Yawezekana ila kiuhalisia ni ngumu Malawi 🇲🇼 kulob hata kule mahakamani. Ukishakua mnyonge at one point utakua mpira wa konaFuatilia kwa makini huu mgogoro utagundua baadae huu mgogoro utatuelemea.
Wenzetu wao wanaweka mpangilio fulani huko umoja wa mataifa ili waonekane wana haki na eneo lote
Nadhani haupo sahihi hapo kwenye Nyanza/ VictoriaRamani iko hivo miaka mingi kabla hata ya Google earth. Kuna siku kwenye ofisi ya ubalozi wa Ujerumani nchini Tanzania ilionekana ramani yenye kuonesha ziwa lote liko Malawi. Ramani za kimataifa zinaliita ziwa Malawi badala ya Nyasa, ni kama uamue kuliita ziwa Nyanza utaliita mwenyewe wengine wataendelea kuliita Victoria.
Malawi wakileta ushahidi wao lazima tutumie akili kuupinga. Sio kukariri resolution ya UN iliyo generalized. UN hawakugawa hizi nchi, waliogawana Tz na Malawi ni Wajerumani waliokuwa German East Africa (ikiwemo Tanganyika) na Waingereza waliokuwa Malawi. Ukitazama Heligoland treaties mbili ndio mpaka ule umewekwa. Sheria za mipaka ya Afrika zinaheshimu mgawanyo wa wakoloni bila kuubadilisha. Sasa Malawi wana treaty ya kwanza inayoonesha ziwa lote ni lao. Treaty ya pili inayoonesha ziwa linagawanywa tulitakiwa tuwe nayo sisi. Hatuna
Angalizo: Nimetumia memories za zamani nilivyoelewa hili suala. Sina uhakika sana
Nampiga mawe muonevu na nimeshaanza kuwapiga kimyakimyaUkiwa unaonewa unachukua hatua gani mkuu?.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Hii ndiyo hasara ya kuwa na Taifa ambalo halina Serikali.
Rudi tena usome historia ya mpaka katika ziwa Nyasa hiki ulichoandika siyo sahihi.Binafsi hiki kitu kilinifikilisha Sana enzi za jk na kujaribu kufuatilia habari mbalimbali, mwishowe nilifika kwenye ukweli mchungu ya kwamba ziwa nyasa lote ni la Malawi ingawaje wagawaji wa mipaka kipindi hicho yaani wakoloni walifanya makosa ya ugawaji kwa kutozingatia baadhi ya kifungu. Kifungu hicho ni kwamba mipakani Kama Kuna ziwa au bahari basi mpaka lazima upite katikati ili kila nchi inufaike na maji. Kwa kuzingatia kifungu hicho wareno ambao walikuwa watawala wa msumbiji walikaa mezani na waingereza ambao walikuwa watawala wa Malawi na kukubaliana kuchora mpaka upya ndiyo maana utaona katika ziwa,msumbiji na Malawi mpaka umepita katikati. Lakini kipindi hayo yanafanyika Tanganyika na Malawi zote zilikuwa chini ya waingereza, kwahiyo hawakuona haja ya kubadili mpaka yote ni makoloni yao na hali hiyo iliendelea mpaka hizi nchi zikapata uhuru. Sasa Malawi hawataki kukaa mezani kugawana ziwa nyasa wanadai kwa mujibu wa mipaka ya mkoloni ziwa ni mali yao, ni kweli lakini mbona walikubali kufanya marekebisho enzi za wakoloni Kati yao na msumbiji? Hii inaonesha haki haikutendeka ndiyo maana Hilo liliwezekana ila halikufanyika enzi za muingereza kwa sababu hakuona haja ya kufanya hivyo nchi zote mbili ziko chini yake. Sasa tukae mezani tugawane ziwa,Malawi hawataki wanasema tufuate mpaka wa wakoloni. Tukumbuke mgogoro huu upo tangu enzi za Nyerere na Kamuzu Banda
Mipaka ilikuwepo ila siyo katika hali ya sasa.Kumbuka Afrika tulikuwa hatuna mipaka kabla ya wazungu kuja kutugawanya
Nchi iliyogawanyika haijawahi kuwa na umojaJamani Watanzania tokeni kwenye mapenzi nchi inamegwa kimasihara 😢
Sio kirahisHuu ni mwanzo. Kama wazungu wamekubali kubadili huo mpaka kwa kumega nchi yetu huoni kuna siku tutapigwa marufuku kukanyaga ndani ya hilo ziwa?
Wewe Jamaa una mihemko ya aina fulani.Tukiendelea kunyamaza kuna siku watasema mkoa wa Mbeya ni wao
Period, tena mie nta volunteer, na ka cheti ka jkt, potelea mbali niwe chambo..Kama wanajiamini Ziwa lote ni lao waanze kufanya mishe mishe zao ziwa zima waone MOTO 🔥🔥