Zitto: Umeme wa Gesi ungezalisha MW 3,500 zaidi ya wa Maji

Zitto: Umeme wa Gesi ungezalisha MW 3,500 zaidi ya wa Maji

Kwaiyo yanaitwa maporomoko ya kidatu?

So jibu nilichouliza maana iwe maporomoko au bwawa lakini zote zina function aina moja ya power, kwanini tusifukie hayo maporomoko ya KIDATU?

Maana tunatakiwa kwenda na fasheni,wajuzi(Porofesa Muongo) na wanasema gesi ndio mpango mzima. Je nchi zinazotumia gesi as source of power wamefukia mabwawa na maporomoko yao?


Mkuu hata mimi naungana na wewe kwamba umeme wa maji unatufaa sana sisi kuliko huo umeme wa gesi nk,

Ila kuna aina mbili za umeme wa maji, ule wa maporomoko na ule wa kujenga bwawa, pale kidatu sio Bwawa bali ni maporomoko ya maji kutoka mlimani na hapo ndipo mashine zimetegwa na maji yanapoporomoka kutoka mlimani ndipo huendesha hizo generators kuzalisha umeme. Kuna ( falls na Dams). Linalotaka kujengwa huko stiegler ni Bwawa ambalo litahifadhi maji kisha zinawewa njia kwenye barrier (Dyke) ambapo katika hizo njia wataweka Generators na maji yanapopita kwa msukumo ndipo huendesha hizo generators.
 
Kwaiyo yanaitwa maporomoko ya kidatu?

So jibu nilichouliza maana iwe maporomoko au bwawa lakini zote zina function aina moja ya power, kwanini tusifukie hayo maporomoko ya KIDATU?

Maana tunatakiwa kwenda na fasheni,wajuzi(Porofesa Muongo) na wanasema gesi ndio mpango mzima. Je nchi zinazotumia gesi as source of power wamefukia mabwawa na maporomoko yao?

Ukipata pesa ukaamua kujenga nyumba ya kisasa ni lazima ubomoe ya zamani? Tulijenga uwanja wa Mkapa hapo pembeni ya wa taifa, mbona hatukuuvunja? Umeishiwa na hoja nini dogo.
 
mkuu uwe unaacha ujinga hata mara moja moja basi.

mbona siasa zinawaharibu hivi!!mnafanya haya kwa maslahi ya taifa kweli??

Umeshaishiwa na hoja, sasa pembeni wenye uwezo wa hoja waongee.
 
Uchambuzi wa ripoti ya CAG ulofanywa na chama cha ACT WAZALENDO inasema tulidharau na kuutupa mradi wa umeme wa gesi ambao tulishakopa fedha China wenye wenye uwezo wa kuzalisha MW 3500 tukakimbilia mradi mpya wa umeme wa Maji wenye kutoa MW 2110 kwa gharama ya Tillioni 6 matokeo yake tumekopa madeni mara mbili kwenye lengo moja.
Zito ni mzigo na si riziki!
Uchambuzi wa ripoti ya CAG ulofanywa na chama cha ACT WAZALENDO inasema tulidharau na kuutupa mradi wa umeme wa gesi ambao tulishakopa fedha China wenye wenye uwezo wa kuzalisha MW 3500 tukakimbilia mradi mpya wa umeme wa Maji wenye kutoa MW 2110 kwa gharama ya Tillioni 6 matokeo yake tumekopa madeni mara mbili kwenye lengo moja.Z

Uchambuzi wa ripoti ya CAG ulofanywa na chama cha ACT WAZALENDO inasema tulidharau na kuutupa mradi wa umeme wa gesi ambao tulishakopa fedha China wenye wenye uwezo wa kuzalisha MW 3500 tukakimbilia mradi mpya wa umeme wa Maji wenye kutoa MW 2110 kwa gharama ya Tillioni 6 matokeo yake tumekopa madeni mara mbili kwenye lengo moja.
Zito no zigo zito na si riziki, iko hivi:
Zito alishiriki kuuza gesi yetu yote kwa hati ya dharula. Na sasa gesi ina mwenyewe japokuwa anaichimbia Tanzania!! Hatuna maamuzi nayo! Tukiitaka lazima tuinunue kwa bei atakayotaka mwenye nayo. Ukweli huu wote zito anaujua. Baada ya kuiuza gesi Leo anataka tuwekeze kwa kutegemea gesi isiyo yetu! Kwa mfano bei ya gesi ikipandishwa tutalazimika kununua hivyo hivyo! Wakiamua kutuhujumu hatuwezi kuwa na ujanja!! Lakini gesi INA ukomo Wa uhakika ila maji hayana uko Wa uhakika! Zito tunakujua, unataka kutufanya watumwa Wa gesi yetu waliyoiuza.
 
Tukubali jambo moja, tulikuwa na kiongozi anayefanya maamuzi kwa kukurupuka.

Uliona wapi kiongozi anamfukuza mfanyakazi mwenye mkataba wa kazi kwa kuwauliza watu waliopo kwenye mkutano, 'Nimtumbue sasa hivi au nimwache?; Wananzengo nao wanajibu, "tumbua"; halafu mfalme anasema, "Kabwe, nimekwishakutumbua". Kweli unaamini huyo ni kiongozi anayeweza kutafakari kabla ya maamuzi?
Halafu baada ya kumtumbua, nafasi yake inachukuliwa na mwingine, THEN KESI MAHAKAMANI... WAKATI HUO NAFASI HIYO MOJA WANALIPWA WATU WAWILI KWA MWAKA MZIMA.. MTUMBULIWA NA MTEULIWA MPYA... gharama hizo hazisemwi
 
Ukipata pesa ukaamua kujenga nyumba ya kisasa ni lazima ubomoe ya zamani? Tulijenga uwanja wa Mkapa hapo pembeni ya wa taifa, mbona hatukuuvunja? Umeishiwa na hoja nini dogo.
Utakuwa juha! Ukipata pesa halafu unajenga nyumba ya kisasa kwenye kiwanja ambacho tayari ulishakiuza utakuwa juha!! Maana utaendelea kulipia pango la ardhi milele yote! Akikutishia kupandisha kodi ya ardhi unalazimika kumwabudu ili ubembeleze!
Iko hivi gesi yetu ilishauzwa!! Sasa tunaambiwa tujenge mitambo ya kuzalisha umeme Wa gesi, nani ajuaye gesi itauzwaje? Akikukatalia kununua kiasi cha gesi unachotaka utafanyaje? Akikupa sharti la kuruhusu usenge wakati nchi yote inategemea umeme wa gesi utafanyaje? Hivi inaingia akilini kuwekeza matrilioni kwenye rasilimali ambayo huna miliki nayo?
 
Je hii Stigler serikali inachimba yenyewe??
Anachimba na kujenga mkandarasi lakini bwawa na mitambo yote itamilikiwa na Tanzania. Lakini gesi wameshamilikishwa wageni sisi tumegeuka kuwa wateja! Hatuna kauli nayo!
 
Uchambuzi wa ripoti ya CAG ulofanywa na chama cha ACT WAZALENDO inasema tulidharau na kuutupa mradi wa umeme wa gesi ambao tulishakopa fedha China wenye wenye uwezo wa kuzalisha MW 3500 tukakimbilia mradi mpya wa umeme wa Maji wenye kutoa MW 2110 kwa gharama ya Tillioni 6 matokeo yake tumekopa madeni mara mbili kwenye lengo moja.
Wawekezaje wa huo umeme ni "thithi" kwa Mgongo wa wawekezaji wa "China" na hata huo wa Bandari ya Bagamoyo wawekezaji ni "thithi" mtaji fedha za sandarusi:
 
Anachimba na kujenga mkandarasi lakini bwawa na mitambo yote itamilikiwa na Tanzania. Lakini gesi wameshamilikishwa wageni sisi tumegeuka kuwa wateja! Hatuna kauli nayo!
Mbona mnapenda kujifariji na KUKERA?
 
Jamani umeme wa Gesi haufai pale kinyerezi kila Mwezi kufanya matengenezo ya mitambo ya MW 300+ ni bilioni Nne, na hiyo ni kila Mwezi, bado wanauziwa Gesi na TPDC ambao nao wanauziwa na mabeberu wanomiliki mitambo ya kuchimba mtwara na ndo wanaipanga Bei , mpaka sasa serikali Haina control na Bei ya umeme kwakuwa Bei ya gesi wanapanga mabeberu.

Stiglers itakuwa Mali ya tanesco yaani serikali. Sasa watu washapewa pesa wapigie debe Gesi Ili mabeberu wauze Gesi nyingi wapate faidi nyingi, umeme wa Gesi ni utoko
Wapiga debe wa mabeberu wanaolilia umeme wa gesi na bandari ya bagamoyo tuwaorozeshe hapa! 1. Propesa Muongo 2. Ziiitoooo Kerbbwe 3. Spuka Nndungayyi 4. Mzee wa Msoga (nyuma ya pazia). tuendeleze orodha hapa!
 
Tukubali jambo moja, tulikuwa na kiongozi anayefanya maamuzi kwa kukurupuka.

Uliona wapi kiongozi anamfukuza mfanyakazi mwenye mkataba wa kazi kwa kuwauliza watu waliopo kwenye mkutano, 'Nimtumbue sasa hivi au nimwache?; Wananzengo nao wanajibu, "tumbua"; halafu mfalme anasema, "Kabwe, nimekwishakutumbua". Kweli unaamini huyo ni kiongozi anayeweza kutafakari kabla ya maamuzi?
Kuna maamuzi lazima uyachukue immediately na hadharani ili watu wajifunze. Ndio maana mwizi anaiba sirini lakini anaadhibiwa hadharani. Marekani walionyonga Sadam Hussein na kusambaza hadharani video, same same kwa Gadafi.
 
JNHPP ni bora ukilinganisha na njia ya pili ambayo tayari kina JK walikua wameshaingia chaka..Mimi hapa hata ubaya wote(unaosemekana) kufanya namuunga mkono

Tatizo langu ni jinsi alivyokua Anafanya miradi hiyo. Kama vile anashindana na watu Fulani/wananchi anajaribu kuprove wrong,matokeo yake aliingia kwa haraka bila utafiti wa kimazingira na kifedha

Na mwisho wake tunaona sasa mradi umemaliza hela zote mtaani na una hatihati ya kutoka milima na pia mrad unatekelezwa kwa feasibility study ya mwaka 1970. Yaaani kama haya ni kweli na ule mradi utashindikana,ntaumiq sana mimi kwakua itakua ni muda wa kupigwa vizuri sasa na hawa wa ges. Na hasara kwa vizazi na vizazi

Vyovyote iwavyo hakuna mtu atanibadilisha msimamo wangu kuwa jamaa alikua ana mapenzi sana na malengo makubwa juu ya Tanzania,ila mawazo yalikua kichwani make,kuyabadili kuyatenda hilo ni swala la debate na tutamjadili kwa toka sasa na vizazi na vizazi
Achana na maneno ya uchochoroni, feasibility study ya mwaka 70s ni ipi na ya 2000s ni ipi? Kikubwa ni umeme uzalishwe. Waziri mkuu juzi amehakikishia uma kua mradi utakamilika kwa wakati
 
Achana na maneno ya uchochoroni, feasibility study ya mwaka 70s ni ipi na ya 2000s ni ipi? Kikubwa ni umeme uzalishwe. Waziri mkuu juzi amehakikishia uma kua mradi utakamilika kwa wakati
Maneno ya uchochoroni=Waziri mkuu

"Muheshimiwa yuko anachapa kazi ana mafaili mengi sana"- Msikitini, Njombe

Ni bora nimuamini CAG kuliko Mwalimu Majaliwa

Ila cha muhimu umeme uzalishwe tu ndio tunachotaka. Kwa hilo uko sahihi
 
Ukipata pesa ukaamua kujenga nyumba ya kisasa ni lazima ubomoe ya zamani? Tulijenga uwanja wa Mkapa hapo pembeni ya wa taifa, mbona hatukuuvunja? Umeishiwa na hoja nini dogo.
Ujamsikia POROFESA MUONGO dogo?
 
Uchambuzi wa ripoti ya CAG ulofanywa na chama cha ACT WAZALENDO inasema tulidharau na kuutupa mradi wa umeme wa gesi ambao tulishakopa fedha China wenye wenye uwezo wa kuzalisha MW 3500 tukakimbilia mradi mpya wa umeme wa Maji wenye kutoa MW 2110 kwa gharama ya Tillioni 6 matokeo yake tumekopa madeni mara mbili kwenye lengo moja.
Zitto anaweza kuwa na hoja lakini shida yake ni ukigeugeu wake ndiyo unatufanya wakati mwingine tusimwamini hata kwa mambo yenye ukweli ...hatabiriki
 
Maneno ya uchochoroni=Waziri mkuu

"Muheshimiwa yuko anachapa kazi ana mafaili mengi sana"- Msikitini, Njombe

Ni bora nimuamini CAG kuliko Mwalimu Majaliwa

Ila cha muhimu umeme uzalishwe tu ndio tunachotaka. Kwa hilo uko sahihi
Katika watu niliowapa credit na kuwaamini ni Majaliwa, lakini nimeshapoteza imani naye, hakuwa na sababu kulisemea jambo ambalo waumini hawakumuuliza swali
 
Uchambuzi wa ripoti ya CAG ulofanywa na chama cha ACT WAZALENDO inasema tulidharau na kuutupa mradi wa umeme wa gesi ambao tulishakopa fedha China wenye wenye uwezo wa kuzalisha MW 3500 tukakimbilia mradi mpya wa umeme wa Maji wenye kutoa MW 2110 kwa gharama ya Tillioni 6 matokeo yake tumekopa madeni mara mbili kwenye lengo moja.
Je, Zitto amezingatia na masuala ya climate change na mitigation zake kwenye hoja yake? Labda kama kuna teknolojia ya clean natural gas!
 
Uchambuzi wa ripoti ya CAG ulofanywa na chama cha ACT WAZALENDO inasema tulidharau na kuutupa mradi wa umeme wa gesi ambao tulishakopa fedha China wenye wenye uwezo wa kuzalisha MW 3500 tukakimbilia mradi mpya wa umeme wa Maji wenye kutoa MW 2110 kwa gharama ya Tillioni 6 matokeo yake tumekopa madeni mara mbili kwenye lengo moja.
Hiyo gesi faida yake yote si tulishanyang'anywa huyu zito nae ni puppet nini??
 
Back
Top Bottom