JamiiCheck - Tanzania

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Nianze kwa ku-declare interest kuwa mimi ni mzaliwa wa Mkoa wa Kagera Wilaya ya Missenyi. Katika makuzi yangu hasa baada ya kutoka nje ya mipaka ya mkoa wa Kagera, nimekuwa nikishambuliwa na kutaniwa sana kuhusu UKIMWI kuanzia mkoa wa Kagera. Hayati Rais Magufuli kwa nyakati tofauti amewahi kunukuliwa akiusema mkoa huko kwamba kila janga baya huanzia mkoa huo. Rais Magufuli awashangaa Kagera kila jambo baya kuanzia mkoa huo Pia watu mbalimbali katika mitandao ya kijamii wamekuwa wakiuponda mkoa huo kuhusu kuwa chanzo cha kuleta UKIMWI Tanzania. Je, ukweli ni upi kuhusu historia ya UKIMWI nchini?
Wakuu mko vyede? Kuna kipindi fulani hili suala lilizuka sana kuwa wanaoishi na HIV hasa matajiri walikuwa wanaenda South Afrika kubadilisha damu ili kupunguza makali ya ugonjwa huo. Hii ilikuwa kweli? Maana mpaka leo naamini walikuwa wanafanya hivyo, ila swali likaja wanabadilishaje? Wanamtoa damu nusu halafu wanamuongezea nyingine ambayo haina virusi ama? Msaada wenu kung'amua hili wajuvi.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza anuai mpya ya COVID-19 iitwayo EG.5 - iliyopewa jina lisilo rasmi "Eris" huku likishauri kila nchi kuchukua hatua mahsusi za kufuatilia uwepo wake. Lakini shirika hilo linasema inaleta hatari ndogo kwa afya ya umma, bila ushahidi kwamba husababisha ugonjwa mbaya zaidi kuliko lahaja zingine zinazozunguka kwa sasa.
Kizza Besigye na Yoweri Museveni walikuwa marafiki walioshibana wakati wa Vita ya Msituni Uganda kumuondoa Milton Obote miaka ya 1980, na Dkt. Besigye aliwahi kuwa daktari binafsi wa Museveni na wanajeshi wengine waliokuwa msituni pamoja na Museveni Rais Museveni na Winnie Byanyima walikuwa wachumba kati ya 1981 na 1986, Bi Byanyima alikuwa pamoja na Museveni alipoingia Kampala akiwa mkuu wa jeshi la waasi mwaka 1986. Lakini Museveni hakuwa tayari kumuacha mkewe, Janet, na Bi Byanyima akafukuzwa. Hatimaye aliolewa na Dkt. Besigye 1998. Inadaiwa kitendo kile kilimuuma sana Rais Museveni, kwanza akataifisha ranchi ya babake Winnie Byanyima, Mzee Boniface Byanyima. Pia matukio hayo ya ngono na usaliti yalijenga uadui mkubwa kati ya...
Kuna maeneo fulani nimepita ya mkoa wa dodoma wilayani huko; nimekuta kuna msururu mrefu sana wa vyombo vya moto kwenye moja ya petrol station. Nikajaribu kuuliza kuna shida gani hapa? Wenyeji wanasema mafuta ya petrol hamna kabisa wilayani hapo. Baadhi ya vituo vya mafuta vimesitisha huduma. Pia majuzi nilisikia kuna sehemu hapa tz pia kuna shida ya mafuta.
Habari ndio hiyo wakuu, Mpaka Tanganyika inapata uhuru wake mwaka 1961, ni wananchi wawili tu walikuwa wamesoma kwa kiwango cha shahada ya kwanza(Degree). Wa kwanza alikuwa ni Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye alikuwa ni Rais wa kwanza na baba wa Taifa. Mwalimu Nyerere alikuwa na Degree ya Uchumi, akachanganya sheria na mambo mengine. Mtu wa pili alikuwa mzee mmoja wa Kisambaa, jina limenitoka. Huyu mzee alikuwa na shahada ya kwanza ya Uhandisi(engineering). Asante sana
Miongoni mwa Wabunge wa Tanzania waliobahatika kuteuliwa kufanya ziara ya siri huko Dubai, yumo mbunge wa Jimbo la Msalala la Mkoani Shinyanga. Taarifa zinaonesha kwamba Mbunge huyu alivyorudi tu yeye hakutaka kununua gari la kuandika jina lake kama alivyofanya Musukuma, bali yeye ameamua kugawa nyama ya ng'ombe kila kijiji, ambako kijiji kimoja kimeambulia ng'ombe kubwa mbili. Ikumbukwe kwamba Jimbo la Msalala lina kata 18, ambapo kila kata ina vijiji 6, unadhani wabunge walioenda kule walilipwa bei gani kila mmoja na kwanini walipwe vitita vyote hivyo? Toa Maoni yako.
Back
Top Bottom