Elections 2015 Zitto: Sitagombea Urais wala Ubunge 2015

Elections 2015 Zitto: Sitagombea Urais wala Ubunge 2015

Haya sasa,
Wale vijana njaa kali wa chadema na wazush wazush na wakaanga sumu kama masaa manane na yericko mdandia nasaba ya nyerere waichukue taarifa hii kama fundisho kwao,

Na ya kwamba mwenzao zitto anaish maisha yake,wao wakibaki kuyachunguza na kuyafuata fuata maisha yake,wanadhani kila mtu anaweza tumain siasa kama maisha ya kudumu kama wao,

Na sasa wajipime na waone je wanaweza kuufuata moto huo??

Badala ya kuyaish maisha yao,wao wako busy kuyaish maisha ya wenzao,

People with Sad Destiny...

Ushauri wako unawalenga watu kama @Mwigulumchemba @NapeNnauye
 
Sipati picha jinsi gani Dr Slaa atakavyo furahishwa na hii habari. Babu relax, Zitto is no longer your threat.

uamuzi wa Zito ni uamuzi mgumu na unahitaji mtu mwenye busura sio kama wewe Mwigulu (Hamy D)unapongeza kinafiki kama mtoto wa nje ya ndoa
 
CDM watakuja kujua umuhimu wa Zitto baadaye. Zitto ni jembe sana ndani ya CDM Hana siasa za maji taka Kama akina Lissu, Lema na Sugu. Hakuna asiyejua mchango wa Zitto kwa CDM. Hawa vijana akina Lema hawajengi CDM Bali wamekidhoofisha sana chama kwa siasa zao za maji taka. Pumzika kaka pumzika Zitto


Acha uchochezi kwani zzk amesema anakihama chama?Kila Mbunge wa cdm ana mchango wake kwa chama na kwa Taifa kwa jumla.Umaarufu wa wabunge wa cdm unatokana na kuwa cdm, nje ya cdm sio lolote sio chochote kwa wananchi waliochoshwa na UDHALIMU wa ccm.
 
sixgates Kila mwenye macho na akili timamu ameiona kazi aliyoifanya Zitto Kabwe CHADEMA,
Unachokiongea hakina uhalisia,
Haki isemwe tuh,hata kama ni inachomachoma,kazi aliyoifanya inafahamika na kila mwenye akili timamu
 
Last edited by a moderator:
haya na Mh.Lowasa nae aseme basi kama anampango au laa 🙂
 
Sidhani kama Zitto ni Msafi kama tunavyomdhania. Vile vile sidhani kama Chadema itateteleka kwa sababu ya kuondoka mtu mmoja. Inabidi ifike wakati kwamba Chadema haitegemei Zitto, Mbowe, Slaa au Mnyika peke yao. This is not a one man party. Ni chama cha watu, yes tunahitaji mchango wa Zitto lkn kama hatuwezi kuchukua madaraka kwa sababu Zitto au Mbowe au Slaa hawapo basi we are not ready kuongoza taifa.
All the best Mr Zitto in your future career.
 
mnyama mwenye sifa za mamalia na ndege POPO.....

Zitto is a Trator yeye na wengine wengi wa CCM na CDM wanajua....

Unajua is better to be loyal to the team than to the truth...,,,,kwenye jeshi wale traitors toka jeshi jingine wakiwaletea habari jeshi jingine mwishoni wale wale wanao pewa habari humuuwa yule mpashaji habari maana wanajua atafanya hivyo kwao pia ...anakuwa hana muamana.

Ningependa kuona upinzani unaimarika zaidi ni muhimu katika ustawi wa nchi ,haipendezi kuona mtu yuko upinzani akitumiwa na chama tawala downlow .Hata chama pinzani chochote kikichukua nchi na kuwa chama tawala still vyama vitakavyokuwa vya upinzania vitakuwa na umuhimu ule ule katika ustawi wa taifa hasa as watch dog


Hata kama unakuja na ID Mpya stil unafahamika wewe ni nani,
Tafuten kazi za kufanya na mjifunze kuish maisha yenu,
Kazi aliyoifanya Zitto Chadema ni kubwa na hadi hivi sasa hakuna mahala alipoonesha ni msaliti,hata viongoz wenzake wanalitambua hilo,
Jiamin,huna haja ya kutumia ID Mpya,Zitto sio size yenu
 
Nadhani wengi wa supporters wa chama chenu kwenye JF nadhani mna "Psychosomatic disorders", mnaanzisha uchuro ili mjadili watu. Mnaudhi sana.
 
Kila mwenye macho na akili timamu ameiona kazi aliyoifanya zitto kabwe chadema,
Unachokiongea hakina uhalisia,
Haki isemwe tuh,hata kama ni inachomachoma,kazi aliyoifanya inafahamika na kila mwenye akili timamu

ukweli gan mkuu, ukweli huonekana hausemwi, uwongo husemwa. Huna sababu ya kutumia nguvu nyingi kutuambia tuone aliyoyafanya Zitto. Kama yapo tutamhukumu kwayo..

Mimi ni muumini wa performaance ya kiongozi wa chama ndani ya chama. Zitto hajafanya lolote kwaa kipindi kirefu kuijenga chadema zaidi amekuwa mtu anaeleta tension na niseme amegundua weakness iliyopo chadema na anaitumia hiyo kuwanyanyasa.

Mfano chadema inapigwa propaganda ya Udini kuwa ni chama cha wakristo. Zitto ni muislam (anitumia hii turufu kuwaacha chadema kwenye mkesha zitto akiondoka itachafua political climate).. Chadema inapigwa propaganda ya ukabila na ukanda (Zitto analijua hili coz yeye ni wa kigoma na muha, anawalaza chadema usiku kucha milango wazi kuombea asiharibu political climate). Chadema inapigwa propaganda ya viongozi wake kukimbia shule..yeye ana shule hivyo kumdeny nayo inawasumbua chadema.

Zitto awepo ndani ya chadema, aondoke ndani ya chadema bado sufferings za chadema zitaremain constant. Ndio maana nasema Zitto ashajiona ni zaidi ya taasisi, anapenda hata jambo alilolifanya chadema lisisemwe chadema wameamua hivi, anataka lisemwe Zitto kaamua hivi. Ni mjinga.
 
Chuki gan ninayo dhidi ya Zitto? BTW ZZK anaamini ili uwe mwanasiasa mzuri lazma urotate katika media iwe kwa negative or positive. Anaamini ili uwe vichwani mwa wananchi lazma uwajengee controversy to keep them into big awaits. Anaamini kuwa baadhi ya watu ni zaidi ya taasisi km anavyojiona yeye..which is wrong..hata taasisi ya ndoa ili ikamilike inahitaji watu wawili, familia inahitaji watu, hivyo hata chama kinahitaji watu. ZZK is no body km sio chadema ila chadema will remain firm without Zito, dokt slaa au hata mbowe. Huwa watu wanacheza na taasisi hawajui nguvu yake.

Taifa ambalo haliheshimu taasisi limekufa. Zitto anahisi ni maarufu kuliko chadema kumbe sio kweli, arudishe mawazo yake nyuma afikiri upya.

Hitimisho lako ni zito sana, una ushahidi wowote kwamba hivi ndivyo alivyo, au ndio mtindo huohuo wa hisia kuzibadilisha kuwa kweli? Wazungu wanasema: 'we suspect in others what we feel in ourselves'. Yaani wakati mwingine binadamu huwa tunawaza kitu fulani akilini mwetu na kujiona sisi tulivyo na kudhani na kujiaminisha kwamba hivi ndivyo walivyo watu wengine. Angalia ndugu yangu usije ukawa hivyo ulivyo ukadhani na wengine ndivyo walivyo!!
 
Haya sasa,
Wale vijana njaa kali wa chadema na wazush wazush na wakaanga sumu kama masaa manane na yericko mdandia nasaba ya nyerere waichukue taarifa hii kama fundisho kwao,

Na ya kwamba mwenzao zitto anaish maisha yake,wao wakibaki kuyachunguza na kuyafuata fuata maisha yake,wanadhani kila mtu anaweza tumain siasa kama maisha ya kudumu kama wao,

Na sasa wajipime na waone je wanaweza kuufuata moto huo??

Badala ya kuyaish maisha yao,wao wako busy kuyaish maisha ya wenzao,

People with Sad Destiny...

Kwa amani kabisa wapumzike kumsumbua zito wawatu.
 
Hitimisho lako ni zito sana, una ushahidi wowote kwamba hivi ndivyo alivyo, au ndio mtindo huohuo wa hisia kuzibadilisha kuwa kweli? Wazungu wanasema: 'we suspect in others what we feel in ourselves'. Yaani wakati mwingine binadamu huwa tunawaza kitu fulani akilini mwetu na kujiona sisi tulivyo na kudhani na kujiaminisha kwamba hivi ndivyo walivyo watu wengine. Angalia ndugu yangu usije ukawa hivyo ulivyo ukadhani na wengine ndivyo walivyo!!

Umeshindwa kuvumilia hii misumari ya moto mwalimu wangu kwa hiyo umekuja kuokoa jahazi?Leo nimeamini kumbe wewe na Zitto huko cdm lenu moja.mbona hujawahi kuja kuwatetea akina slaa,mbowe na viongozi wengine au cdm kinapopigwa hapa?
 
CDM watakuja kujua umuhimu wa Zitto baadaye. Zitto ni jembe sana ndani ya CDM Hana siasa za maji taka Kama akina Lissu, Lema na Sugu. Hakuna asiyejua mchango wa Zitto kwa CDM. Hawa vijana akina Lema hawajengi CDM Bali wamekidhoofisha sana chama kwa siasa zao za maji taka. Pumzika kaka pumzika Zitto

Poleni sana..Drama za hilo jembe lenu hazijaaisha....hana umuhimu wowote zaidi ya kujitafutia umuhimu wa kuibukia.Jembe gani sasa km amekulia ktk chama hadi sasa hajajua anafit wapi?Watz wenye hata PHD na first classes kibao ni watu wa hovyo sana.Sijui Zitto hadi sasa ana nini cha tofauti na loosers za CCM.



Soon utasikia anacheza dili za kijinga km za makamba mwenzie ktk "un holy trinity Makamba, Zitto, Jussa".Watoto wa Uswazi ni wepesi sana kupanda na kuanguka ghafla.

Hakuna mtu asiye na mchango anaweza kukubalika sehemu, na mara nyingine ni chama kukutumia kwa kutuma ktk mambo mengi kutegemea na mazingira na hii ni sehemu ya majukumu ya kazi.


Sijui nani atafundishwa na Zitto ....zaidi ya material things biasness yake ktk vitu vyenye different school of thought.Wanafunzi wataishia kuwa km wa Haroub Othman.
 
kwa mpenda maendeleo ya nchi yetu hili ni pigo kwa wanaoujua michango ya zitto bungeni na kwenye kamati,hakika tutammisi sana!!!,nimesikitishwa na habari hii..
 
Hitimisho lako ni zito sana, una ushahidi wowote kwamba hivi ndivyo alivyo, au ndio mtindo huohuo wa hisia kuzibadilisha kuwa kweli? Wazungu wanasema: 'we suspect in others what we feel in ourselves'. Yaani wakati mwingine binadamu huwa tunawaza kitu fulani akilini mwetu na kujiona sisi tulivyo na kudhani na kujiaminisha kwamba hivi ndivyo walivyo watu wengine. Angalia ndugu yangu usije ukawa hivyo ulivyo ukadhani na wengine ndivyo walivyo!!

Maneno yako ni busara sana dr.
 
Back
Top Bottom