JamiiCheck - Tanzania

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Yandex ni njia nyingine ya utafutaji inayotumika sana kufanya uhakiki wa picha. JamiiCheck imekuandalia utaratibu wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kutumia Nyenzo hii kufanya uhakiki wa picha. 1. Fungua Kivinjari Chako Anza kwa kufungua kivinjari chako kwenye kifaa chako cha mkononi au kompyuta. 2. Tembelea Tovuti ya Yandex Ingiza 'Yandex' kwenye sanduku la utafutaji la kivinjari chako na bonyeza kwenye matokeo yanayofanana na tovuti rasmi ya Yandex. 3. Pakia Picha Kuna njia mbili za kupakia picha kwenye tovuti ya Yandex Bofya kwenye alama ya kamera iliyo kwenye sanduku la utaftaji la Yandex na chagua 'Pakia Picha' au 'Upload' kisha upakie picha unayotaka kufanya uhakiki. Ikiwa picha tayari iko kwenye wavuti, unaweza kunakili URL...
Baada ya kauli ya CDF wa Tanzania Jenerali Mkunda kusema kuwa 'Baadhi ya Wakimbizi wamepewa teuzi Serikalini katika nafasi zenye maamuzi' imenifikirisha sana nikakumbuka nilishawahi kusikia tetesi kuwa Paul Kagame wakati akiwa mkimbizi nchini Uganda, aliwahi kuhudumu kwenye jeshi la nchi hiyo na mpaka kufikia cheo cha Mkuu wa usalama wa Jeshi Uganda. Mpaka sasa tunaona jinsi Kagame anavyoisumbua Uganda labda kutokana na ukweli kuwa anaijua nje ndani. Je, ni kweli Paul Kagame aliweza kuaminiwa na kupewa cheo nyeti kwenye Jeshi la Uganda?
Matamshi ya chuki yaweza kuwa maneno au vitendo vinavyoonyesha hisia za uadui, dhihaka, au kutokuwajali kuelekea mtu au kundi fulani. Yanaweza kujitokeza kwa misingi ya tofauti za kijamii, kitamaduni, kidini, kisiasa, au mambo mengine. Chuki inafarakanisha makundi, huchangia vurugu na migogoro, na hudhoofisha jitihada zetu zote za amani, utulivu na maendeleo endelevu. Hata hivyo, sasa ukubwa na athari yake umesambazwa zaidi na teknolojia mpya za mawasiliano ambayo sasa yanawafikia watu wengi sana kwa haraka sana. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres anasema "Tunahitaji kuchukulia hotuba za chuki kama tunavyochukulia vitendo vyovyote vibaya: kwa kuzilaani, kutoziendeleza, kukabiliana nazo na ukweli na kuchagiza...
Habari wakuu, Nimeona taarifa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki imetambulisha noti yake itakayotumika katika nchi wanachama, iliyopewa jina la SHEAFRA (SHF). Wengi wameinukuu akaunti kutoka mtandao wa X (zamani Twitter) inayojulikana Government of East Africa Moja ya chombo kikubwa kilichoinukuu akaunti hiyo ni pamoja na ITV , binafsi bado nina mashaka na hii taarifa kutokana na kwamba akaunti maalum ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ninayoifahamu siyo hii. Ukweli ni upi?
Habari Wadau, Nimekutana na tangazo la kazi likionesha kuwa Kampuni ya usafirishaji ya Tilisho inahitaji Wafanyakazi kwa nafasi ya Wakatisha Tiketi na wahudumu wa ndani ya Mabasi. Nimepata mashaka baada ya kuona ukilifuata tangazo hili ndani yake linahitaji usambaze link kwenye magroup ya WhatsApp na Facebook ili kuendelea hatua inayofuata. Je, kuna ukweli juu ya Tangazo hili?
Kuna dada zetu wanapenda sana urembo hivyo kujiongezea baadhi ya vitu kama matako, kope, lenzi kwenye macho, matiti vimekuwa vitu vya kawaida sana kwao. Ukweli hayo yote wanayojiongea yanakuwa na madhara. Mimi nipende tu kutoa hadhari kuwa kope na lenzi bandia mnavyojiongezea ni hatari kwa afya ya macho yenu. Chonde chonde ridhikeni na mlivyoumbwa navyo. Khadija Omary ni mmoja wa wahanga wa kupofuka baada ya kuwekewa kope bandia. Ni hayo tu.
Salaam wakuu, Wakati mikoa mingi nchini ikiendelea kupata mvua ya kutosha, kwa wengine imekuwa neema kwao kwani sasa wanaweza kuvuna maji ya kutosha kwa ajili ya matumizi ya nyumbani, mifugo na hata mazao. Sasa kwa matumizi ya nyumbani ni pamoja na kuyatumia kwa kunywa bila kuyafanyia treatment yoyote. Tokea nakua kumekuwa na kasumba na kuaminishana kuwa maji ya mvua ni bora kwa kunywa. Mvua ikinyesha tumekuwa tukiyakinga na kunywa moja kwa moja bila kujua madhara yake Pamoja na kubeba vimelea vingi na kila aina ya takataka, pia kuna aina ya madini maji hayo hukosa kwa ajili ya afya ya binadamu. Pia kuna jamii zinaamini kuwa maji ya mvua yanatibu magonjwa mbalimbali. Maji ya mvua yanaweza kuwa safi lakini siyo salama.
Jukwaa la Jamiicheck lipo mahsusi kwa ajili ya kufanya uhakiki wa taarifa ili kujua kama ni kweli, uzushi au nadharia. Hukuwezesha raia kufanya uhakiki kwa kuweka maudhui ndani ya jukwaa yanayotakiwa kuhakikiwa na kutoa mchango wa kuhakiki taarifa hizo kwa kile wanachokifahamu. Je, ungependa Jamiicheck ihakiki jambo gani la kijamii ili upate kujua uhalisia wake?
Haya mambo yasikie tu, watoto wetu siku za shule huwa wanalazimishwa kulala tu punde wamalizapo kula. Hii ni hatari kwa mujibu wa tafiti za afya. Uelewa mdogo na kutojali kwa wazazi kunaweza kupelekea watoto wetu kupata madhara hapo mbeleni. Kulala mara baada ya kula ni kitendo ambacho hupendelewa kufanywa na mamilioni ya watu japokuwa tabia hii si nzuri kiafya, kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa na wansayansi wa chuo kikuu cha Loannina Medical watu wanaosubiri kulala kwa muda kidogo mara baada ya kula wana nafasi ndogo ya kupata ugonjwa wa mshtuko na hii ndio sababu inashauriwa kukaa masaa mawili mara baada ya kula ndipo kulala.
Wote mnaweza kufikiria ni namna gani mtu asiye mkazi au mfanyakazi au mwenye appointment kwenye makazi rasmi ya Malkia wa Uingereza angeweza kupenya bila kuonekana, akafanikiwa kuingia ndani ya jumba hilo, akapiga misele kidogo, akaingia ofisi ya Malkia Elizabeth kufyonza mvinyo maalum wa Malkia, na mwisho wa siku akazama ndichi kwenye hiyo room ya Malkia na kumkuta Malkia akiwa katikati ya njozi tamu, akaketi pembeni yake na kumsubiri Malkia aamke ili wayajenge/wapeane maelekezo. Basi kunaye dogo mmoja alileta makwaru na kufankiwa mpaka Malkia mwenye alipomsanukisha. Inadaiwa tukio hilo lilisababisha ulinzi zaidi uimarishwe na baadhi ya walinzi walifukuzwa.
Viongozi wanaweza kupotosha umma kwa njia mbalimbali ili kujiongezea umaarufu na kukubalika kwa wananchi. Mojawapo ya njia wanazoweza kutumia ni kutoa ahadi ambazo hawawezi kutekeleza au kuficha ukweli ili kuepuka lawama. Aidha, wanaweza kutumia propaganda na mawasiliano ya kisiasa yenye kuleta hisia za uaminifu na ufanisi, hata kama si kweli. Wakati timu ya wahakiki wa Maudhui (Fact Checker) wa The Washington Post ilipoanza kwanza kuhesabu madai ya uzushi au yenye kudanganya ya Donald Trump, ilirekodi madai 492 ya kutiliwa shaka katika siku 100 za kwanza za urais wake. Novemba 2 pekee, siku kabla ya kura za 2020, Trump alitoa madai ya uwongo au yenye kudanganya 503 aliposafiri kote nchini katika jitihada za kuomba kura akitaka...
Back
Top Bottom