Zitto: Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema...

Zitto: Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema...

Status
Not open for further replies.
Jomba unaacha kazi ya kumpikia mmeo unahangaika na waume za watu..unachekesha..kwanini usitafte mme mwingine kwani lazima huyu mzee
Kwa sababu wewe umeolewa na unalala bila chupi unadhani wote wanaolewa.

Ni aibu sana kwa mpuuzi kama huyu kigogo kuteka akili za wasomi, ni kielelezo cha kuwa na taifa la wapenda mizaha ya kitoto.
 
Maswali mawili kwa mleta mada: Huo uvumi kwa mara ya kwanza uliupata kwa nani na muda gani!? Kwa nafasi uliyonayo kama kiongozi wa kisiasa nchini ulichukua hatua gani kupata uhakika wa 'uvumi" huo kutoka vyombo sahihi vya nchi!?
===
Najua ni mara chache sana kujibu maswali kutoka kwa kapuku kama sisi. Hivyo sitashangaa kutojibiwa maswali yangu haya.
 
wewe ulitudanganya sijui hawala yako anafanya kazi na rais kumbe uongo wa kitapeli tu
Hawara yangu ? ???Wewe mimi nina mme wangu jamani. Ni kweli Rais anaumwa. Sema hajafa kama wazushi walivyozusha.
 
Hawara yangu ? ???Wewe mimi nina mme wangu jamani. Ni kweli Rais anaumwa. Sema hajafa kama wazushi walivyozusha.

Ulitudanganya mumeo anafanya kazi na Rais, acheni kubadili maneno kuumwa ndio nini?! Hata mafua ni ugonjwa mlisema yuko ICU Ujerumani [emoji23]
 
Hawara yangu ? ???Wewe mimi nina mme wangu jamani. Ni kweli Rais anaumwa. Sema hajafa kama wazushi walivyozusha.
dada angu lakini usiwage too emotional na vitu vya kuambiwa juzi ulipagawa kabisa utajipa presha bure kumbe idara ipo kazini kigogo ni mpiga bangi tu kama mwinjaku
 
Ulitudanganya mumeo anafanya kazi na Rais, acheni kubadili maneno kuumwa ndio nini?! Hata mafua ni ugonjwa mlisema yuko ICU Ujerumani [emoji23]
Mme wangu Yes. Sasa Nilikudanganya wapi?Nimebadili maneno wapi?
 
Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema:

Mosi: Afya ya Rais wa nchi ni maslahi ya taifa na inapaswa kutofanyiwa soga. Afya ya Rais inahusika na maslahi ya nchi yetu ndani na nje. Tusiuendee uvumi huu kwa papara. Tuwe watulivu, tuipe nafasi Serikali na mamlaka zake zitupatie taarifa kamili na kwa wakati unaofaa.

Inawezekana kuwa katika hali hii ya sintofahamu baadhi yetu tumefanya mambo yanayotafsirika kuombea mabaya kutokea. Binafsi naomba radhi kwa tafsiri hizo hata kama haikuwa nia wala madhumuni.

Pili: Tuendeleze tunu yetu ya utu, umoja na mshikamano ambazo tumeachiwa na Mwalimu Nyerere ambaye tumetoka kuadhimisha miaka 20 ya kifo chake wiki iliyopita. Tusiruhusu chuki kuteka mijadala yetu. Chuki haiwezi kuwa jawabu la chuki. Utu ndio jawabu sahihi la chuki.

Tatu: Ni busara kwa Serikali kuwaondoa hofu wananchi juu ya uvumi huu maana kutofanya hivyo kunazua taharuki inayoweza kuepukika. Ikiwa kweli Rais wetu amepata dharura ya kiafya kama uvumi unavyosema basi haitakuwa mara ya kwanza kwa hilo kutokea nchini.

Watanzania ni waelewa na wenye mapenzi na wenye utu. Tumeona walivyowaombea marais wao Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete walipopata matatizo ya kiafya wakiwa madarakani. Naamini wataungana na kusimama pamoja kama taifa kumuombea Rais wetu na nchi yetu.

Zitto Kabwe, Mb
Kiongozi wa ACT Wazalendo
Kibingo, Mamlaka ya Mji Mdogo Mwandiga, Kigoma
20/10/2019
Kaka zitto wakati mwingine mnajishushia heshima, kwa kiongozi kama wewe kuungana na wazushi wa mitandaoni ni fedheha , kupitia hili mjifunze kuchunga midomo siyo kila kitu ni siasa.
 
Ulitudanganya mumeo anafanya kazi na Rais, acheni kubadili maneno kuumwa ndio nini?! Hata mafua ni ugonjwa mlisema yuko ICU Ujerumani [emoji23]
Mimi nilisema yupo Dar,ni wapi nilisema yupo Ujerumani ?
 
dada angu lakini usiwage too emotional na vitu vya kuambiwa juzi ulipagawa kabisa utajipa presha bure kumbe idara ipo kazini kigogo ni mpiga bangi tu kama mwinjaku
Pressure ipi sasa ? Nijipe pressure na ukweli naufahamu ?
 
Kuna somo amejifunza, kama ataendelea kuwa mbishi tu shauri yake.
 
Huyu ndio wale wale... Alikuwa mstari wa mbele na lema kubonga bonga uzushi na kumsapot kigogo.... Mambo yamejamba anazuga kuleta busara.


Washakumark.. Kuwa mpole tu
 
Zitto ni mnafiki yeye naye ndio alikuwa ana eneza uvumi huo na uzushi hahahaha koma acha unafiki bora uendelee kuwa mchawi kuliko kuwa mnafiki!
Alilishwa Tangopori akatapika uongoo.Sasa baadae akashtuka amesema uongo kwa Twitter kama Kigogo,akaamua kuja huku jf kujisafisha kimtindo.Waliomdanganya kwakweli wamemuaibisha
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom