Aibu kubwa! Msomi unakosaje kazi ya kufanya nchi hii yenye kila aina ya rasilimali?

gunia la bangi ni 1.2m(unnecessary needs), gunia ya mahindi elfu 20000, nchi ina vituko hii...nlilima mahindi nimeyaweka ndani bei mbovu ukiuza hasara..na nna fanya kazi sa hali ipoje kwa wanaotegemea kilimo cha mahind ?.. mleta post hajui game lipoje kaweka na post inayohusu RC wa mwanza ambaye ye mwenewe mfanyakazi wa kaz ya kupewa..kmmmk....ccm mbwa sanaa
 
Acha watu waendelee kupaka piko na kujichubua nyuso hapa mjini. Tutakutana uzeeni
 
Unatafuta uchochoro tu wa kujifichia. Hicho kifaa unachotumia kuingia humu jf ni mtaji tosha kabisa. Muda unaotumia kujaribu na kushindwa utalishwa na wanaokulisha hivi Sasa ambapo umekaa kwao ukisubiri ajira ambazo hazipo
 
Ndugu yangu kilimo siyo sawa na betting inayoanza siku ama muda mchache kabla ya mchezo.

Kuna muda wa miezi 3 mpaka 5 ya kuandaa mashamba. Vijijini tunaishi kijamaa, hivyo baiskeli tunaazimana tu wala hazikodishwi. Au waweza kuinunu (sh elfu 70) ukaitumia kusombea samadi miezi mitano. Acheni kukaa mjinini mnaishia kujichubua usoni na kupaka piko tu
 
Hivi kilimo kinachoongelewa huku jukwaani ni hichi kilimo nachokijua mm au kingine jamani. Kilimo kisikieni tu.
Tunakiongelea hicho hicho. Hakuna kazi rahisi hapa duniani, yoyote inayoingiza pesa. Nia na uvumikivu ndivyo hugmfanya mtu afanikiwe
 
Ukiwa na nia inawezekana kabisa. Omba fedha toka kwa hao wanaokulisha na kukuvisha miaka yote hii ambayo unasubiria qjira.

Ama uza hicho kifaa kinachokuwezesha kuingia humu jf. Pia save hiyo hela ya bando utapata mtaji wa kilimo. Kilimo hwkihitaji mtaji mkubwa ndiyo maana hata bibi ywngu ni mkulima
 
Hakuna mtu ambaye ni mjinga wa kuacha biashara inayolipa.
Boda boda inalipa na iko wazi pesa ya fasta fasta mkononi tu! Hukosi elf 10 p

 
Kilimo kingelipa kusingekuwepo na machinga mijini.
Machinga wapo kwasabb ya fikra potofu kwamba kilimo ni cha watu wasiosoma ama wazee tu.

Kumbuka Dangote(tajiri na 1 Afrika) katoboa maisha kupitia kilimo.
 
Unafurahisha genge ....!
 
Kilimo cha biashara siyo aina ya mazao yanayolimwa bali ni malengo uliyojiwekea. Unaweza kulima maharagwe, mahindi, mpunga ama viazi kwa lengo la kuuza ili kupata pesa. Tayari hicho kinakuwa kilimo cha biashara.

njoo basi huku kanda ya ziwa upime kama utapata hayo malengo ya kibiashara
 
Unajua uwekezaji wa maua wewe, biashara hiyo mfano halisi TANZANIA/Mount Meru FLOWERS Arusha anashare Mzee Sarakikya mkuu wa jeshi mstaafu na mzungu na Mama mmoja anaitwa mama Uriyo, ni uwekezaji wa billions bro
uwekezaji kwenye maua ndio nimesema ni mfano wa kilimo biashara...nisome tena!
 
Hizo ekari tano zilime kwa mkono wako mwenyewe. Anza miezi mitatu kabla ya msimu
Wewe unajishughulisha na nini kwanza tuanzie hapo naona unaleta umotivasheno spika tu apa dangote dangote ile kiwanda ya simenti ni kilimo pia maana nimeanza kupata mashaka na akili yako

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Unatafuta uchochoro tu wa kujifichia. Hicho kifaa unachotumia kuingia humu jf ni mtaji tosha kabisa. Muda unaotumia kujaribu na kushindwa utalishwa na wanaokulisha hivi Sasa ambapo umekaa kwao ukisubiri ajira ambazo hazipo
Sa
Unatafuta uchochoro tu wa kujifichia. Hicho kifaa unachotumia kuingia humu jf ni mtaji tosha kabisa. Muda unaotumia kujaribu na kushindwa utalishwa na wanaokulisha hivi Sasa ambapo umekaa kwao ukisubiri ajira ambazo hazipo
Sasa nikiuza kifaa hiki madini ya JF nitakuwa nayapata wapi?
Sema nitafute namna nyigine ya kupata mtaji na sio kuuza kifaa cha ujuzi aaaah!!!
 
 
Machinga wapo kwasabb ya fikra potofu kwamba kilimo ni cha watu wasiosoma ama wazee tu.

Kumbuka Dangote(tajiri na 1 Afrika) katoboa maisha kupitia kilimo.
Kama kilimo kingelipa kwa kutumia nguvu nani anapenda kukaa barabarani kuganga Ili apate 2000 au 3000 kwa siku.
Kilimo ni pesa,akili,maarifa na ujuzi.
 
Hela iliyotupwa kwenye ndege ingewekezwa kwenye miundombinu ya umwagaliaji na chain nzima ya kilimo ingemaliza tatizo la ajira na la machinga na bodaboda kupoteza mda mijini.
Na wala tusingetegemea kukopa Ili kuendesha nchi.
Wakoloni waliendesha nchi kwa kilimo na wakafanya makubwa Sana.Soko la mazao huko duniani hatuwezi lijaza hata KILA mtza akilima mazao.
Tatizo sera mbovu.
Ni aibu sana kwa mito kwa mito kumwaga maji bahari yapotee bure inatakiwa maji ya mito yaishie mashambani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…