Wadau nililima mahindi Kiteto nimejaliwa kupata gunia km 100 natafuta soko nchi ya jirani Kenya.
Mwenye kuweza kuniunganisha nikauze mazao yangu anipe mwelekeo
Mzuka wanajamvi!
Serikali au wadau mbalimbali wakitoa data kuhusu upungufu ama chakula kuwepo wanatumia mahindi. Baa la njaa ikiikumba nchi mahindi yanatumiwa kama kipimo cha chakula pekee kuonesha kama kuna njaa au la. Tuna ona serikali kupitia wizara ya kilimo inanunua mahindi tu meengii...
Miaka ya hivi karibuni kumezuka viwanda vingi sana mitaani vinavyosaga unga wa mahindi na muhogo, ubora wa unga huo u atia mashaka kwani viwanda husika haviko kwenye usafi unaoridhisha.
Kiwanda ambacho hakiko kwenye usafi hata ubora wa unga wake utatia shaka, ni wazi viwanda hivyo vina mashine...
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimewataka wakala wa chakula NFRA kuweka utaratibu mzuri ili kumaliza sintofahamu iliyopo juu ya ununuzi wa mahindi Manispaa ya Songea kwa kuhakikisha wananchi wote waliokwisha kuorodheshwa Mahindi yao yananunuliwa pamoja na kuongezwa kwa kituo kimoja cha ununuzi wa...
Tanzania bado ina safari ndefu ya kumwinua mkulima ili ajikwamue kutoka kwenye kilimo cha kujikimu kwenda kwenye kilimo cha kibiashara ambacho kitamwezesha kuwekeza kwenye sekta hiyo kikamilifu.
Zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania ni wakulima lakini wengi wao wanafanya kilimo cha kujikimu wakati...
Baada ya kusikia serikali imetoa bilioni 50 kwa ajili ya manunuzi ya mahindi.
Nikaona huu ndio wakati muafaka wa kuuza nikajaza howo zangu tatu mzigo kupeleka kwenye kitengo.
Dah nilichokutana nacho tajiri atabaki kuwa tajiri nae maskini atazidi kuwa maskini hasa kwenye nchi zetu za Kiafrika...
Amesikika Mh Waziri Mkuu bungeni akimpongeza Rais Samia kwa kuongeza pesa ya kununua Mahindi ya Wakulima zilizofikia Bilioni hamsini.
Kwa kadri ya ufahamu wangu Mh Rais hakuitoa hela hii kutoka kwenye Mshahara wake bali ametoa hela hii kutoka kwenye Mfuko wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa...
Ningependa kuchangia walau kidogo kuhusu mahindi kukosa soko
Hizo ni dalili la kutokua tayali hayo ni matokeo ya kuto kukijua vyema Tanzania endapo Kila mkulima stamina kisses Kama tuna to shawishi Hali itakuaje?
Hiyo ni neema kidogo tu ya mahindi tayari Changa moto mahindi tusiyachukulie ni...
Kumekuwa na kelele sana juu ya anguko la bei ya mahindi kote nchini. Kiasi ambacho imebidi CCM iingilie kati. Nimewaona wabunge wote hasa wa CCM wakionyesha kutorodhishwa kwao jinsi NFRA inavyonunua mahindi toka kwa wakulima.
Ongezekeo hili la wingi wa mahindi ni mwitikio wa wakulima kwani...
Bunge limesitisha kwa muda shughuli zake za leo ili kujadili changamoto ya bei duni inayowakumba wakulima wa mahindi nchini. Wabunge wameeleza kutoridhishwa na bei ndogo ya mahindi, bei ghali ya mbolea hivyo wameitaka Serikali kuiongeza hela NFRA ili inunue mahindi kwa wakulima.
Waziri wa...
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHATOA MAELEKEZO MATATU KWA SERIKALI, AHUENI KWA WAKULIMA WA MAHINDI NCHINI.
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa maelekezo matatu kwa Serikali kuhusu ununuzi wa mahindi ya wakulima, vituo vya kununulia mahindi pamoja na bei ya mbolea nchini.
Maelekezo hayo yametolewa...
Leo muda wa jioni nilikuwa maeneo ya Mbezi ya Kimara nilikuwa nimesimama namsubiri rafiki yangu pembeni kwa mbele kulikuwa na mtu anauza supu ya pweza na vipande vyake na ngisi na kachori.Nikiwa pale walikuja watu kadhaa kununua nilichokiona.
Mteja alikuwa anachukua kijiti cha kuchomea anatoboa...
Kupitia kwa WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imeshatoa sh. bilioni 15 kwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) ili kununua mahindi kutoka kwa wakulima.
“Uzalishaji wa mahindi ni mkubwa lakini na sisi pia tumeimarisha hifadhi yetu ya Taifa ya chakula. NFRA tumeipa fedha za...
Nimekuwa mjini muda mrefu sana
Nimeona kukaa mjini hailipi
Napanga niende kijijini nikalime
Niepukane na matozo ya serikali ambayo yanaletwa kila uchao
Niko kanda ya ziwa
Unanishauri nihamie wapi ambapo naweza kufanya kilimo cha mahindi karanga mahindi maharage na mpunga
Na nikafanikiwa...
Leo TBC 1 Tv,nimeona Mkuu mpya wa Mkoa wa Ruvuma amezungukwa na magunia ya mahindi,hakuna soko.
Hii inaashiria nini endapo aliyekuwepo mambo yalikuwa hayohayo? Ukienda mkoa wangu wa Rukwa ni yaleyale.
Tunakosaje sera endelevu ya soko la mahindi Kitaifa?
Kuna wale Malazy waliopinga safari ya rais Samia Suluhu kuja Kenya. Walisema kwamba rais Samia hapaswi kuja Kenya na alistahili kuendeleza roho mbaya na mikwaruzano aliyoanzisha mwendazake ambaye sitamtaja hapa. Lakini cha kushangaza ni kwamba baada ya rais Suluhu kutembea Kenya, sasa Kenya...
Habari marafiki zangu wapendwa?
Mimi naomba kujua jinsi nitakavyopika ugali wa mahindi, pia mboga zinazofaa (kama vile mchuzi wa nyama au biringani za kukaanga). Mimi ni mpishi mpya, lakini nitajaribu kuzipika vizuri kama iwezekanavyo.
Shukrani
Ripoti ya wizara ya mifugo kwa mwaka 2019 inaonesha kwamba sekta ya mifugo inachangia 6.9% ya pato la taifa,na kwa upande wa taarifa ya wizara ya Kilimo ya mwaka 2020 inaonesha kwamba sekta ya Kilimo inatoa robo tatu ya mauzo ya nje ya bidhaa,inachangia 95% ya mahitaji ya chakula nchini,26.8% ya...
Natafta wateja wa jumla wa mahindi kuanzia gunia hamsini na Bei ya mahindi ni 5000 kwa debe kazi yangu ni kumkusanyia atanilipa elfu moja kwa kila gunia na gharama za usafirishaji ni juu yake so kama kuna mtu unaweza niunganisha nae naomba nisaidie.
Namba ya simu 0688633630
Awali ya yote npende ktanguliza salamu, kwa yeyote mwenye connection za biashara za nafaka hasa mahindi, yaani nahitaji kuwa mnunuzi wa jumla kwa sehemu kama Geita, Rukwa na Shinyanga
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.