JamiiCheck - Tanzania

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Nani asiyemjua mbabe Simba mfalme wa nyika? Yaani ukutane naye paaah! Utamzame machoni aone aibu na kuondoka? Bado siamini hili jambo naona hawa vijana wa ovyo wanataka kuniingiza chaka siku nikikutana naye mbashara nisichukue njia nyingine za kujiokoa eti nimtizame. Hivi kweli Simba huyu kweli wa kumwonea aibu binadamu kisa kumuangalia machoni ana kwa ana kwa ujasiri. Wakuu naombeni taarifa sahihi kuhusu hili jambo, huenda mada ikawa kichekesho lakini hili jambo linasemwa sana mtaani.
Matumizi ya tumbaku ni moja ya maafa ya afya ya umma yanayojulikana sana. Licha ya ripoti nyingi kuhusu afya ya umma, matumizi ya tumbaku yanazidi kuongezeka katika nchi zinazoendelea na zilizoendelea. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), takriban watu Bilioni 1.3 duniani wanavuta sigara ambapo 80% kati yake wanatoka kwenye nchi zenye uchumi mdogo na uchumi wa kati. Aidha, takriban watu Milioni 7 hupoteza maisha kutokana na athari za moshi wa sigara unaotokana na kuvuta sigara moja kwa moja au pia kuvuta moshi uliotolewa na mvutaji wa Sigara. Tumbaku huathiri karibu kila kiungo na mfumo katika mwili, ikisababisha matatizo mbalimbali kama vile saratani, Magonjwa ya mfumo wa upumuaji, Ugonjwa wa Mishipa ya Moyo, Kiharusi...
Kuna picha nimeona Rais Mstaafu wa Marekani, Barack Obama akizindua uidhinishaji wake wa mwisho wa mgombea urais 2022 nchini Kenya ambapo alionesha wazi kumuunga mkono Naibu Rais Ndugu William Ruto. Barack Obama ana vinasaba vya Ujaluo, sijui ilikuwa vipi akashindwa kumuunga mkono Mjaluo mwenzio Mwamba Raila Amolo Odinga. Chanzo: BBC === Video halisi iliyotumika kutengeneza picha hiyo
Leo nimesoma mtandaoni kuwa Vidonda vya tumbo(Ulcers) huweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Naomba kujua kama ni kweli maana siku zote mie najua vidonda vya tumbo huvipata mtu kutokana na mtindo wake wa maisha(kutokula) au kwa kutumia baadhi ya dawa ambazo zinaweza kuchubua utumbo. Sasa hii ya kuambukiza kwangu imekuwa mpya sana, tena mwandishi alifafanua zaidi kuwa eti iwapo mwenza wako ana ulcers basi uwezekano wa wewe kuupata ni mkubwa maana anaweza kukuambukiza.
Kumekuwepo na barua inayiosambaa Mtandaoni ikionesha kuandikwa na Mfalme Mswati III ametoa tangazo linalodai kuwa kutokana na uhaba wa Wanaume kwenye nchi yake, amewaomba wananchi wanaoishi Kusini mwa Jangwa la Sahara kuomba uraia kwenye nchi yake, na kila mwanaume atayeoa walau wanakwake 5 atamlipia gharama za harusi zao pamoja na kuwanunulia nyumba. Ukweli wa taarifa hii upoje?
Katika pitapita mitandaoni nimekutana na huyu chawa wa Mtoto wa Rais Museveni, Kainerugaba Muhoozi akimtuhumu Kakwenza Rukira kuingia makubaliano ya siri na umoja wa Ulaya nchini Uganda katika kuhamasisha ushoga nchini humo. Nakumbuka Uganda imezuia mahusiano ya jinsia moja na Rais Museveni amebana kweli kweli wazungu hawana pa kupumulia, naona wameamua kupitia njia za panya kuleta ushenzi wao.
TinEye ni nyenzo nzuri ya kutafuta picha kwenye wavuti ambayo inaweza kutumiwa kufanya uhakiki wa Picha. JamiiCheck imekuandalia utaratibu wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kutumia Nyenzo hii kufanya uhakiki wa picha. 1. Fungua Kivinjari Chako Anza kwa kufungua kivinjari chako kwenye kifaa chako cha mkononi au kompyuta. 2. Tembelea Tovuti ya TinEye Ingiza 'TinEye' kwenye sanduku la utaftaji la kivinjari chako na bonyeza kwenye matokeo yanayofanana na tovuti rasmi ya TinEye. 3. Pakia Picha Kuna njia mbili za kupakia picha kwenye tovuti ya TinEye Bofya kwenye kitufe cha 'Pakia Picha' au "Upload' kisha pakia picha unayotaka kufanya uhakiki. Ikiwa picha tayari iko kwenye wavuti, unaweza kunakili URL (Link) ya picha hiyo na kuibandika...
Back
Top Bottom