Zitto: Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema...

Zitto: Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema...

Status
Not open for further replies.
Bahati nzuri zaidi ni kwamba tangu uvumi huu umeanza hadi hii leo, niliamua kiwa kimya kabisa na kuto comment jambo lolote kwenye mtandao wowote ule wa kijamii.
Kuhusu kututimia mitandao kufanya yenye tija ujue tu kwamba mtandaoni yapo mengi nimesha yafanya na naendelea kuyafanya

Kwa hiyo hao waliocomment kwenye huo uvumi hawana lolote la maana wanalofanya kwenye mitandao, mpaka upendekeze hatua dhidi ya hizo smart phones? Kwenye huo uvumi hisia nyingi za watu ilikuwa ni jinsi hawaridhishwi kiongozi wao mkuu anavyowatendea na hawana jukwaa lolote rasmi wanaruhusiwa kufanya hivyo.

Ni vyema ungejikita kwenye hisia za hao watu wamefikaje huko, na sio kuleta vitisho vya kubana watu kukidhi hisia za kiongozi. Ushauri wa kujipendekeza hauna maana karne hii ya 21.
 
Una nia gani na Rais wetu kwa hiki ulichokuwa umekiweka? baadaye unakuja na ngonjera za alinacha....
tapatalk_1571583600825.jpeg
 
Kumekuwa na tabia ya kuzusha taarifa kuhusu Viongizi na Serikali zinazoleta taharuki kwa jamii.

Wahusika na udhibiti wa taarifa mitandaoni wafanye msako kwa kina kuwatia wahalifu hao korokoroni ili iwe fundisho kwa wengine.

Hatuwezi kuona Kila wakati mambo kama haya yanatokea.
 
KIGOGO AGARAGAZWA ROUND YA KWANZA,ZITTO & CO WAMTELEKEZA UJERUMANI.

Leo 16:00pm,20/10/2019.

Siwezi kuamini kama taifa kubwa duniani kama Tanzania linaweza kuendeshwa na propaganda za Kigogo,Zitto,Shangazi,Tundu,Maria na Lissu.Niwatake radhi kwa kuwaita ninyi ni wapumbavu na upumbavu wenu ni kuwa sehemu ya mchezo huu mchafu unaofanywa na Upinzani nchini Tanzania.

Kinachonifanya nianze-kupoteza imani juu ya Uzalendo wa Wapinzani ni jinsi watu kama kigogo wanavyotunga uwongo na kuusambaza duniani pasipo kuwa na tone la aibu,hata kufikia kusambaza uzushi wa kifo cha Mkuu wa Nchi,

Hivi ni kweli Wapinzani hamna mnachofahamu juu ya uzima,ugonjwa au kifo cha Mkuu wa Nchi kama ni kifo cha Taifa na mkwamo wa Taifa hata muanze kusambaza uzushi mkijua madhara yake,Enyi wapinzani fedhea na aibu mliyoipata kwa uzushi wa Uwongo mtawaambia nini Wafuasi wenu hata wakawaelewa,wapumbavu wakubwa ninyi.

Sasa ukweli umedhihirika kama haya tunayoambiwa Watanzania na Viongozi wa Upinzani ni uwongo uwongo na kamwe hatutawaamini tena.

Nawataka radhi kwa kuwausisha na mambo yasiyoafa kwa kuwa daima mmekuwa mkifurahia kigogo anavyosema na pengine kuitia aibu nchi, kama haya mambo ya kigogo ambaye mnamjua na mnamficha kwa kuwa ninyi nyote mna uwezo wa kuitumia account hiyo ya Kigogo,

Sasa mkijua Kigogo analishwa uwongo ama anapata data zisizo za kweli kutoka kwenye vyanzo vya uwongo na nyinyi Wapinzani mnajua hivyo na mnashirikiana na hao kina kigogo kutudanganya,

Ni wakati sasa umefika mtapima wenyewe kama kweli bado mnahadhi ya kutambulika kama ninyi ni Upinzani wenye tija au tuendelee kuwa na CCM kwa miaka 100 ijayo,Shame on you Kigogo,Zitto,Membe,Shangazi,Maria na Mazwazwa yote yanafuatilia account ya kigogo2014.

-Kigogo apigwa Home and Away.

Asubuhi nilisimama yalipokuwa mataa ya ubungo ambapo hivi sasa inajengwa Ubungo Interchange nikajiuliza mara kumi;Je kama asemayo huyu kigogo ni sahihi inamaanisha hii Ubungo interchange tunaikosa tena maana mwenye maono hatokuwepo tena,nikakumbuka treni ya Umeme nikajisikia nasema huyu shetani kigogo ashindwe kabisa lazima niende Morogoro nikamcheki Baba na Mama kwa treni ya Umeme nikitumia saa moja,

Lazima niende Makao makuu ya nchi,Dodoma na treni ya Umeme lazima niende Mwanza kwenye harusi ya mdogo wangu kwa treni ya Umeme,hakika habari ya kigogo kwa sekunde chache ilinifanya nifikirie mengi sana,Mungu ni mwema kumbe nilikuwa naota na kamwe naikemea ndoto hiyo isiwe kweli.

Niliingia kwenye whats up nikakutana na neno toka kwa Maregesi likisema,Hata uwe mwema kiasi gani tukumbuke huwezi kulazimisha watu wote wakupende na huwezi kupendwa na kila mtu hata kama umeboresha maisha yake.

Kama kiongozi fanya wajibu wako na daima Uzalendo ukuongoze kuwaandalia ajira kizazi cha tatu na cha nne na uheshimu wengine hakika utakuwa na wengi wa kukupenda kuliko kukuchukia.

Tukumbuke kila kiongozi ana watu wampendao na wamchukiao kila mtu kwa muono wake,wengine wakimpenda kwa mema afanyayo kwa manufaa ya Taifa zima lakini wengine wakimchukia kwa wivu kwa kuwa anatenda zaidi yao,neno hilo nikakubaliana nalo.

-Wenye hekima watavuna heshima, lakini wapumbavu watapata fedhea.

Watu wameshikia bango Serikali ikanushe au iseme ukweli juu ya kinachosemwa mitandaoni,lakini itajihusisha vipi na uwongo wa kutungwa ni sawa mtu abishanie jinsia yako wakati wewe unajijua mwenyewe,sasa ya nini kubishana nae.

Nilikumbuka kazi ya shetani ni kama hiyo tuliyoiona ikifanywa na Kigogo na wafuasi wake wakishangilia mabaya,tumeuona uovu mioyoni mwa watu waliojivika moyo wa kihayawani.

Moyo wa kihatlyawani na upumbavu,kufurahia ama kifo au ugonjwa uwapo kwa ndugu zao. Hawa ndiyo mashetani.

Kigogo anaonyesha mchoro wa moyo,nahisi wameamua kujipeleka wao icu baada ya Kumuona live Mkuu wa nchi,Wakapata heart attack wao na yule bwana wao kigogo wote wametokomea ujerumani,sasa wamelazwa huko Frankfurt.

-Kigogo proved failure 100%%%

Kuna jamaa huko twitani anamlaumu Kigogo, eti yeye hajulikani ila amewatia aibu kubwa wafuasi wake ambao wanajulikana.

Kigogo nae anamlaumu Zitto kwa kumpa tango pori na kukiri kuwa tutapata malipo kwa Mungu kutokana na matango pori wanayowalisha watu.

Wapinzani walikubali kushikiwa akili na kigogo ni hatari kwa mustakabari wao kisiasa.

Lakini je Kigogo kaleta taharuki,Watanzania tumejifunza nini, nataka kujua tumejifunza nini juu ya hili?

Ndugu zangu wakati wa Mwanadamu si wakati wa Mungu na awazayo Mwanadamu siyo awazayo Mungu,Kusudi la Mungu kwa mtu mwenye haki halitakatizwa na binadamu yeyote .Ahsante Mwenyezi Mungu kwa ajili ya neno lako ambalo ni kweli,Ahsante Mwenyezi Mungu kwa kudhihirisha tena Ukuu wako katika Taifa la Tanzania,Ahsante kwa kuibariki Tanzania,Ahsante kwa kumlinda na kumbariki Rais wetu John Pombe Magufuli sasa na siku zote.

Nikiishia hapa,Mimi ni,
Msemakweli Chakubanga.
Dar es Salaam.
0755078854.
 
Vizuri, aache sasa roho mbaya na visasi. Nadhani amejifunza ni namna gani Wananchi wake wengi wanavyomtakia mabaya (kifo), na wapo tayari kufanya sherehe muda wowote iwapo mauti yatamfika. Akiendeleza kiburi shauri yake.
 
Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema:

Mosi: Afya ya Rais wa nchi ni maslahi ya taifa na inapaswa kutofanyiwa soga. Afya ya Rais inahusika na maslahi ya nchi yetu ndani na nje. Tusiuendee uvumi huu kwa papara. Tuwe watulivu, tuipe nafasi Serikali na mamlaka zake zitupatie taarifa kamili na kwa wakati unaofaa.

Inawezekana kuwa katika hali hii ya sintofahamu baadhi yetu tumefanya mambo yanayotafsirika kuombea mabaya kutokea. Binafsi naomba radhi kwa tafsiri hizo hata kama haikuwa nia wala madhumuni.

Pili: Tuendeleze tunu yetu ya utu, umoja na mshikamano ambazo tumeachiwa na Mwalimu Nyerere ambaye tumetoka kuadhimisha miaka 20 ya kifo chake wiki iliyopita. Tusiruhusu chuki kuteka mijadala yetu. Chuki haiwezi kuwa jawabu la chuki. Utu ndio jawabu sahihi la chuki.

Tatu: Ni busara kwa Serikali kuwaondoa hofu wananchi juu ya uvumi huu maana kutofanya hivyo kunazua taharuki inayoweza kuepukika. Ikiwa kweli Rais wetu amepata dharura ya kiafya kama uvumi unavyosema basi haitakuwa mara ya kwanza kwa hilo kutokea nchini.

Watanzania ni waelewa na wenye mapenzi na wenye utu. Tumeona walivyowaombea marais wao Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete walipopata matatizo ya kiafya wakiwa madarakani. Naamini wataungana na kusimama pamoja kama taifa kumuombea Rais wetu na nchi yetu.

Zitto Kabwe, Mb
Kiongozi wa ACT Wazalendo
Kibingo, Mamlaka ya Mji Mdogo Mwandiga, Kigoma
20/10/2019
Jiwe walilolikataa waashi limekua jiwe kuu la pembeni, nikupongeze kwa kuomba radhi ni jambo la hekima na kwa nia ileile usisite kumuomba radhi mweshimiwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli.
 
Vizuri, aache sasa roho mbaya na visasi. Nadhani amejifunza ni namna gani Wananchi wake wengi wanavyomtakia mabaya (kifo), na wapo tayari kufanya sherehe muda wowote iwapo mauti yatamfika. Akiendeleza kiburi shauli yake.
Sema mawakala wa shetani na mafisadi wanaoipata joto ya jiwe!
 
Hawatasahau Jumapili ya leo

Kigogo aka mimi nilishajiambia.. tangu zamani ni wa sebuleni

Gemu hili nimelipenda sana.. zaidi ya zilizopita. Hadi signature nayo ikacheza😀



 
Huyu kigogo asingekuwa anonymous, sijui Leo ingekuwaje. Hivi kisheria kupublish kifo cha kiongozi wa Nchi hususani amiri jeshi sio uhaini?
 
Yaani ni kama wamemchokoza nyati. Wataomba poo. Na sisi wakianza kuminywa wasitukimbilie. Tutawapa za mbavu waende kwa makaburu wanaowatumia.
 
Bado mnamuwaza Tundu tu! Haya endeleeni lkn mtambue dhambi ya kutaka kumuua Tundu kwa watanzania wenye akili haisafishishiki hata kwa propaganda gani!! Hata mungemuweka kwenye jeneza huyo nduli, tungemnanga tu!
 
mimi nahisi huyu kigogo ni spin doctor wa serikali, imefika wakati watu wajifunze.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom