JamiiCheck - Tanzania

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Taarifa potofu ni habari ambayo si sahihi. Taarifa potofu inaweza kuwa na athari hasi au kuwachanganya watu kutokana na ukosefu wa usahihi au udanganyifu. Athari za taarifa potofu yanaweza kuwa makubwa au vinginevyo kulingana na unyeti wa taarifa iliyosambazwa ikiwa haina usahihi. Kadiri inavyozidi kusambaa na kuchukua muda mrefu bila kukanushwa au kutolewa ufafanuzi wa upi usahihi wake ndivyo huweza kuathiri kundi kubwa zaidi na kuleta madhara zaidi. Pamoja na hatari iliyopo juu ya usambazaji wa taarifa potofu bado jamii hailichukulii kwa uzito suala la kufanya uhakiki wa taarifa unozopokea wala kusambaza wala kutilia mkazo elimu ya ya kutambua ubaya wa taarifa potofu, lindi la kusambaa kwa taarifa potofu kupitia mitandao ya kijamii...
Upotoshaji kwa kutumia jina ni kitendo cha kutumia jina la mtu, kundi, taasisi au kampuni ambayo si wewe na kulifanya kama lako. Upotoshaji wa jina mara nyingi huwalenga watu, kampuni au taasisi maarufu ili lengo la mpotoshaji litimie kwa urahisi. Upotoshaji wa jina umekithiri sana katika mitandao ya mbalimbali ya kijamii ambapo ukimtafuta mtu fulani maarufu utaona jina lake linatumiwa na watu wengi. Sababu za upotoshaji wa jina Upotoshaji wa jina huweza kuwa kwa sababu mbalimbali miongoni mwa hizo ni: Kujinufaisha au kuingiza kipato - Huu ni upotoshaji wa jina unaohusu zaidi matumizi ya jina la biashara au Kampuni ya kutoa huduma fulani. Mpotoshaji wa jina anatumia jina la Kampuni fulani kama lake Ili aweze kupata wateja wanaopenda...
Wataalamu wa afya huelezea umuhimu na faida za kufanyika kwa tendo hili kwa wanaume. Baadhi ya sehemu wanaume huwa hawatahiriwi kabisa, na wengine wanaotahiri husubiri hadi mtoto afikishe walau miaka 12 ndipo afanyiwe tendo hilo kwa uoga wa kupunguza ukubwa wa viungo hivyo. Madai haya yamekuwepo kwa muda mrefu, na majibu sahihi bado hayajatewa. Ni kweli kuwa tohara hupunguza ukubwa wa via vya uzazi vya mwanamme?
Vichwa vya habari vinaweza kuwa sehemu muhimu katika kusambaza habari potofu kwa sababu vinaweza kuvutia umakini wa wasomaji, kuchochea hisia, na hata kutoa taswira isiyo sahihi ya habari kamili. Katika dunia ya sasa ambayo teknolojia ya habari imekua kwa kiasi kikubwa, baadhi ya watu wanaweza kutumia uandishi wa vichwa vya habari kama njia ya kuhadaa umma ili kufikisha ujumbe wanaokusudia. Hapa kuna njia kadhaa ambazo vichwa vya habari vinaweza kuchangia katika kusambaza habari potofu: 1. Kuchagua Maneno yanayovuta Upande Mmoja: Vichwa vinavyoleta hisia ya upendeleo au kuunga mkono upande fulani wa habari vinaweza kusababisha upotoshaji wa mtazamo wa habari. Mfano: Wakristu (au waislam) wanyayasika huko XYZ Jinsi inavyopotosha...
Uhakiki wa Taarifa hudumisha uwazi, kujenga imani kwa jamii, kukomesha upotoshaji pia kuwepo kwa taarifa sahihi katika jamii itaifanya jamii iweze kufanya maamuzi sahihi kwenye jambo sahihi. Kuchochea uwajibikaji- Uhakiki wa taarifa utachochea makundi mengi kuwajibika kwani watakosa fursa ya kusambaza taarifa potofu kwa manufaa yao. Mfano, wanasiasa husambaza taarifa au kutoa ahadi nyingi za kweli na za uongo ili kuwaaminisha watu wao ni sahihi kuchukua wadhfa wanaokuwa wanagombea na baada ya kupata nyadhfa huendelea kusambaza taarifa ili aidha kuwapumbaza wananchi juu ya mabaya yao au kupalilia nafasi zao. Kwa kuhakiki taarifa jamii itaweza kuwawajibisha pale watakapokuwa wanaweza kubaini kuwa taarifa fulani si kweli au kweli...
Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia kumeibuka Application nyingi za kutengeneza picha, ambazo zinaweka kubadili muonekano wa picha kwa namna nyingi na hata kuleta sintofahamu baadaye Upotoshaji katika picha ni kitendo Cha kuhariri (edit) picha kwa kuongeza kitu, kupunguza kitu kuwaaminisha watu kuhusu jambo fulani kutokana na muonekano mpya ulioutengeneza katika picha hiyo. Upotoshaji wa picha huweza kufanywa kwa namna mbalimbali, zifuatazo ni namna chache kati ya nyingi: 1. Kuhariri au kutengeneza Huu ni upotoshaji katika picha ambapo mpotoshaji hutumia utaalamu kuhariri au kutengeneza picha fulani kwa lengo la kuitoa uhalisia wake na kuifanya iwe kwa namna inayoendana na lengo lake. Picha huweza kuhaririwa kwa kubadili...
Beki wa Simba Che Malome,siku ya tarehe 05.11.2023 wakati wanakandwa kichapo cha mbwa mwizi kutoka kwaa watani zao Yanga, alionyeshwa kadi mbili za manjano. Kitu ambacho kilipaswa kupewa card nyekundu, lakini refa na wasaidizi wake hawakuliona hili sijui hawakuwa na kumbukumbu vizuri, Che Malome hakutoka nje kwa adhabu ile, alicheza tu. Juzi kati, kati ya Mechi ya Simba na Namungo,Che Malome alicheza tena, Simba walimchezesha mchezaji mwenye card nyekundu kwa sababu zipi? Bodi ya Ligi mko wapi? TFF mko wapi? Wapeni Namungo ushindi wa point tatu na magoli mawili kama kanuni inavyotamka.
Baada ya kukutana na taarifa yoyote unayoitilia shaka, kuna hatua kadhaa unaweza kuchukua ili kujiridhisha uhalali wa taarifa hiyo. Kuchukua hatua za haraka na kutoa habari sahihi ni muhimu ili kuzuia kuenea kwa habari feki au gushi. Hizi ni baadhi ya hatua za kuchukua unapokutana na taarifa au habari unayohisi ni gushi au feki: 1. Usieneze Taarifa hiyo mpaka upate uhakika: Usiisambaze au kueneza taarifa hiyo kwa wengine kabla ya kuithibitisha kuwa ni taarifa sahihi ili kuzuia kusambaa kwa taarifa feki. Kusambaza taarifa/ habari unayoitilia shaka kunaweza kuchangia kusambaa kwa habari potofu 2. Tafuta Ukurasa wa Kukosoa au kuhakiki taarifa/habari: Kuna mashirika na tovuti zinazochambua na kukosoa habari feki, moja ya kurasa hizo ni...
Huu Muungano ni chenga kabisa una kero nyingi mno, naona kwa Zanzibar wao ni raha kwenda mbele. Sisi wote ni Watanzania lakini ajabu Mtanganyika akienda Zanzibar endapo atahitaji kuendesha gari basi atatakiwa kuomba kibali maalum kinachotolewa na mamlaka za huko, vinginevyo utakuwa unavunja sheria. Hili suala halijakaa sawa kabisa, sawa na lile la kulipia kodi electronics kutoka Zanzibar, au Mzanzibar kumiliki ardhi Bara wakati Mtanganyika anawekewa vikwazo mfululu kumiliki ardhi Zanzibar. Huu Muungano ni wa kishenzi sana.
Habari Potofu ni Taarifa au Maelezo yaliyobuniwa kwa kuiga mtindo fulani ili zionekane zina ukweli au halisi. Taarifa hizi hulenga kuleta Athari fulani, kuzua Taharuki au kudanganya Umma. Unaweza kubaini taarifa potofu kwa kufuata hatua hizi: Tathmini (thaminisha) chanzo Hakikisha kwamba chanzo cha habari ni halali na kinachoaminika. Unaweza kutumia vyanzo vya habari rasmi, kama vile vyombo vya habari vya kuaminika, magazeti, na tovuti za habari zenye sifa nzuri. Epuka kuchukulia kwa uzito habari kutoka kwenye vyanzo visivyojulikana au vyenye sifa ya kuzusha mambo mara kwa mara. Kagua vyanzo vingine Tafuta habari hiyo kwenye vyanzo vingine vyenye sifa nzuri ili kuona ikiwa habari hiyo inathibitishwa na vyanzo vingine. Tathmini lugha...
Usambazaji wa taarifa potofu umekuwepo kwa muda mrefu katika historia ya binadamu. Hata kabla ya teknolojia ya kisasa na mitandao ya kijamii, watu wamekuwa wakisambaza taarifa za uongo au potofu kwa njia tofauti, kama vile kupitia vyombo vya habari, mdomo, au vyanzo vingine vya habari. Hata hivyo, katika nyakati za hivi karibuni, hasa na baada ya kuongezeka kwa matumizi ya mtandao na mitandao ya kijamii, usambazaji wa taarifa potofu umezidi kuwa suala kubwa duniani. Ulianza kuwa suala kubwa zaidi katika miaka ya hivi karibuni, na linaweza kuwa na athari kubwa kwa jamii, siasa, na masuala mengine. Kampeni za kueneza taarifa potofu zinaweza kuwa za kimkakati na kutumika kwa madhumuni mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kujenga hisia za chuki...
Tulianza na shopping mall Dodoma, sasa tena ni kiwanda cha Tumbaku. Yasemekama wahusika ni wale wale! Ukiingia mjini Morogoro, umbali kidogo kutoka mzunguko wa Msamvu kuelekea Iringa, unakutana na daraja la reli na pembeni yake unakuta shughuli za ujenzi wa kiwanda kipya cha Tumbaku. Eneo hili kwa miaka mingi lilieleweka ni eneo la wazi, na kwa sheria zetu za ardhi, hakuna aliye na madaraka ya kubadili matumizi ya eneo la wazi.
Wakati napitia pitia mitandaoni kutafuta style mpya kwa ajili ya shangazi yenu ndio nikakutana na hili bandiko kuwa aina ya kujamiiana huku mwanamke akiwa amemkalia mwanaume juu ('woman on top' or 'cowgirl' or 'reverse cowgirl'), hatari kwa afya ya mwanaume kwani hupelekea maumivu makali kwani hupekelea fracture ya uume kwa asilimia kubwa wakati wa kushiriki tendo la ndoa. Inashauriwa mwanaume ndio akae juu ili kupunguza uwezekano wa kupata madhara.
Licha ya kufanya makubwa kwa muda mfupi ndani ya Mhula wa Kwanza, Rais wa Zambia Hakainde Hichilema ametangaza hataomba muhula wa pili kwenye uchaguzi mkuu wa baadae 2026. Hapa Tanzania hakuna chochote kafanya na bado chawa wanataka aongeze muda mpka 2030! Tamaa na Uroho wa Madaraka. Tazama video hii ujionee mwenyewe. Video ya Rais Hakainde Hichilema akisema hatagombea tena mwaka 2026.
Back
Top Bottom