JamiiCheck - Tanzania

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Kando ya barabara ya Iringa - Mbeya maeneo ya Njia panda ya Mlolo kuna Kaburi la mtu aliyekuwa maarufu katika fani ya Uganga wa jadi mkoani Iringa na alifahamika kama Mzee Martin Kiyeyeu. Inaelezwa mzee huyu alifariki mwaka 1974 na kuzikwa lakini muonekano wa Kaburi hilo ni kama alizikwa hivi karibuni. Inaelezwa baada ya kufariki, Mganga huyo alizikwa kwa kufuata taratibu na mira za Machifu ambapo alizikwa kwa kusindikizwa na mtu aliye hai, aliyejitolea kuzikwa naye akiwa hai ili kumsindikiza, ambapo inadaiwa mtu huyo alikaa na kumpakata Mganga huyo aliyezikwa huku akiwa amekaa. Kaburi la Mganga Martin Kiyeyeu na nyanya za umeme zilizohamishwa upande Inadaiwa kumekuwa na maajabu mengi yanayotokana na Kaburi hili ila moja maarufu ni...
Katibu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Charles Kitima, ameisifu Katiba ya mwaka 1977 huku akitoa rai kwa vyama vya upinzani, hususan Chadema, kuheshimu na kushiriki kikamilifu kwenye chaguzi kwa mujibu wa Katiba iliyopo. Padri Kitima alieleza kuwa, licha ya kuwepo mijadala kuhusu katiba mpya, Katiba ya sasa bado ina uwezo wa kuhakikisha uwazi na ushiriki wa kila mtu katika siasa. “Katiba hii imerekebishwa mara kadhaa na bado inatosha kutuongoza kushiriki siasa kwa ufanisi. Muhimu ni kuielewa na kuzingatia ili kuimarisha demokrasia yetu,” alisema. Aidha, alisisitiza kuwa msingi wa Katiba hiyo uliwekwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. “Hii ni Katiba nzuri iliyoundwa na Nyerere, mtu wa Mungu. Msisitizo...
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimeibua mkanganyiko mkubwa kwa wanachama na wananchi baada ya kubadili msimamo wake kuhusu kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.Awali, chama kilieleza nia ya kushiriki uchaguzi lakini Freeman Mbowe alinukuliwa akisema hawatashiriki. Baadaye, chama kilikanusha kauli hiyo kikisisitiza hakijajitoa. Kwa mshangao mkubwa, Oktoba 27, Chadema kimetoa taarifa rasmi ya kutoshiriki uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Novemba 27.Akitoa tamko hilo, Suzan Limo Spika wa kinachoitwa Bunge la Chadema alisema: "Leo tumewaita kwa hoja mahususi kuhusu mchakato wa kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa... Chadema imejiondoa rasmi kutoka uchaguzi wa vitongoji, vijiji na mitaa." Hatua hii imeshtua wengi hasa...
Nakumbuka shule niliyosoma tulikuwa tunawekewa mafuta ya taa kwenye chakula, Katika kudadisi kwa nini watuwekee mafuta hayo niliambiwa kuwa wanatuwekea ili kutufanya tusiwe na hamu au kupunguza hamu ya kufanya mapenzi ukizingatia wanafunzi wanakuwa wameanza au walishapevuka tayari. JamiiCheck naomba mnijibu, je ni kweli yanapunguza hamu ya kufanya mapenzi au walikuwa wanatulisha bure tu?
Na Mwita Mwija Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika ameeleza kuwa kutokana na uhaba wa fedha, kwa sasa wagombea wote ngazo za mitaa, vijiji na vitongoji lazima wachangie kukiwezesha chama shilingi Laki nne (400,000) hii itasaidia uwezeshaji katika usimamizi wa chaguzi hizo kwa kuweka mawakala wa kusimamia zoezi hilo. "Pia chama bado tunaendelea kutafuta wafadhiri wa kutufadhiri katika chaguzi hizi ili tuwe na nguvu kubwa na vigezi vyote watakavyo vitoa ili kutupa msaada huo wa kifedha tutavitimiza na hadi sasa tumemtuma Mhe. Tundu Lissu huko huko duni (nje ya nchi ) azungukie wadau na kutafuta fedha kwa masharti yeyote yale watakao yatoa tupo tiyari kuyatimiza na hadi sasa yuko mbioni kufanikisha hilo," amesema Katibu Mkuu CHADEMA...
Back
Top Bottom