Afghanistan: Talibani imepiga marufuku wanawake kuongea ama kubadilishana mawazo. Marufuku mwanamke kuongea na mwanamke mwenzie

Hao talibani kuna mambo wanafanya ambayo sio katika sheria za kiislamu kabisa au kinyume na uislamu,kama mtu anauona uislamu kupitia talibani hakika hatapata uislamu sahihi,hao asilimia kubwa mambo yao kama wanaharakati

Uislamu haujakataza wanawake kuongea na wanawake wenzao na wala si sunna ya Mtume wala maagizo ya Allah. Wake za Mtume tu walikuwa wanaongea na wanaume nyuma ya pazia katika kuwaelekeza mambo fulani fulani ya dini,kama hiyo haikuruhusiwa je ilikuwaje wakeze wakafanya hivyo?

Kuhusu wanaume kunyoa nywele au ndefu wanaruhusiwa sana,ila si katika uislamu sijui kunyoa kiduku na stahili za ajabu ajabu,kama unaondoa nywele zote basi ondoa na kama unanyoa kawaida basi nyoa kwa heshima

Kuhusu kufuga ndevu hiyo ni sunna sio lazima kwa wanaume kufuga ndevu,ingawa ni bora kufuata sunna ya Mtume,binafsi nanyoa ndefu,sio agizo la lazima la dini

Kuhusu wanawake kwenda saluni,wanawake wanatakiwa kujipamba kwa ajili ya waume zao,wapendeze na wanoge,ila naona kuna namna labda hizo saluni zimeonekana ni sehemu ambazo kuna ajenda nyingine zinafanyika

Kuhusu wanawake kuongea kwenye redio au television,kwa mfano katika tv yapaswa mwanamke ajistiri anapokuwa hewani na si kuwa uchi kwa mujibu wa uislamu,kuhusu kuongea kwenye redio,hiyo hata huku Tanzania kuna redio moja Redio imani nayo kipindi fulani fulani walikataza lakini wakapewa hoja mbona wake za Mtume Muhammad (s.a.w) walikuwa wanaongea na wanaume nyuma ya pazia,kwahiyo hapo hoja nzito ilipatikana

Kwahiyo si kila linalo fanywa na hivi vikundi vyenye misimamo mikali ni uislamu bali mengine ni taratibu zao binafsi

Asante
 
Hili ni la kwenu hamuwezi kulikwepa labda uislamu haukutokea middle east ntakuelewa ila
Uislamu matopeni
 
hawa vichaa tu eti sheria za kiislam inamaana hizo sheria wanazijua wao tu ulimwenguni..eti mwanamke hana ruksa kuongea na mwanamke mwenzie il mumewe tu hawajiulizi kabla ya kuolewa si yupo kwa familia yake mama,bibi,Shangazi,dada zake wote hao marufuku kuongea nao.! sema hawa wajinga matamanio ya nafsi zao ndio wanafanya sheria za dini wakati ndani ya uislam wenyewe hamna hizo sheria kwahiyo wanaume hawana sheria
 
Hawa wenzetu wanashida Gani na wanawake?? Maana Kila kukicha wanatunga Sheria za kumkandamiza mwanamke, je wanawake waliwakosea Nini?? Aisee hii dini haifai hata kidogo.
 
Umeshavunja ungo uko kwa familia yako unasubiri nini? Olewa haraka upate wa kuongea naye! Else, shut up your mouth.
 
Hawa wenzetu wanashida Gani na wanawake?? Maana Kila kukicha wanatunga Sheria za kumkandamiza mwanamke, je wanawake waliwakosea Nini?? Aisee hii dini haifai hata kidogo.
Dini imemweka mwanamke katika daraja ya juu iliyo bora kabisa. Hapana dini nyingine popote duniani yenye viwango hivi vya ubora kwa mwanamke. Tatizo mnatazama kwa mtazamo hasi!
 
Ni nchi yao acheni watumie uhuru wao vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…