Kuna tafiti za hivi karibuni zimethibitisha kwamba hata wanaume hupata hedhi, ingawa wanaume hawana alama za nje za kuwaonesha kwamba wako kwenye hedhi, kama walivyo wanawake ambao hutoka damu siku zao za hedhi zinapofika na kukamilika.
Dalili za mwanaume aliye kwenye hedhi ziko akilini zaidi, mwanamke asili yake ni kimwili zaidi, kihisia zaidi. Lakini mwanaume anapata usumbufu ule ule anaopata mwanamke anapokuwa kwenye hedhi.
Tofauti ni moja tu, kwamba mwanaume hatoki damu. Lakini kila mwezi, baada ya siku 28, hali fulani ya kiakili na kihisia itakuwa inajirudia.