Kuhusu hili la kuuzima moto wa richmond ambao kiukweli bado tulikua na kazi nao aliwakera wengi mpaka reginald mengi ambae pia alikua nyuma yake alikasirika sana na nasikia mpaka akawaagiza wahariri wake wasimpe tena sitta coverage kwenye vyombo vyake vya habari,na hata sijui kama uswahiba wao umerejea katika hali ya kawaida,mengi alichukia sana inasemekana.Lakini kama mnavyojua shinikizo lilikua kubwa sana ndani ya ccm kipindi kile ambamo mafisadi walikua na nguvu kubwa mno wakati ule,na kama si jitihada na busara za wajumbe wawili wa kamati kuu bwana ABDULRAHMAN KINANA na BERNARD MEMBE,Sam six ilikua avuliwe uanachama,lakini wawili hao na hasa kinana ambae alionekana kama hana upande alisimama kidete kumtetea spika na kuwaeleza wazi wazi wajumbe wa kamati kuu akiwemo mwenyekiti kwamba spika hana matatizo yeyote anafanya kazi yake na kiukweli anakisaidia chama ambacho kimechafuka..ndio akaponea kwenye tundu la sindano na kupewa masharti ya kuuzima huo mjadala bungeni kwa kuwa unakichafua chama na serikali yake,hapa ndipo alipokosea mzee wangu huyu,hakutakiwa kuyumba kwani tayari alikua na base kubwa ya wabunge na sisi wananchi kiujumla,lakini akaufyata mkia ndani ya ccm lakini bado alikua na uchungu ndio maana mkawa mnasikia habari za CCJ zikipamba moto kwa kasi,ni kweli sitta na wenzake walipanga kujionadoa kwenye chama kama udhibiti dhidi yao kama wapambanaji wa ufisadi utaendelea na hasa kama jk atamrudisha Ngonyani Lowassa serikalini (mpango ambao alikua nao kweli),lakini lowassa hajarudi serikalini mpaka leo na wao nadhani baadae wakaona hakuna haja ya kujitoa badala yake wapambane na mafisadi goi goi wakiwa humo humo ili kama ikibidi mafisadi ndio waondoke...matokeo yake ndio hii issue ya kujivua magamba japo inaonekana kukwama kutokana na udhaifu wa mwenyekiti na pia hujuma za mafisadi.Lakini habari ya ccj ama kujiunga na chadema vyote vilikuwepo na vikao vya kina sitta na viongozi wa chadema na ccj vilishika hatamu sana kipindi hicho,mh.mboe kama anaingia na kusoma haya atakua anaelewa nazungumzia nini,sitts ndio alikua awe mgombea urais wa chadema badala ya slaa kwa msiojua,na hasira za chadema kwa sitta na huu wimbo wa usaliti wa sitta unaoimbwa hapa ni kutokana na tukio la sitta kuwatosa chadema dakika za mwisho,ikabidi wamtafute mgombea wa fasta bwana slaa,ambae hata hivyo kwa muda ule uliobaki alifanya vizuri,nampongeza kiukweli kwa kuwa alitokeo from no where na kutikisa,kama angekua sitta angemshinda jk kwa wakati ule,alikua juu mno.