Mtumiaji wa Mtandao wa TikTok anayetumia jina la Leonard Clasic (User4692412178624), Julai 3, 2023 mchana, aliweka video moja kwenye ukurasa wake pasipo kufafanua chochote.
Video hiyo inamuonesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akikemea baadhi ya watendaji wa Serikali wanaoingia mikataba mibovu na kusababisha hasara kubwa kwa taifa.
Video hii inahusianishwa na Sakata la uwekezaji wa Bandari unaotarajiwa kufanywa na Kampuni ya DP World ya Dubai, imeendelea kusambaa sehemu mbalimbali huku baadhi ya watu wakimpongeza Rais Samia kwa kutoa kauli hiyo.