JamiiCheck - Tanzania

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Huyu ni mnyama mkali sana, mkorofi, na mwenye nguvu katika jamii ya paka. Akiingia bandani, anondoka na kuku mzima na anaenda kula kichwa mpaka shingoni. Kama ni kifaranga, anakula chote au akikuta mayai ambayo bado kidogo ya yaanguliwe, ndio soshi wake. Anakaa vichakani au porini, sehemu yenye msitu mkali. Akigundua kwamba yupo kwenye eneo lenye adui kama mbwa, chui, fisi au binadamu, anaachia ushuzi wake ambao unanukia kama wali au ubwabwa, kiasi kwamba utadhani mtu kaficha huo wali vichakani. Kumekuwa na dhana kwamba ukisikia harufu ya ubwabwa vichakani, ni chatu. Hapana, sio kweli; ni huyu mnyama anayeitwa kanu katika Kiswahili (kwa huku mtaani, sijui upande mwingine). Naendelea kutega; nikikamata nitawaletea mumjue. Huyu...
Chadema imewapiga marufuku maelfu ya watanzania ambao wana elimu ya msingi na kidato cha nne wasigombee uongozi wowote katila chama hicho katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu. Chama hicho, japo kimewanyima haki ya kugombea, kinatarajia kwenda kuwaomba kura ili kuwatumia kisiasa kwa faida yao Ni nadra sana kukutana na mjumbe wa serikali ya mtaa au kitongoji mwenye elimu ya kidato cha sita, achilia mbali mwenyekiti wa mtaa na wa kijiji. Sasa ni zamu ya watanzania hao kuwaadhibu chadema kwa dhambi hii ya ubaguzi
Tumefanikiwa kuipata picha hii ambayo inaaminika huyu ndio Gustave. Kuna Mamba katika Ziwa Tanganyika anayeitwa "Gustave" ambaye inadaiwa ameua zaidi ya watu 300 katika miongo kadhaa iliyopita. Kumekuwa na majaribio kadhaa ya kumuua au kumkamata bila mafanikio. Gustave ni mamba wa kiume yupo tangu mwaka 1955 ambaye huzurura katika fukwe ndani ya Ziwa Tanganyika. Inasemekana kuwa Gustave aliua watu 300, amepata hadhi ya kuzungumzwa na anaogopwa sana na watu. Uwezo wake ni mkubwa sana wa kukamata na nguvu zake hazieleziki. Urefu wake ni mita 6.1 ana uzito wa kilo 907 kwa mujibu wa tafiti zilizofanyika. Ana uwezo wa kukamata mnyama yeyote yule wa nchi kavu na majini ikiwemo Kiboko. tembo n.k. Wazungu wamelichukulia swala hili ni maajabu...
Tangu nikiwa mdogo nilisikia na kuamini kwamba ute/ mapovu yanayokuwa kwenye mimea ni mate ya nyoka. Mpaka kufika wakati huu bado sijajua kama suala hili lina ukweli ama la. Naomba wataalamu mnisaidie kujua uhalisia wa jambo hili Kielelezo 1: Picha ikionesha mmea umeachiwa mapovu Kielelezo 2: Picha ikionesha mdudu aina ya Spittlebugs anayetengeneza Povu kwenye mimea Video ikionesha namna wadudu aina ya Spittlebugs wanavyotengeneza povu
Nimesikia sehemu kuwa binadamu anaweza kupata usugu wa vimelea kutokana na kutumia mazao yatokanayo na wanyama mbalimbali, mfano wa mazao hayo ni nyama nk. Hofu yangu ni kuwa wafugaji wengi siku hizi wamekuwa si waaminifu kabisa, wamekuwa wakitumia madawa hatari kwa ajili ya kukuzia haraka wanyama ili waingize sokoni, au wakati mwingine wamekuwa wakitumia madawa kwa ajili ya kuhifadhi mazao hayo ili yakae muda mrefu bila kuharibika. Kumekuwepo cases nyingi za nguruwe na kuku kuchanganyiwa dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI. JamiiCheck.com naomba mniondoe wasiwasi huu maana tunakoelekea huko mbeleni ni hatari.
Back
Top Bottom