#COVID19 Afisa Elimu Mkoa wa Arusha na Muuguzi waliofanya maigizo ya chanjo wasimamishwe kazi mara moja

#COVID19 Afisa Elimu Mkoa wa Arusha na Muuguzi waliofanya maigizo ya chanjo wasimamishwe kazi mara moja

MR TOXIC

Senior Member
Joined
Jun 4, 2019
Posts
190
Reaction score
525
Sitaki kutia neno, Jionee mwenyewe na uchukue hatua.




UPDATE: 06 August, 2021

Waziri wa OR-TAMISEMI, Ummy Mwalimu amemuagiza Katibu Mkuu OR-TAMISEMI kumsimamisha kazi Mwalimu Omary Abdallahemed Kwesiga ambaye ni Mkuu wa Idara ya Elimu ya Msingi Halmashauri ya Jiji la Arusha.

Aidha ameagizaScolastica L. Kanje Afisa Muuguzi Msaidizi apelekwe Baraza la Wauguzi na Wakunga kwa hatua zaidi.

Zaidi soma > #COVID19 - Arusha: Watumishi waliofanya igizo kwenye chanjo ya Corona wasimamishwa kazi

Nidhamu.jpg
 
Baadaye wakija kuchukua damu waone kama chanjo imefanya kazi, watu kama hawa watachangia data za uwongo........hapo ndo watafiti wanapochanganyikiwa na kuanza kujiuliza, why? what has gone wrong with this data? au wametuchanganyia damu ya kenge.....
 
Hawa ndio wanawapa vichwa Kauzu wanaoamini Wazungu wamekaa wanataka kuwaua.
 
Teknolojia inaruhusu hata editing kufanyika kwenye video..
Wapinga chanjo wapo kazini.
Tuliwambia pesa mlokula zitawatokea puani lakini hamkusikia. Haya sasa mmeanza kukwama na maigizo yenu ya danganya toto
 
Nilijua tu😂 zamu yangu sasa??
Nitadungwa sindano lenye maji ya hill water
 
Hapa wahusika wanapaswa kulitolea maelezo ili kuondoa sintofahamu
 
Meta mada kuwa serious.
Watu tumechanja for real kwa malengo endelevu tu ya kudhibiti kuenea kwacorona.
Msituletee vituko vya kwenu mitaani.
 
Sijaelewa lolote!

Jana katika shule moja ya msingi hapa zilipelekwa chanjo
Hahah!!
watoto kusikia kuwa ni chanjo
wakapita madirishani, wengine mlangoni
wakatoka nduki ya ajabu
speed mbaya sana
Kasi kubwa mno
Hadi makwao wakawaambia wazazi wao
kuhusu walichotaka kufanyiwa shuleni.
Hahaha ikapigwa yowee hatari
mwenye mkuki sawa
mwenye panga sawa
mwenye kisu sawa
mwenye fimbo sawa
mwenye upinde sawa
mwenye Jiwe sawa
mwenye manati sawa
mwenye nondo sawa
Hahah
hadi shuleni
wakakuta walimu na Jamaa wa chanjo
wazazi full Gadhabu plus mahasira kibao!
Ilibidi police waitwe fasta kuokoa Jahazi!
ila baadhi ya wazazi na walezi ilibidi wachukuliwe na police wakaondoka nao!
Hizi chanjo hahah yetu macho
 
Back
Top Bottom