Wakuu leo mapema nimekutana na hii barua nimepata mashaka kama imetolewa kweli na BAVICHA tafadhali naomba msaada wa kujua uhalisia wa barua hiyo kwa umma.
Katika Uchunguzi uliotajwa na Jarida la MailOnline, unasema kuwa UBER wamekuwa na tuhuma hizo za kuchaji wateja bei kubwa kama simu zao ziko low Battery.
kwasababu wanajua unaharaka, na huna namna nyingine hivyo inakufanya kuwa mteja wa uhakika ambaye huwezi kukataa Bei utakayopewa.
Naomba JamiiCheck msaada wa kuchunguza hili.
Salaam Wakuu,
Nimekutana na stori mtaani zinadai kwamba mnamo mwaka 1990 Bondia Maarufu Muhamedi Ali alienda nchini Iraq kuzungumza na rais wa nchi hiyo wakati huo Sadam Hussein kuwaachia mateka wa Marekani na kufanikiwa.
Je, kuna ukweli wowote kuhusu sakata hili?
Tunaombeni ufafanuzi
Habari Wakuu,
Nimekutana na video hii TikTok inayodai hii pande kubwa la theluji lipo Mlima Kilimanjaro na lilikuja kutokana na mabadiliko ya Tabianchi. Kuna ukweli hapa?
Naombeni mtusaidie
---
Wakuu Salaam,
Nimekutana na na barua ambayo inasambaa mtandaoni ambayo inaonekana kama imeandikwa na Naibu wa Rais wa Kenya ikiwa na dhumuni la kujiudhulu, je kuna uhalisia wowote juu ya suala hili?
Nimekuwa nikisia mara nyingi kuwa kunguru akifa haozi, bali hukauka tu na kadiri siku zinavyozidi kwenda hupukutika mpaka kuisha ila huwezi kuta kaoza wala kutoa harufu.
Badhi ya watu huwa wanasema haozi kwa sababu hali chumvi japo sina hakika katika hili maana mara kibao amekula vyakula vyenye chumvi kama nyama na vyakula vingine hapa home.
Je kuna ukweli wowote katika hili? Kama ni kweli sababu ni nini?
Wakuu nimekutana na video inayosambaa kwa kasi sana mtandaoni ambapo wanaonekana John Mrema na John Mnyika, na Mrema akisikika kuwa atatoa maoni juu ya usafiri huo mara baada ya safari kukamilika lakini kinachonipa utata ni sauti inayosikika katika video hiyo baada ya Mrema ikisema viongozi hao wamesifia huduma za usafiri wa treni ya mwendokasi (SGR) na filamu ya royal tour wakati Mnyika na Mrema hawaonekani wakitoa maoni hayo, Je kuna ukweli wowote hapa?
Katika pita pita zangu mitandaoni leo nimekutana na "Twit" inayosema kwamba Gavana wa BOT Gilman Rutihinda (1989 - 1993) alifariki kutokana na ajali ya gari mwaka 1993 kama hii tweet inavyojieleza:
Hata hivyo kuna article ya Mwaka 2011 hapa katika Forum inayoelezea kifo cha Gavana Rutihinda pamoja na Waziri wa Fedha wa wakati huo Steven Kibona kwamba vilitokana na 'food poisoning' baada ya kurudi kutoka safarini India.
- Sababu ya kifo cha Steven Kibona na Gilman Rutihinda
Je tunaweza kupata ukweli wa vifo hivi?
Wakuu habari,
Leo katika pita pita zangu nikakutana na uvumi kuwa mtu akila Tango na Asali anaweza kufa.
Je kuna ukweli wowote juu ya hilo? Na kama kuna ukweli chanzo kitakuwa nini?
Wakuu,
Nimekutana na video huko duniani, kahawa hii wanapewa tembo wale na tembo hao wakijisaidia inaenda kusafishwa kisha kuuzwa, wanadai eti ikipita kwenye mwili wa tembo inapunguza ladha ya uchungu, yaani isiwe kali sana.
Hii ni kweli wataalamu?🥲
Video hii hapa👇
---
"Mama kuwa na umri zaidi ya miaka 35 au Baba kuwa na miaka zaidi ya 40 kunaweza kupelekea kupata mtoto mwenye mtindio wa ubongo, kupata infection wakati wa ujauzito, Mama mjamzito kuumia sababu zipo nyingi ambazo zinapeleka mtoto kuzaliwa na mtindio wa ubongo" Dkt. Alvin Miranda.
vijana wenye malengo ya kupata watoto, jitahidi uzae ukiwa under 35
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.