu watapatikana tokea kwenye mchakato wenye usaili wa waombaji, nk yanatia moyo.
13. Kuhusu madai ya u CCM B wake; hajawahi kuwa CCM, amekuwa upinzani muda wote, hajawahi kuunga mkono juhudi. Hata hivyo anatambua siasa zake ni tofauti na za wengine, ambalo hilo ni suala binafsi.

Maneno kuntu kabisa kutoka kwake Zitto Zuberi Kabwe.

Kwa hakika kama asemavyo Prof. Lwaitama adui yetu ni mmoja:

Lwaitama: Kwenye maslahi ya nchi, adui yetu ni CCM
Kwahiyo huko ACT wazalendo hakuna mgombea urais zaidi ya Zitto na ni kazima chama kimpitishe.
Huyu bado kiongozi na ana maamuzi huko ACT.
 
Huwezi kumtenga zitto na udini popote pale
Mimi ni nani kumtenga mtu na lolote? Au wewe ni nani kumuunganisha mtu na lolote kama yeye hajatamka mwenyewe kwa maneno au maandishi yake?

Nisiache kuwaka angalizo hili:

1. Moderator kulikoni mmebadili title kutoka iliyokuwapo na kuchapia kama wanafunzi wa primary?

2. Kwani title iliyokuwapo:

DW: Zitto afunguka yakiwamo ya u CCM B

Ilikuwa na tatizo gani?
 
Kwahiyo huko ACT wazalendo hakuna mgombea urais zaidi ya Zitto na ni kazima chama kimpitishe.
Huyu bado kiongozi na ana maamuzi huko ACT.

1. Sijasikia kwenye mahojiano hayo kuwa hakuna mgombea mwingine ila yeye.

2. Nikadhani kutokea hapo #1 hata kama ACT wakimpendekeza 2025 hatakubali ila labda 2025.

3. Kutokea #1 na #2 nikadhani labda wasipompendekeza 2030 atagombea tu like jua au mvua ikibidi ugombea binafsi.

4. Hudhani Kwa mukthadha huo hitimisho lako laweza kuwa si sahihi?
 
CCM ndiye adui yetu mkuu na sio zitto wala nani

1. Kasema sana Prof. Lwaitama. Tatizo zaidi ninadhani ni makamanda uchwara wasioweza kutambua umoja wetu ulikuwa muhimu zaidi kama kipaumbele:

a) Lwaitama: Kwenye maslahi ya nchi, adui yetu ni CCM

b) CHADEMA wa Mtandaoni watamwelewa lini Dr. Lwaitama?


c) Tuwatambue wanaohaha kutusambaratisha kama Taifa

2. Ajabu na kweli makamanda kama hao wako radhi kushirikiana na CCM ikibidi lakini si dhidi ya mpinzani mwenzao.

3. Ya zama zile Mbeya ni kama haya haya.

4. Kwamba tunasaka ustaa, au kumfurusha CCM?

Al Watani, Bams, JokaKuu, Economist
 
Kuhusu 'u-CCM B' wake amejibu kuwa hilo ni suala binafsi, hapo nimeelewa vema.

1. Tatizo ni kutaka kumuwekea maneno mdomoni:

13. Kuhusu madai ya u CCM B wake; hajawahi kuwa CCM, amekuwa upinzani muda wote, hajawahi kuunga mkono juhudi. Hata hivyo anatambua siasa zake ni tofauti na za wengine, ambalo hilo ni suala binafsi.

Tatizo sugu la makamanda uchwara.

2. Clip Iko pale rejea kusikiliza vizuri. Kama vipi hakikisha dishi haliyumbi yumbi.

3. Hoja zake haziwezi kupingwa Kwa viroja na hasa mbele ya wenye kutafakari juu ya nani anasema Nini.
 
Nipe mfano wa chama kingine cha upinzani ambapo mwenyekiti au kiongozi wake ameheshimu ukomo wa uongozi kikatiba hapa Tanzania!..
Ukishindwa jitambue kuwa wew ni zwazwa
Zwazwa mwenyewe chawa wa CCM. Ukiona kiongozi bado yupo kwenye cheo Ina maana katiba bado inampa muda. Wewe kweli jinga la CCM . Huyo Zito kaondoka maana katiba inatambua miaka kumi. Sasa hapo unamsifu ya Nini? Yani Kikwete kamaliza miaka kumi ya uongozi, halafu mnaanza kumsifu wakati katiba imemlazimisha. Acheni unafiki
 
1. Kasema sana Prof. Lwaitama. Tatizo zaidi ninadhani ni makamanda uchwara wasioweza kutambua umoja wetu ulikuwa muhimu zaidi kama kipaumbele:

a) Lwaitama: Kwenye maslahi ya nchi, adui yetu ni CCM

b) CHADEMA wa Mtandaoni watamwelewa lini Dr. Lwaitama?


c) Tuwatambue wanaohaha kutusambaratisha kama Taifa

2. Ajabu na kweli makamanda kama hao wako radhi kushirikiana na CCM ikibidi lakini si dhidi ya mpinzani mwenzao.

3. Ya zama zile Mbeya ni kama haya haya.

4. Kwamba tunasaka ustaa, au kumfurusha CCM?

Al Watani, Bams, JokaKuu, Economist
Shida yako una hasira na CHADEMA kuliko CCM . Mnaboa Sana nyie wanafiki wa ACT
 
Akikujibu, mrejesho wako tafadhali.
Mrejeshi wa Nini? Nimeshamjibu. Ukiona kiongozi wa chama Cha siasa yupo madarakani Ina maana Katiba inamruhusu kuendelea. Huyo Zitto Katiba ya ACT ilimwekea limit ya miaka kumi. Sasa unafiki wenu mnadhani ni hiari yake. Acheni hizo.
 
Hiki chama huwa tunakiita CCM- mazambarao. Ngoja nikuonyeshe walivyo wanafiki. Mwaka 2020 waliingia kwenye kile walichokiita serikali ya umoja wa kitaifa. Hii ni baada ya kudhulumiwa uchaguzi, baadhi ya viongozi wake na pia wananchi kupigwa na polisi na kuumizwa, na wengine kuuawa. Walipoingia kwenye serikali ya umoja wa kitaifa, kuna makubaliano walifanya na CCM-kijani ili kuhakikisha makovu ya uchaguzi yameponywa. Baada ya viongozi wake kupewa magari yenye ving'ora na kina Zitto kuingizwa kwenye kamati zisizo na maana, walisahau kabisa kabisa yale makubaliano waliopanga na CCM-kijani ili waingie kwenye serikali. Muda wote wa 2020 mpaka 2024, wako kimya, mwaka huu wameona uchaguzi unakaribia, wanajifanya kusema watajitoa kwenye serikali ya umoja. Yaani kipindi chote kilichopita walikuwa kimya, wameona uchaguzi unakaribia, wakaanza kuhofu watawaambia nini wananchi, hasa wale walioumizwa, ndiyo wamekumbuka shuka.

Umeandika mambo ya kushangaza:

1. Unajua wanachama wa hicho chama leo ndiyo hao hao waliouliwa na kuumizwa 2020?

2. Unajua wanachama wa hicho chama ndiyo hawa hapa:



3. Tunawazodoa wapi hao #1 na #2?

4. Kama wao kama sisi tuliingia kwenye maridhiano mezani na CCM kusaka nusu mkate?

5. Kulikoni nusu mkate yao ni haramu ila yetu?

6. Ulitafakari kweli yote yakiwamo hayo kabla ya kuwaangushia tuhuma labda zisizo wahusu?

7. Kulikoni tusijikite kusaka umoja badala ya mifarakano dhidi ya adui yetu?
 
Back
Top Bottom