Kizza Besigye na Yoweri Museveni walikuwa marafiki walioshibana wakati wa Vita ya Msituni Uganda kumuondoa Milton Obote miaka ya 1980, na Dkt. Besigye aliwahi kuwa daktari binafsi wa Museveni na wanajeshi wengine waliokuwa msituni pamoja na Museveni
Rais Museveni na Winnie Byanyima walikuwa wachumba kati ya 1981 na 1986, Bi Byanyima alikuwa pamoja na Museveni alipoingia Kampala akiwa mkuu wa jeshi la waasi mwaka 1986. Lakini Museveni hakuwa tayari kumuacha mkewe, Janet, na Bi Byanyima akafukuzwa. Hatimaye aliolewa na Dkt. Besigye 1998.
Inadaiwa kitendo kile kilimuuma sana Rais Museveni, kwanza akataifisha ranchi ya babake Winnie Byanyima, Mzee Boniface Byanyima.
Pia matukio hayo ya ngono na usaliti yalijenga uadui mkubwa kati ya...