2024 Africa Cup Of Nations (AFCON) | Special Thread. Mechi ya fainali, FT: Nigeria 1 - 2 Ivory Coast. Ivory coast abeba ubingwa. 11.02. 2024

Jumla ya Magoli 143 yamefungwa katika mechi 48 mpaka sasa, wastani wa magoli 2.97 kwa kila mechi.

AFCON ya mwaka huu imevunja rekodi ya magoli 100 yaliyofungwa kwenye 2021 AFCON na Magoli 102 yaliyofungwa kwenye mashindano ya AFCON 2019.

Emilio Nsue anaongoza mpaka sasa kwakuwa na magoli 5.
 
Hahahaaa. Bado hujasema Mkuu.

Sisi tusio na timu yeyote apitaye na apite. 😂😂

Cc. Rafiki Mahondaw.
Yan wamejua kuifanya siku yangu kuwa ngumu😄 Cape verde walimtoa south kwakuwa walikuwa hawana mfungaji...😃 Ila Nigeria hii strikers wake hawezi kukuacha kwenye nafasi hata moja wakipata

Advantage nyingine ya Bafanabafana nadhani ni kujituma uwanjani sema tuone nani atapita... Baada ya kipenga cha mwisho
 
Yan wamejua kuifanya siku yangu kuwa ngumu😄
Hahahaa. Pole sana Mkuu.
Umeonaee. Osimhen na Lookman hawanaga masihara pale mbele.

Ila mnaweza enda final Mkuu mwishowe mkachukua ndoo. 😀
 
Klabu ya Chippa united ya South Africa wameikana kiana timu yao taifa leo na wanaamua kuiunga mkono Nigeria ambayo anadakia golikipa wao namba moja, Stanley Nwabali

Chippa united wanaitakia kila la heri timu ya taifa ya Nigeria

Ikumbukwe Chippa united hawana mchezaji yoyote kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Afrika Kusini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…