Zitto: Msaidizi wa Maalim Seif alinipigia simu mara 4 kutaka kunijulisha msiba sikupokea ndipo akanipigia Rais Mwinyi nikapokea kwa mujibu wa sheria

Kwani kuna tofauti na wale wanaojiaminisha kwamba tatizo lipo wakati halipo ?

Wanasiasa wote ni walewale, By the way karne hii kiongozi anachohitaji ni Diplomasia, hio ni maradufu ya ubabe....
 
Hivi Kuna sheria inayohusiana na kupokea simu za viongozi?
 
Kuna mtu alimwaga chozi kwenye msiba wa Mkapa pale uwanjani
Kumwaga machozi na kuogopa kupokea sim havifanani
Hata mwenye furaha anaweza kumwaga machozi kama ilivyo kwa mwenye huzuni, hilo ni tendo lisilo la hiari
 
Kumwaga machozi na kuogopa kupokea sim havifanani
Hata mwenye furaha anaweza kumwaga machozi kama ilivyo kwa mwenye huzuni, hilo ni tendo lisilo la hiari

Acha kuleta bla bla hapa,msiba na machozi ya furaha wapi na wapi?
 
Mbona simu ya Rais Mwinyi aliipokea wakati maudhui ni yale yale?

Ila nimekuelewa sana bwashee!
 
Ukimuamini M Mungu unayaelewa kabisa maneno ya Zitto, lakini ukiwa na akili ya kibinaadamu tu ni vigumu kuelewa maelezo yake.

Nakumbuka mtangazaji wa CNN akimhoji mwanasaikolojia maarufu akifanya kazi CIA (shirika la kijasusi marekani). Kazi yake kubwa ilikuwa ni kuwashawishi watekaji wa ndege/watu wabadili mawazo yao na waweke silaha zao chini ili wajisalimishe. Alimuuliza swali moja linalolingana na hilo: " Inakuwaje mnapoteza muda kuwashawishi watekaji ambao wameshadhamiria kufa na wapo tayari kwa lolote wajisalimishe?" Jibu lake alisema: Katika kila dakika mioyo yao inaweza kubadili mawazo na kufikiri pengini siku yangu ya kufa sio leo na wakasubiri kesho yake au siku nyingine.

Ninachotaka kukueleza ni kuwa hata huyo afisa wa CIA akikutwa kisawasawa moyo wake unaweza kuwa mlaini kuliko wako, na ukashangaa hivi aliwezaje kupata nafasi kubwa kama hiyo!

Kifupi mwanadamu yeyote jinsi M Mungu alivyomuumba, moyo wake ni dhaifu kweli kweli kuliko unavyofikiria wewe. Lakini kulifahamu hilo inabidi umjue M Mungu.
 
Zitto bado kijana mdogo, msimshambulie sana..
 
Mungu huwa anatuepusha mengi sana,

ile nafasi ya Urais huwa sio kwa kila mtu,

Ni Mungu pekee ndiyo anampa anayeona anafaa,
 
Muha kweli muha,kwa kupenda sifa, zamani Waha utawasikia ukiwe kwenye treni usiinite Kalumanzira niite braza K.
 
Kiongozi ambaye hasikilizi wasaidizi๐Ÿค”๐Ÿค”๐Ÿค”๐Ÿค”
Kutopokea sim ya msaidizi wa maalim seif ni dharau. Sijui kama za wasaidizi wengine na wananchi zinapokelewa
Hapo hajakua raisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ