JamiiCheck - Tanzania

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Kukoma hedhi ni wakati ambapo mzunguko wa hedhi wa mwanamke hukata. Ki kawaida hutokea mwanamke anapokaribia umri wa miaka hamsini. Wakati hedhi inapokaribia kukata, wanawake hupitia dalili mbalimbali kama mzunguko wa hedhi usio wa kawaida, matatizo ya kihisia na ya kimwili ambayo hawajawahi kuyapata. Mwanamke akinyanyua vyuma vizito (Chanzo: Adobe Stock) Kuna nadharia kwamba wanawake wanaofanya mazoezi ya kutunisha misuli na kunyanyua vyuma vizito vinaweza kusababisha mwanamke kufika (menopause) mapema kabla ya umri wake. Umri wa mwanamke kufikia kikomo cha hedhi ni umri wa 50.
Nimekuwa nikisikia kuwa wabunge wetu hawalipi kodi kwenye mshahara mnono wanaopata. Kuwa walimu wanalipwa Tsh 400,000 lakini kamshahara hako kanaliwa na PAYE. Wabunge wetu wakiwa kwenye vikao, sitting allowance na Perdiem wanakunja 470,000 kwa siku, Mshahara wa mwisho wa mwezi nao mnono hatari. Je, hakuna sababu ya wabunge kulipa kodi kwa ajili ya maendeleo ya nchi? Tena napendekeza hata yale marupurupu wanayopata nayo yakatwe kodi.
Kama ilivyozoeleka kwenye jamii nyingi kuwa ukiwa Rastafarian basi kwa asilimia kubwa utakuwa unatumia bangi/marijuana na majina mengine lukuki kama inavyojulikana. Leo kwenye mitandao ya kijamii kulikuwa kuna meme inasambaa ikiwa na ujumbe "Wakati Lucky Dube anaimba "Born to Suffer" me nilidhani ni sababu anavuta bangi" Meme hii ikanikumbusha article niliyowahi kusoma kuwa Lucky Dube alijiepusha na matumizi ya bangi, pombe na sigara ili kuwa mfano mzuri kwenye jamii.
Hatua za ukuaji wa mtoto huambatana na mabadiliko mengi ya kimwili. Mojawapo ya mabadiliko hayo ni kung’oka kwa meno ya awali na kuota kwa meno ya kudumu. Mdau wa JamiiForums ametoa hoja kuwa meno ya mtoto mwenye umri kati ya miaka 6-7 yanapotingishika kisha yakaendelea kukaa pasipo kung’olewa husababisha meno mengine kuota kwa pembeni, hivyo ni lazima yang'olewe ili kuepusha kutokea kwa tatizo hili. Madai haya yana ukweli kiasi gani?
Kuna kijiwe huku Bonyokwa tunapiga stori za kawaida kuhusu nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Sasa kuna jamaa kasema kuwa Rais wa awamu ya pili nchini Kenya, Hayati Daniel Arap Moi wakati anaingia madarakani hakuwa na mahusiano kabisa na hakutaka kujihusisha nayo kabisa. Nguvu kubwa alielekeza katika malezi ya watoto. Jambo hili lilimfanya ahudumu miaka 24 ya urais bila kuwa na mke (First Lady) jambo ambalo halijazoeleka ulimwenguni, kwamba kuwe na mtawala asiye na mwenza. Daniel Toroitich Arap Moi (Google)
Bado nipo njiapanda, nimesikia kuwa mwanamke mjamzito akinywa pombe kwa kiwango kikubwa wakati wa ujauzito basi huweza kusababisha changamoto kubwa sana kwa mtoto. Kuna wajawazito kadhaa nimepata kuwaona wakinywa pombe tena kali sana lakini hizo changamoto kwa watoto wao sijaziona. Baadhi ya changamoto nilizoambiwa ni kuwa na kichwa kidogo isivyo kawaida, uso bapa, macho madogo, pua ndogo nk Naomba kujua hili ili nimkanye mama kijacho kufakamia mipombe asijeleta balaa ndani.
Kuna mwanamama aliwahi nipa ushuhuda kuwa matiti yake yalianza kuanguka akiwa na miaka 23 kutokana na mitomaso aliyokuwa anafanyiwa na mpenzi wake wa kwanza. Aliendelea kwa kusema kuwa, kabla ya kuanza michezo na wanaume alikuwa na chuchu dodo zilizosimama na kuchoma. Hivi ni kweli kuwa matiti ya mwanamke yanapopapaswa na viganja vya mwanaume hupelekea kuanguka na kuwa ndala?
Link zinazowekwa kwenye taarifa zinaweza kutumika kwa njia kadhaa kuchangia upotoshaji wa taarifa kwa kuwaunganisha wasomaji kwenye tovuti zisizoaminika au zinazojulikana ili kutangaza habari za uwongo. Hii inaweza kuongeza uaminifu wa habari hiyo kwa watu wasiojua ukweli. Mathalani, 'links' katika machapisho ya kisayansi vinaweza kutumika kupotosha taarifa kwa njia kadhaa. Mara nyingine, waandishi wasio waaminifu wanaweza kuchagua na kunukuu vibaya matokeo ya utafiti ili kuendana na hadithi fulani au ajenda. Wanaweza pia kutumia 'link' kuelekeza kwa machapisho yasiyo na uhusiano au yanayojitokeza kama vyanzo vya kuaminika, huku wakichanganya ukweli na upotoshaji. Aidha, kutoa taarifa bila kutoa muktadha sahihi au kuchagua link...
Back
Top Bottom