Aibu kubwa! Msomi unakosaje kazi ya kufanya nchi hii yenye kila aina ya rasilimali?

Aibu kubwa! Msomi unakosaje kazi ya kufanya nchi hii yenye kila aina ya rasilimali?

Mwamba kumbuka kuna kilimo cha kujikimu na kilimo cha biashara. Huku kanda ya ziwa kilimo ni cha kujikimu, ziada ndio tunauza.

Lau tungefanya kilimo cha biashara, maarifa ambayo hatunayo kama wenzetu wa Nyanda za juu kusaini, mjadala huu ungekuwa na afya.

Mfano WA kilimo cha biashara ni kilimo cha maua huko Kaskazini, kilimo cha chai na Pareto huko kusini.
Unajua uwekezaji wa maua wewe, biashara hiyo mfano halisi TANZANIA/Mount Meru FLOWERS Arusha anashare Mzee Sarakikya mkuu wa jeshi mstaafu na mzungu na Mama mmoja anaitwa mama Uriyo, ni uwekezaji wa billions bro
 
Kwani umachinga na bodaboda vinahitaji ujinga mkuu? Kazi ya elimu ni kupambana na changamoto za mazingira yako.

Nchi zetu za Afrika hazina mazingira yanayomfanya msomi aishi mtaani kwa elimu yake. Watu hawasomi vitabu, watu hawahitaji msaada wa kisheria, hawahitaji ushauri wa kisaikolojia, hawahitaji ushauri wa kuanzisha na kuendeleza biashara, hawahitaji ramani kujenga nyumba, hawahitaji ushauri wa kiafya na kitabibu. Haya yangefanyika wasomi wangekuwa lulu.
[emoji3581]
 
Jiweke kwenye miguu ya kijana asiye na ajira mtaji wake ni elimu huo uwekezaji kulima kibiashara anapataje, Ukizingatia umesema bado yuko anafua chupi za shemeji na hata Kama ardhi ni bure
Aanze kuendesha bodaboda mwaka mzima ili apate mtaji halafu ajiingize kwenye kilimo. Tunategemea msomi atatafuta taarifa sahihi za anachotaka kulima na hivyo atapata faida
 
Mkuu unaongea vitu practically havipo,kula mashambani as if unapanda leo na vitu vinaota kesho!
Hapana. Hapa namjibu aliyeuliza kuwa mhitimu akienda vijijini kujiajiri kwenye kilimo, atakula nn muda ambao atakuwa anaandaa shamba na kusubiria mazao yakomae?
 
Hivi wewe ambaye unajiita umesoma halafu inalalamika kuwa huna kazi, unafahamu kwamba unajidhalilisha?

Acha wakose kazi vijana wa Ulaya na Marekani huko lkn siyo hapa Tanzania. Ardhi yenye rutuba isiyohitaji mbolea imejaa tele kwann usijiajiri kwenye kilimo?

Ardhi ya bure ipo tele katika mikoa ya Tabora, Katavi, Tanga, Ruvuma, n.k.

Kwani lazima ukae mjini? Mbona watanzania zaidi ya 80% wamejiajiri ktk kilimo tena wengi wao hawana madigrii kama ninyi lkn maisha yanasonga na ni watulivu wala hawapigi kelel za kukosa ajira.

Wengi wenu mmesomeshwa na wazazi wenu ambao ni wakulima wasiokuwa na elimu. Hawajawahi kuajiriwa na yeyote maisha yao yote.

Mmerogwa na nani ninyi mnaoenda shule? Kama hizi shule na vyuo mnavyoenda ndiyo vinawapeni huu ujinga mm nashauri zifutwe.

Kuna vijana chungu nzima walioishia darasa la saba wanaendeleza maisha kwa kilimo na shughuli nyingine hatusikii wakililia ajira. Wewe msomi umesoma halafu unalia. Usingesoma je? Jinga kabisa!

View attachment 1974112
Kilimo sio nguvu bwashee killmo ni pesa.Kilimo kingekuwa kinalipa usingeona hayo mapori.
Hapo ni sawa na kusema pwani ardhi tele watu wavivu awalimi kalime wewe kama ni rahisi.
Kilimo kingelipa kusingekuwepo na machinga mijini.
 
Huyu engineering graduate afanye kilimo basi ungemuandaa kwa ku incorporate agriculture kwenye syllabus aliyokua anasomea.
Siyo kweli, hiki ni kinatumika Kama kichaka tu Cha kufichia udhaifu wa wasomi.

Wale wanaomaliza SUA wamesoma miaka 4 Mambo ya kilimo mbona hawajiajiri kwenye kilimo?

Kuna graduates kibao wamejiajiri kwenye bodaboda na machinga. Kwenye syllabises zao kuna umachinga na bodaboda?

Graduates wengi wana mentality kwamba kilimo ni kazi ya wasiosoma. Ndiyo maana mnatoa visingizio kibao
 
Umetengeneza hoja yako vizuri sana 👍 tunahitaji cross sectoral approach ie mtu kasoma HR apewe basi idea ya kilimo na ufugaji au ujasiliamali hivyo kwa wahandisi na fani zingine lakini serikali haiwezi kukwepa jukumu la kuweka mazingira wezeshi
Hapa hamna kitu mnajificha tu kwenye hizi sababu. Graduates wanaoingia kwenye bongo flava walifundishwa? Wale waliomaliza SUA mbona hatuwaoni kwenye kilimo?
 
Mkuu Unafikir hatulimi sasa mtu unalima na mahindi unapata ya kutosha ila sasa changamoto n nying kuliko faida mkuu mm n mwenyej wa mbeya ukiacha mbali madawa na mbolea ukija kupiga usafir ukija kupiga vibarua ukija kupiga tozo kod haya unataka kuuza Unakuta gunia ef 30 soko market n tatizo pia
Sawa mkuu pamoja nachangamoto unapitia lakini sio sawa na kukaa tu kusubiri ajira
 
Niko tyr mkuu nikopeshe mtaji nitakuripa nikivuna kwa riba nafuu nami niingie huenda unarengo la kutusaidia wasomiii . Maana nijaribu kuangalia hiyo ardhi ya bure wakaniambia wanakodisha alfu hamsini kwa ekari .

Mafanikio ni zaidi ya juhudi na akili
Mtaji unao tayari, hiyo elimu ni mtaji miubwa sana. Wewe ni zaidi ya bibi yako aliyeko kijiiini lkn anaishi kwa kutegemea kilimo.
 
Huku kusoma kwa madesa sio kusoma. Ukijaribu kusoma vitabu vya Library ukaacha kusoma notes ambazo hata hazieleweki, huwezi kumaliza. Halafu tunajiita wasomi. Wasomi kweli???
Safi sana mkuu. Umepiga pale pale kwenye mshono.
 
Mkuu kilimo cha kisasa lazima uwe na mtaji, na siyo wote waliosomea kilimo......wengine ni magwini wao wanataka kuucharaza mdomo tu pesa iingie.
Mr Bin (sijui ni Mr. Been mtajua wenyewe). Huyu alisomea uhandisi wa umeme lkn leo ni mchekeshaji wa kimataifa. Msomi sahihi ni yule anayebadilika kulingana na mazingira
 
Kwaiyo nikiwapa vyeti watanipa mashamba na pembejeo au mi ndo sijaelewa elimu ni mtaji kiaje

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
Tumia akili yako kulima kwa mtaji mdogo unapata mazao.mengi. kwa mfano unaweza usitumie mbole za viwandani badla yake ukakusanya samadi toka kwa wafugaji kwa kuwapati pesa kidogo sana. Ukamwaga samadi hekari tano. Ukavuna mpk dunia ikakushangaa
 
Kwaiyo nikiwapa vyeti watanipa mashamba na pembejeo au mi ndo sijaelewa elimu ni mtaji kiaje

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
Tumia akili yako kulima kwa mtaji mdogo unapata mazao.mengi. kwa mfano unaweza usitumie mbole za viwandani badla yake ukakusanya samadi toka kwa wafugaji kwa kuwapati pesa kidogo sana. Ukamwaga samadi hekari tano. Ukavuna mpk dunia ikakushangaa
 
Back
Top Bottom