JamiiCheck - Tanzania

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Habari potofu au habari za kupotosha zimekuwepo kwa muda mrefu kabla ya kuibuka kwa mitandao ya kijamii. Hata kabla ya enzi za teknolojia ya digitali, watu walikuwa wakitumia njia mbalimbali kusambaza habari potofu kwa lengo la kufikia malengo yao, iwe ni kisiasa, kiuchumi, au kijamii. Hapo awali, habari potofu ilisambazwa kupitia njia kama vile magazeti, redio, televisheni, na mdomo kwa njia ya mikutano au mazungumzo ya kijamii. Hata vyombo vya habari vya zamani vilikuwa na uwezo wa kuathiri mawazo ya umma kwa kuchapisha habari zilizopotoshwa au za kupendelea upande fulani. Hata hivyo, mabadiliko ya kiteknolojia, hususan kuibuka kwa internet na mitandao ya kijamii, yameongeza kasi na ufanisi wa usambazaji wa habari potofu. Ugunduzi...
MADAI Mdau wa JamiiForums ametoa mkasa mmoja unaomhusisha mume wa rafiki yake wa kike aliyeanza kuonesha dalili za ujauzito kwenye ujauzito mchanga wa mkewe. Mdau anaeleza kwamba shemeji yake huyu ilikuwa kila asubuhi anatapika njano, na homa za hapa na pale na kila alipoenda hospital Ugonjwa haukuonekana, ilifikia wakati mwanamme akawa hawezi kufanya shughuli zake kwa sababu ya kutapika sana. Baada ya kupima ilikuja kugundulika kuwa mkewe alikuwa na ujauzito. Ikasemekena kwamba kuna nyakati fulani ujauzito anabeba mwanamke Ila mabadiliko na dalili za ujauzito anakuwa nazo mwanaume. Jambo hili ni kweli au uzushi?
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres wakati akizindua ripoti maalumu iliyoundwa ili kuimarisha uadilifu wa habari kwenye majukwaa ya kidijitali. Kengele ya hatari kuhusu tishio linaloweza kusababishwa na maendeleo yanayokuwa kwa kasi ya Akili Bandia (AI) haipaswi kuficha uharibifu ambao tayari unafanywa na teknolojia za kidijitali zinazowezesha kuenea kwa matamshi ya chuki mtandaoni, pamoja na taarifa potofu na za uongo, alisema. Muhtasari wa sera ya uadilifu wa habari unasema kunapaswa kuwa na wahusika muhimu katika kuhakikisha usahihi unadumishwa, uthabiti na uaminifu wa taarifa zinazosambazwa na watumiaji. “Ni matumaini yangu kwamba (sera hii) itatoa kiwango cha dhahabu kwa ajili ya kuongoza hatua ili kuimarisha...
Salaam Wakuu, Kupitia WhatsApp yangu nimetumiwa ujumbe wa tahadhari kuhusu kuwepo kwa Mvua katika mikoa mbalimbali nchini Tanzania. Ujumbe huo unaeleza: Shinyanga, Dar, Pwani, Mafia,Tanga, Mwanza, Geita, Mara, Simiyu, Kigoma na Kagera tujiandae, kutakuwepo na Pacific El nino na Atlantic El nino, mvua zitakuwa kubwa na hatari sana, Mungu atunusuru. Hali ya hewa tayari imebadilika kuanzia juzi, upepo umeanza katika bahari za Atlantic, Pacific na Hindi, Wavuvi wameanza kuzuiwa kwenda kuvua na Meli za tafiti zimeanza kukumbana na dhoruba kali sana Baharini, picha za satellite sio nzuri kabisa. Tunatarajia magonjwa ya Kuharisha, Dengue, Malaria na Homa kuongezeka, tuchukue tahadhari mapema. Tuangalie nyumba zetu kama zinavuja...
Utengenezaji wa taarifa potofu unapingwa katika nchi mbalimbali. Baadhi ya watu katika jamii nyingi wamejikuta matatizoni kwa kuingia vifungoni au kulazimika kulipa fidia kwa sababu ya kutoa taarifa potofu kuhusu watu, kampuni na taasisi mbalimbali. Tanzania, kama nchi nyingine, ina sheria zinazodhibiti uzalishaji na usambazaji wa habari feki au za uongo. Sheria zinaweza kutofautiana kidogo kulingana na nchi, lakini lengo ni kudhibiti habari ambazo zinaweza kuleta madhara kijamii, kisiasa, au kisheria. Kwa mfano, Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 kifungu cha 16 nchini Tanzania inadhibiti matumizi mabaya ya teknolojia ya habari na mawasiliano. Sheria hii inaweza kutumika kufuatilia na kuchukua hatua dhidi ya watu wanaotengeneza...
Akiwa anatoa hija yake kuhusu athari za habari potofu Mwandishi w Urusi Julia Loffe anaeleza: Habari Potofu inaweza kugeuza Maoni ya Umma na kusababisha uungwaji mkono wa Sera na Viongozi wa Kisiasa wasiofaa. --- Habari Potofu huathiri Michakato ya kupata Viongozi wa Kisiasa, hushusha Imani ya Wananchi kwenye Mifumo ya Kidemokrasia pamoja na kusababisha kuchaguliwa kwa Viongozi wasiofaa au wenye uwezo Mdogo. Hivyo kutokana na hoja ya Mwandishi huyu ni Muhimu kupata Habari kutoka Vyanzo vya Kuaminika pamoja na kuzithibitisha kabla ya Kuziamini au Kuzisambaza ili kuepuka athari hizi ambazo huchochea Mgawanyiko kwenye Jamii na Kurudisha nyuma Mshikamano wa Kitaifa.
Usambazaji wa taarifa potofu umekuwapo muda mrefu sana, usambazi wa taarifa potofu umekuwa ukifanywa kupitia njia mbalimbali kama; Mitandao ya Kijamii Mitandao ya kijamii imekuwa ni njia ya haraka na inayoweza kufikia watu wengi zaidi ndani ya muda mfupi, hii imekuwa ni moja kuu ya kusambaza habari. Kupitia njia hii watu waovu wamekuwa wakiitumia kusambaza habari potofu kwa manufaa yao. Wamekuwa wakitumia majukwaa kama Facebook, Twitter, WhatsApp, na Instagram kusambaza habari za uwongo au uzushi. Barua pepe na Ujumbe Njia hii imekuwa ikitumiwa kwa muda mrefu kusambaza jumbe za uongo, mara nyingi imetumiwa a matapeli kuibia watu. Watu wamekuwa wakitumiwa barua pepe zenye jumbe zushi za kulaghai huku zikiwataka wasambaza zaidi ili...
Nimekuwa nikisikia kuwa Rais wa zamani wa Malawi, Dkt. Hastings Kamuzu Banda aliwahi kuwa Daktari wa Malkia wa Uingereza na alihasiwa asije akatembea na Malkia Elizabeth na kuzaa naye. Kuhasiwa kwake huko kulipelekea Dkt. Kamuzu Banda mpaka anafariki dunia mwaka 1997 akiwa na umri wa miaka 99 kutobahatika kupata mtoto yeyote. Malkia Elizabeth ii akiwa na Dkt. Kamuzu Banda (Mwaka 1985)
Takwimu ni taarifa (data) zilizokusanywa, zikahesabiwa, na kuchambuliwa ili kutoa ufahamu au maelezo kuhusu kitu fulani. Kwa mfano, takwimu zinaweza kuwa idadi ya watu katika eneo fulani, matokeo ya utafiti, au hata vipimo vya kisayansi. Takwimu zinaweza kutumika katika nyanja mbalimbali kama vile sayansi, biashara, sera, elimu nk ili kusaidia katika kufanya maamuzi mbalimbali na ikiwa takwimu hizo zitakuwa potofu zitasababisha kupatikana kwa matokeo potofu yatakayoharibu malengo na mipango ya jambo kusudiwa. Udanganyifu wa takwimu huweza kutokea au kufanywa katika uchambuzi wa data au utafiti. Wakati data zinakusanywa, kuchakatwa, na kuanaliziwa kunaweza kufanyika upotoshaji au udanganyifu wowote ili kutimiza lengo lolote...
Back
Top Bottom