2024 Africa Cup Of Nations (AFCON) | Special Thread. Mechi ya fainali, FT: Nigeria 1 - 2 Ivory Coast. Ivory coast abeba ubingwa. 11.02. 2024

Taifa Stars ndio inawachezaji wenye umri mdogo zaidi (Average)
 
Taifa stars 75% ya wachezaji fitness Yao ni zero na hii ndiyo itatugharimu ikiwemo umri mkubwa n.k .

Angalia Mozambique , Cape Verde , Namibia au Angola mataifa Madogo kisoka wana fitness nzuri wanakimbiza Mpira .
Sasa hao fitness coach wa kigeni wanafanya kazi gani....tuwafukuze tuu
 
Refa aliyechezesha gama ya Zambia na Kongo uwa namkubali sana ananikumbusha Pielugi Corina.

Ukitaka kujua timu yetu ni mbovu wachezaji karibu asilimia 85 wanacheza ligi ya ndani ambayo mastaa wake ni kina Inonga, Mayele na Chama wakat timu zao za taifa ni chaguo la 3 la kocha ukiondoa Inonga ila huku kwetu ndio ma Godfather.
 
Tulikuwa tunachangisha Pesa za nini? Maana nimeangalia kwenye jukwaa mashabiki wa Taifa stars walikuwa ni Bongozozo na Ally Mayai pekee na watu kadhaa wakiwa wamevaa suti. Nikiona nchi nyingine wamepeleka mashabiki waluwalu kama akina Mzee wa utopolo wenye uwezo wa kujichafua mwili mzima na makorokocho yenye rangi za Taifa. Naamini kama garama za wachezaji caf wanalipa. Nilitarajia harambee zingewasafirisha mashabiki halisi wa mpira tunaowafahamu kutoka kwenye timu zetu
 
Bongozozo amejisafirisha mwenyewe na watu wake .

Tundu Lisu vilevile amejisafirisha mwenyewe na watu wake .
 
Tanzania hakuna tunachoweza kufanya kwa ufanisi yaani chochote tunachofanya sisi bas wenzetu wanaweza kufanya mara 4 zaid yetu.
 
yaha mashindano ya AFCON yanayoendelea yalipaswa kufanyika mwaka jana ila kutokana na hali mbaya ya hewa nchini ivory coast yakasogezwa mbele nakufanyika 2024 ndio maana yanaitwa AFCON 2023 kitu ambacho kitapelekea kuwa na mashindano mawili ya AFCON yanayofatana kwakua AFCON inayofata nimwakani tu hapo 2025 nchini morroco kabla ya nchi za tanzania,kenya na uganda kwa pamoja hawajaandaa AFCON nyingine 2027, kwakua hii AFCON 2023 imegongana kinyakati na mashindano ya ASIAN CUP 2024 yanayoendelea pia mda huu, ni mashindano gani yamekuwa na msisimko sana!? binafsi sijafatilia hata mchezo mmoja katika mashindano ya ASIAN CUP 2024 na nimejiuliza kwa mda leo swali hilo bila kupata majibu kwakua sina access ya kufatilia mashindano hayo. timu za taifa kama australia, japan na korea kusini zimekuwa na wachezaji baadhi maarufu wanaokipiga ulaya , mnaofatilia pia hayo mashindano ya ASIAN CUP 2024 mnijibu hapa! Japo sijaridhiswa na mahudhulio kwenye mechi nyingi za AFCON
 
Kule Asia Japan asipo beba ndoo itakuwa sio poa. Japan wapo vizuri sana. Pia kura yangu inaenda kwa Korea Kusini [emoji2406]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…