Absalom Kibanda awakosoa vikali CHADEMA, asema "Ukishakula nyama ya mtu huachi", Lema amjibu

Absalom Kibanda awakosoa vikali CHADEMA, asema "Ukishakula nyama ya mtu huachi", Lema amjibu

Yaani mwandishi wa habari ana support kugushi nyaraka kubwa kama za ubunge. Tanzania tuna kazi hawa eti ndiyo wadai haki wetu !🤔
Ndio ule weledi unaitwa WA kitanzania🤔
 
Hakupenda kuwa chongo kumbuka hilo, hujafa hujaumbika.

Kosoa alichokiandika mengine sio laz
Kwani walio.pa uchongo si ndo hao hao anaowalamba miguu sema labda anaogopa wasije ondoa na jicho la pili
 
View attachment 2229699

Mwanahabari mkongwe na Mchambuzi wa siasa Absalom Kibanda amekosoa maamuzi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwafukuza uanachama Halima Mdee na wenzake 18.

“Ni kweli Mdee na wenzake 18 walikosea. Msingi wa makosa yao ni kupinga ubabe wa kihistoria wa viongozi wenzao na kudai kwao haki kibabe. Ni kweli pia viongozi wakuu CHADEMA waliwahukumu kabla ya vikao. Kosa la kimaadili limetolewa 'hukumu ya kifo'.

“Huu ni ulaji wa kisiasa. CHADEMA inadai haki yake, akina Mdee wanapigania jasho lao. Orodha inaongezeka, hawakuanza na Davidi Kafulila, Zitto Kabwe, Wilbroad Slaa wala Kitila Mkumbo na hawatamaliza na hawa Wanawake 19. Ukishakula nyama ya mtu huachi,” – Kibanda.

Kumbuka kuwa Kibanda ni mmoja wa waandishi wakongwe waliowahi kufanya kazi kwa ukaribu na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na walikuwa na ukaribu hata nje ya masuala ya kikazi.

Kibanda aliwahi kuwa Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Free Media, wachapishaji wa magazeti ya Tanzania Daima na Sayari ambayo ni mali ya Mbowe, pia Kibanda amewahi kuinia matatizoni mara kadhaa kwa kuikosoa Serikali na kuonekana yupo upande wa CHADEMA, hivyo kwa kauli hiyo ni wazi kuna vitu havipo sawa.

GODBLESS LEMA AMJIBU
Baada ya kauli hiyo, mwanachama mkongwe wa CHADEMA, godbless Lema naye akamjibu kwa kuandika hivi:

"Kama utaendelea KUKAUKIWA nakushauri uende kwa Mwamposa niliambiwa anatoa mafuta ya kuvunja nira ya KUKAUKIWA. Hata hivyo jambo gumu ktk jamii ni pale wazee wenye masharti ya kula wanapo kuwa na njaa kuliko vijana wasio na masharti na diet. Sijui njaa ni nini sasa ?"
Wafuasi wa Chadema watampiga vita sana huyu jamaa , na kwa bahati mbaya Magufuli ambaye ndiye angebebeshwa lawama zote hapa hayupo tena. CHADEMA kama chama walianz sakata hili kwa munkali sana. Mnyika akaitisha waandishi wa habari na kupayuka mambo mengi sana. Majuzi nimesikia naibu katibu mkuu naye akirudia makosa yale yale ya kupayuka.

Hili ni jambo ambalo lilitakiwa lishughulikiwa kichama ndani bila makeke yoyote hadi hapo solution nzuri inapopatikana. Mnyika naye kama Katibu mkuu ndiyo hasara kubwa kwa chadema kwani hana hata punje ya busara katika kutatua migogoro. Hii shortcut inayotumiwa na chadema ya kuweka lebo za "msaliti" zikifuatiwa na kufukuza uanachama ni makosa yaliyo ndani ya damu ya Chadema, na ni sahihi kabisa kama jamaa alivyoiweka
 
Yaani mwandishi wa habari ana support kugushi nyaraka kubwa kama za ubunge. Tanzania tuna kazi hawa eti ndiyo wadai haki wetu !🤔
Hujitambui wewe.
Jamvi la ufurukutwa limekugubika.
Kwani hutambui kama kughushi ni kosa la jinai na convicted anafungwa.
Kama kweli walighushi mngewapeleka mahakamani, Wakitiwa hatiani kwa kughushi wanafungwa na automatically wanapoteza Ubunge na vyeo vyao chamani.
Kwa nini hawajawashitaki?
Kwa nini wamekimbilia kuwavua uwanachama wakati njia ya mkato ipo?
 
Wanaodai wabunge hao waligushi nyaraka kwa Nini CHADEMA hawakuwabuluza mahakamani kwa kosa hilo na badala yake wachukue mkondo waloeenda nao?
UMBWA KABISA criminal ni kazi ya Polisi Chadema wanatakiwa kuthibitsha tu
 
Halafu kuna mahali wameandika eti Lema amejibu!!! Majibu yako wapi, mafuta ya Mwamposa?!
 
Kwa hiyo ni haki yao kufoji nyaraka ili mradi kupinga matumizi ya nguvu kudai haki?
Hii nchi ikija kupata maendeleo hata angalau kuwafikia Kenya basi ujue Mungu amekufa.
Nchi ina akili takataka sana.
N huyo ndio anaitwa mwandishi nguli,sijui anawaza kwa kutumia nini.
 
N huyo ndio anaitwa mwandishi nguli,sijui anawaza kwa kutumia nini.
unaweza kujiuliza ndiyo huyu wa miaka ile "Raia Mwema na Tanzania Daima"

Kweli njaa inaumba !!
 
Mbona Kibanda ameandika kwa mihemko sana?

Anaposema; "Ni wazi kuwa viongozi wa Chadema waliwahukumu kabla ya vikao" anamaanisha nini?

Vile vikao vya KK na baadae Baraza Kuu hakuviona?

Ajabu Kibanda anazungumzia haki ya kina Mdee, haki ipi, ya kufoji? au ya mtu kuchomolewa gerezani kimya kimya usiku? Hawa waandishi na njaa zao wanataka tuwe na taifa lisiloheshimu sheria.

Sasa naanza kuamini, kuna kundi la waandishi wa habari [ wakujitegemea na wa vyombo mbalimbali] wamenunuliwa na serikali ili kuichafua Chadema, kwa kuwatetea wale wahuni 19 bungeni.

Yule wa kwanza ameshajulikana yupo humu ndani, huyu Kibanda ni wa pili, tusubiri wa tatu, wanne, .....

Samia na serikali yake ni corrupt, kuwalipa wale wahuni posho na mishahara kule bungeni, na kuwapa posho hawa waandishi njaa kueneza uzushi.Mbowe jitoe kwenye meza ya mazungumzo.
Kati ya Kada ambazo zimejaa Makanjanja nchi hii ni HABARI na SHERIA.

Sent from my M2003J15SC using JamiiForums mobile app
 
Hata huyo Lema ipo siku! ipo siku! ipo siku! Hataamini kama ni yeye anashughulikiwa na Chadema! Tunza hii comment!
 
Hakupenda kuwa chongo kumbuka hilo, hujafa hujaumbika.

Kosoa alichokiandika mengine sio lazima.
Ameandika Uchongo anaficha Ukweli amba wengi tunajua..

Kumtoa mtu Gerezani Usiku na kumpa ubunge sio jambo dogo...

Ni Chongo pekee ndio hatoweza liona ho
hili....

Kibanda ni njaaaaaa
 
Kundi la kina Halima limewanunua waandishi kujaribu kuwatetea - sijui hela wamepata wapi za kuwalipa....

wamo wakongwe njaa kali kina Kibanda, Paskali wa Jf na wengineo...

kweli Taifa letu linaliwa.
 
Back
Top Bottom