JamiiCheck - Tanzania

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Licha ya kuwa Mazoezi husaidia kujenga na kulinda Afya, kuna masuala muhimu ya kuzingatia kabla ya kuanza mazoezi ikiwemo kuchagua eneo la kufanyia mazoezi ambalo litakuwa salama kimiundombinu na kimazingira. Katika siku za hivi karibuni watu wengi wamekuwa na utaratibu wa kufanya mazoezi katika maeneo ya jirani au pembezoni mwa Barabara zinazotumiwa na Vyombo vya Moto (Magari, Pikipiki Bajaj na Mitambo mbalimbali) hali inayodaiwa kuwa watu hao huvuta hewa chafu. Je kuna ukweli wowote hapo?
Hivi karibuni kumekuwa na taarifa zinazohusisha taasisi na watu maarufu duniani kuwa na mpango wa kupunguza idadi ya watu duniani. Miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na Bill Gates kuelezwa kuandika katika mitandao wa kijamii akimshauri kiongozi wa World Economic Forums (WEF), Klaus Schwab juu ya matumizi ya "death panels" kupunguza watu duniani. Lakini pia, video nyingine ambayo imesambaa mtandaoni inamuonesha Mtendaji Mkuu wa Pfizer, Albert Bourla, akidaiwa kusema wanatazamia kufanikisha kupunguza idadi ya watu duniani kwa 50%. Je, taarifa hizi zina ukweli?
Hoja ya Serikali ya Tanzania kufanya Makubaliano ya awali na kampuni ya DP World ya Dubai kwenye kuendeleza bandari ya Dar Es Salaam imezua mambo mengi yanayojadiliwa sana. Mojawapo ya Mambo hayo ni kuhusisha Bandari kuwa miongoni mwa masuala ya Muungano. Baadhi ya watu wamekuwa wanadai kuwa Bandari ni Suala la Muungano huku wengine wakipinga. Ukweli upoje?
Rais Mstaafu Joseph Kabila inasemekana hakuwa mtoto halisi(Biological Son) wa Rais Mstaafu Joseph Desire Kabila. Inasemekana jina halisi la Joseph Kabila ni Hypolite Kanambe Kazemberembe akiwa na asili ya Kitusi kutoka nchi ya Rwanda. Pamoja na machapisho mengi kumtambua Joseph Kabila kama mtoto halisi (Biological son) wa Hayati Joseph Desire Kabila, baadhi ya machapisho yamehabarisha kuwa baba mzazi wa Joseph Kabila Kabange anajulikana kama Christopher Kanambe Kazemberembe na mama yake akiitwa Marcellina Mukambukuje. Maswali ambayo wakongo wengi wanajiuliza, ilikuwaje wakatawaliwa na Rais aliyezaliwa Rwanda na mwenye asili ya Kitusi kutoka Rwanda huku Moise Katumbi aliyezaliwa Congo DR na Mama Mkongo na Baba Mgiriki akiwekewa...
Wiki mbili zilizopita kwenye mitandao mbalimbali ilionekana mwendesha bodaboda asiye na woga akiwaacha wengi katika mshangao baada ya kupita kwa utulivu katikati ya kundi simba wenye njaa wanaokula mnyama waliyemuua. Inasemekana baada ya kuwapita Simba, pikipiki yake ilipata hitilafu ambapo alishindwa kuendelea na safari ndipo Simba waliweza kumshambulia na kujipatia kitoweo. Picha ya mwisho iliyobandikwa ilionyesha simba wakiwa wamekaa pembeni ya pikipiki hiyo iliyokuwa imebeba na ndizi, lakini mtu huyo hakupatikana, jambo ambalo liliwashangaza wengi na kuamini kuwa ameliwa na simba hao. VIDEO: Simba wakizunguka pikipiki huku dereva akiwa haonekani. Katika Mtandao wa Twitter, mtumiaji mmoja maarufu kama Mwaisa MtuMbad...
Jamani kichwa kinajieleza. Kwanza ni kweli mende anazalisha maziwa? Mende hawa hawa tunaowaona chooni? Sasa maziwa yenye yanakaa wapi na wanakamuaje? Halafu eti inasemekana maziwa ya mende yanavirutubisho kuliko ya ng'ombe, si makubwa haya! Mende walivyo wachafu na wanavyoogopesha leo mtu ukanywe sijui ule maziwa yake, yaani sitaki hata kupata picha kwakweli. Wakuu hili ni kweli?
Kuna wakati jengo la Burj Khalifa lilisambaa mtandaoni likiwa na bendera ya Tanzania na Picha ya Rais, lakini kwa siku za hivi karibuni nimeona tena mitandaoni kuna picha za bendera za majirani zetu zikiwa kwenye jengo hilohilo. Mjadala wa bendera za nchi za Afrika mashariki kuwekwa kwenye jengo la Burj Khalifa umeshika kasi zaidi mitandaoni leo 14/07/2023 baada ya Rais Samia kudokeza kuwa ipo nchi jirani bendera yake imewekwa pale baada ya kuwapo kwa malumbano ya mkataba wa bandari nchini. Ukweli wa jambo hili upi? Je, picha za majirani zetu ziliwekwa baada ya Tanzania kuwekwa?
Wajumbe, Hili dude la mkataba wa DP World na Serikali ya Tanzania ina makando-kando mengi. Katika kufukunyua nimekutana na wavaa miwani mieusi tena ni PSU. Huyu Bwana amenidokeza kwamba katika uwekezaji huu Rwanda ya Paul Kagame anayo hisa 17% katika kampuni ya DP World na ndiye amekuwa na ushawishi mkubwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan. Katika ziara ya Kagame siku za karibuni ilikuwa ni kukamilisha dili lenyewe. Ikumbukwe Kagame amekuwa na hamu ya kumiliki Bandari ya Dar es salaam kwa miaka mingi akiamini kwamba "tumeshindwa kutumia Bandari ya Dar es salaam kutuletea faida". Hata hivyo, mtoa habari huyo amedai hatua hiyo haijamfurahisha Jakaya Kikwete na ndiye yuko nyuma ya wapinzani wa mkataba huu wa kifedhuli. Paul Kagame, Rais...
Julai 12, 2023, Balozi mstaafu wa Tanzania Nchini Sweden, Dkt. Wilbroad Slaa akiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari alitoa kauli inayotuhumu waandishi wa habari kwa kufanya upotoshaji wa matamshi yake kwenye sakata la uwekezaji wa Bandari. Baada ya kauli hii, wadau mbalimbali walianza kutoa maoni yao ambapo jioni ya siku hiyo ilianza kusambaa barua inayodaiwa kutolewa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) ikionesha masikitiko na kulaani kauli za Dkt. Slaa. Barua hiyo ilienda mbali zaidi kwa kumtaka Dkt. Slaa kumba radhi kwa matamshi yake.
Wakuu, Nimekutana na ujumbe unasambaa kwenye mitandao ya kijamii Twitter, Instagram na hata humu JF nimeona mtu kaweka uzi kuwa wanafunzi tena wakike kutoka shule ya wasichana ya Lucas Malia walifungiwa mlango na hivyo kulazimika kulala nje sababu eti walichelewa kufika siku waliyotakiwa kuripoti shuleni. Tukio hilo limetokea Julai 9 na mpaka sasa hawajapolewa wako wanaranda tu mtaani. Wakuu taarifa hii ni ya kweli?
Mdau wa JamiiForums ameweka Chapisho lenye kichwa cha habari "CCM kimeanza kuumana" akimaanisha kuwa hali imeanza kubadilika kwenye Chama cha Mapinduzi baada ya Serikali inayoongozwa na Chama hicho kusaini Mkataba na kampuni ya DP World kuhusu uwekezaji kwenye Bandari ya Dar es Salaam. Hali hii imesababisha kuvunjwa kwa mojawapo ya Ofisi za Chama hicho iliyopo Kinondoni. Ukweli wa suala hili upoje?
Nimekuwa nikisikia kutoka kwa watu mbalimbali kuwa pindi hutumiapo dawa zozote basi itakupaswa usitumie maziwa aina yoyote kwasababu matumizi ya maziwa hupunguza au kuondoa kabisa ufanisi wa dawa hizo hivyo kupelekea kutotibu ugonjwa uliokusudiwa. Kwa uelewa wangu ni dawa mbili tu ambazo hushauriwi kutumia maziwa pindi ukiwa unazitumia ambazo ni Tetracycline Antacids Je, upi ukweli kuhusu jambo hili? Nawasilisha.
Kijana mmoja aliejulikana kwa jina la Israel Daudi, amefariki dunia baada ya kupigwa risasi 3 na askari Polisi kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kuachia ng'ombe kuingia shambani. Tukio hilo limetokea katika Mtaa wa Olaresho, Kata ya Olasiti katika Halmashauri ya Jiji la Arusha. Akizungumzia tukio hilo Diwani wa Kata ya Olasiti, Alex Martin amesema hilo ni tukio la pili kwa askari huyo kufanya mauaji katika Kata hiyo ya Olasiti kwani huko nyuma alishafanya mauaji na Wananchi walitaka kumuua askari huyo lakini diwani aliingilia kati kwa kumuepusha askari huyo kuuliwa na Wananchi. Lakini cha kushangaza askari huyo amerudia tena kufanya mauaji katika kata hiyohiyo. Diwani Alex ametoa wito kwa Jeshi la Polisi kutotumia nguvu na mabavu kwa...
Back
Top Bottom