Ajali mbaya Inyala Mkoani Mbeya, idadi ya waliofariki yafikia watu 19

Ajali mbaya Inyala Mkoani Mbeya, idadi ya waliofariki yafikia watu 19

Makala hii hapa chini niliiandika Facebook mwezi wa Saba baada ya Ile ajali mbaya ilioua watu zaidi ya 20 pale Inyala . Bado hatujasahau na hata arobaini za waliokufa zikiwa hazijatimia Leo Tena wamekufa wengi zaidi chanzo kikiwa kilekile, ufinyu wa Barabara, mlima na mteremko mkali, kufeli breki n.k . Kama hatua za zarura hatizochukuliwa hakika tutalia sana maana hili eneo ni zaidi ya machinjio .

Niliandika hivi [emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]

Barabara ya Tunduma Hadi Dar es salaam naamini ndio barabara ya kwanza nchini kupitisha magari mengi ya mizigo kwa kuwa inahudumia nchi karibu kumi. Ajabu barabara hii hasa kuanzia Igurusi ndipo tatizo linapoanzia hasa hasa ajali kuanzia Ilongo Hadi mlima nyoka kisha mlima Iwambi na Mlima Senjele.

Huwa haziishi siku mbili bila kutokea ajali kwenye maeneo ya mlima Iwambi, Senjele, mlima nyoka Hadi Ilongo maana ndio maeneo yenye milima na miteremko mikali.

Shughuli kubwa ipo katikati ya Jiji kuanzia Nsalaga Hadi mbalizi, hapo ndipo Pana utitiri wa ajali za bajaji, pikipiki na magari maana ni barabara Moja tu hutumika kwa vyombo vyote vya moto.

Kibaya zaidi barabara hii yote kuanzia Tunduma Hadi Igawa ni barabara nyembamba yakizamani kwa kuwa ilijengwa zamani sana .

Kama Mzee Kinana ameliona hili tatizo nadhani imefikia Wakati Sasa amshauri boss wake ambaye ndiye rais wa nchi barabara mpya ijengwe haraka maana kwa wingi wa magari yanayopita Mbeya barabara haiwezi Tena kuhimili.

Pia
Kwa maoni ingependeza sana barabara ya malori itengwe na barabara ya magari madogo na haya ya abiria kama ilivyofanyika pale Arusha ambapo wamejenga barabara maalumu ya magari ya mizigo inayopita nje ya Jiji la Arusha kuanzia Ngaramtoni Hadi USA river . Mfano, kwa hapa Mbeya kuanzia pale Ilongo barabara ya Malori ijengwe mpya ipite bondeni kule chini ije itokezee Ndundu Uyole kisha ipite Isyesye ikatize Nanenane iende Hadi Ivumwe juu ikatokezee Tazara ikunje Iwambi chini ikatokezee Mbalizi Nsalala ndio iendelee Hadi Tunduma kisha hii ya Sasa ijengwe mpya ibaki na magari ya abiria na magari madogo.

Nayasema haya sababu Huwa haziishi siku mbili bila Lori kupoteza mwelekeo barabara ya Mlima nyoka Hadi Shamwengo ambapo ndipo penye milima na miteremko mikali sana . Hata ajali ya mwezi huu iliyoua zaidi ya watu 20 pale Inyala akiwemo mwalimu Iddy Mwandete ilisababishwa na Lori kuvamia Costa na vibanda sababu ya kufail breki kwenye mteremko wa Itewe kwenda Inyala.

Eneo hili limekuwa hatari mno kwani licha ya barabara kuwa ndogo, mbovu na yenye Konakona inapita kwenye mlima na mteremko mkali ambapo magari ya mizigo Huwa rahisi kufeli breki .

Kwa katikati ya Jiji ndipo napo panahitajika ujenzi mkubwa wa barabara angalau kuwe na njia nne kama Ile barabara ya Majengo Hadi Tengeru.
Ukiwa katika Jiji la mbeya unashindwa kuelewa hili ni Jiji au wamelisingizia, maana barabara ni ndogo, imejaa mashimo na imebonyea sana hasa maeneo ya uyole njia panda, Mteremko wa Nzovwe na Maeneo ya kuelekea Sokoine. Barabara ni changamoto kubwa sana ambapo bila kujengwa mpya ajali na usumbufu utaendelea kuwa mkubwa maana Kuna ongezeko kubwa sana la magari na watu ndani ya mkoa hasa jijini.

Mkoa wa Mbeya na Mkoa wa Songwe ni mikoa ambayo ni kama maghala ya Chakula hapa Tanzania. Unapozungumzia Mbeya unazungumia store ya Chakula lakini kiukweli kihuduma hasa barabara ni mkoa uliosahaulika sana. Wilaya ya Mbeya hasa halmashauri ya Mbeya vijijini ndio wilaya inayotoa viazi karibu mwaka mzima viazi vinavyoenda kuliwa Dar es salaam, Zanzibar, Nairobi, Kongo, Zambia na kwingineko lakini ndio halmashauri ambayo imesahaulika kabisa kwa barabara nzuri.

Kuna barabara ya Isyonye kwenda Makete, barabara ya Mswiswi kwenda Makete hizi ni barabara ambazo zibahitaji lami kwa haraka sana . Ni barabara ambazo zinapitisha malori yaliyobeba viazi, vitunguu swaumu, mahindi, mbao na mazao mengine mwaka mzima kwa wingi mkubwa lakini ajabu Kuna msimu hazipitiki sababu ya mashimo, matope na utelezi.

Ipo barabara ya Mbalizi Hadi Izyira, Mbalizi Hadi Ikukwa n.k ni barabara muhimu kwa uchumi wa nchi hii lakini nani wakuzikumbuka Ikiwa mbunge hata kuzizungumzia bungeni hatusikii,!!

Chondechonde Serikali, ikumbukeni mbeya kwa barabara maana Hali sio nzuri kabisa. Hali ya barabara mkoa wa Mbeya ni mbaya ikizingatiwa mbeya ni lango la nchi za SADDC na ndio lango la kuingia border kubwa kuliko zote Tanzania yaani Tunduma.

Mfikishieni Salam Rais, waziri wa fedha, waziri wa ujenzi, spika wa bunge na wadau wote wa maendeleo. Mzee Kinana alipita hapa Jana awe Balozi mzuri maana yeye ni shuhuda.

Ni hayo machache
Ndimi
Mwanshinga Jr
Hayo ndio machache? Huwajui watz kuhusu kusoma
 
Makala hii hapa chini niliiandika Facebook mwezi wa Saba baada ya Ile ajali mbaya ilioua watu zaidi ya 20 pale Inyala . Bado hatujasahau na hata arobaini za waliokufa zikiwa hazijatimia Leo Tena wamekufa wengi zaidi chanzo kikiwa kilekile, ufinyu wa Barabara, mlima na mteremko mkali, kufeli breki n.k . Kama hatua za zarura hatizochukuliwa hakika tutalia sana maana hili eneo ni zaidi ya machinjio .

Niliandika hivi [emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]

Barabara ya Tunduma Hadi Dar es salaam naamini ndio barabara ya kwanza nchini kupitisha magari mengi ya mizigo kwa kuwa inahudumia nchi karibu kumi. Ajabu barabara hii hasa kuanzia Igurusi ndipo tatizo linapoanzia hasa hasa ajali kuanzia Ilongo Hadi mlima nyoka kisha mlima Iwambi na Mlima Senjele.

Huwa haziishi siku mbili bila kutokea ajali kwenye maeneo ya mlima Iwambi, Senjele, mlima nyoka Hadi Ilongo maana ndio maeneo yenye milima na miteremko mikali.

Shughuli kubwa ipo katikati ya Jiji kuanzia Nsalaga Hadi mbalizi, hapo ndipo Pana utitiri wa ajali za bajaji, pikipiki na magari maana ni barabara Moja tu hutumika kwa vyombo vyote vya moto.

Kibaya zaidi barabara hii yote kuanzia Tunduma Hadi Igawa ni barabara nyembamba yakizamani kwa kuwa ilijengwa zamani sana .

Kama Mzee Kinana ameliona hili tatizo nadhani imefikia Wakati Sasa amshauri boss wake ambaye ndiye rais wa nchi barabara mpya ijengwe haraka maana kwa wingi wa magari yanayopita Mbeya barabara haiwezi Tena kuhimili.

Pia
Kwa maoni ingependeza sana barabara ya malori itengwe na barabara ya magari madogo na haya ya abiria kama ilivyofanyika pale Arusha ambapo wamejenga barabara maalumu ya magari ya mizigo inayopita nje ya Jiji la Arusha kuanzia Ngaramtoni Hadi USA river . Mfano, kwa hapa Mbeya kuanzia pale Ilongo barabara ya Malori ijengwe mpya ipite bondeni kule chini ije itokezee Ndundu Uyole kisha ipite Isyesye ikatize Nanenane iende Hadi Ivumwe juu ikatokezee Tazara ikunje Iwambi chini ikatokezee Mbalizi Nsalala ndio iendelee Hadi Tunduma kisha hii ya Sasa ijengwe mpya ibaki na magari ya abiria na magari madogo.

Nayasema haya sababu Huwa haziishi siku mbili bila Lori kupoteza mwelekeo barabara ya Mlima nyoka Hadi Shamwengo ambapo ndipo penye milima na miteremko mikali sana . Hata ajali ya mwezi huu iliyoua zaidi ya watu 20 pale Inyala akiwemo mwalimu Iddy Mwandete ilisababishwa na Lori kuvamia Costa na vibanda sababu ya kufail breki kwenye mteremko wa Itewe kwenda Inyala.

Eneo hili limekuwa hatari mno kwani licha ya barabara kuwa ndogo, mbovu na yenye Konakona inapita kwenye mlima na mteremko mkali ambapo magari ya mizigo Huwa rahisi kufeli breki .

Kwa katikati ya Jiji ndipo napo panahitajika ujenzi mkubwa wa barabara angalau kuwe na njia nne kama Ile barabara ya Majengo Hadi Tengeru.
Ukiwa katika Jiji la mbeya unashindwa kuelewa hili ni Jiji au wamelisingizia, maana barabara ni ndogo, imejaa mashimo na imebonyea sana hasa maeneo ya uyole njia panda, Mteremko wa Nzovwe na Maeneo ya kuelekea Sokoine. Barabara ni changamoto kubwa sana ambapo bila kujengwa mpya ajali na usumbufu utaendelea kuwa mkubwa maana Kuna ongezeko kubwa sana la magari na watu ndani ya mkoa hasa jijini.

Mkoa wa Mbeya na Mkoa wa Songwe ni mikoa ambayo ni kama maghala ya Chakula hapa Tanzania. Unapozungumzia Mbeya unazungumia store ya Chakula lakini kiukweli kihuduma hasa barabara ni mkoa uliosahaulika sana. Wilaya ya Mbeya hasa halmashauri ya Mbeya vijijini ndio wilaya inayotoa viazi karibu mwaka mzima viazi vinavyoenda kuliwa Dar es salaam, Zanzibar, Nairobi, Kongo, Zambia na kwingineko lakini ndio halmashauri ambayo imesahaulika kabisa kwa barabara nzuri.

Kuna barabara ya Isyonye kwenda Makete, barabara ya Mswiswi kwenda Makete hizi ni barabara ambazo zibahitaji lami kwa haraka sana . Ni barabara ambazo zinapitisha malori yaliyobeba viazi, vitunguu swaumu, mahindi, mbao na mazao mengine mwaka mzima kwa wingi mkubwa lakini ajabu Kuna msimu hazipitiki sababu ya mashimo, matope na utelezi.

Ipo barabara ya Mbalizi Hadi Izyira, Mbalizi Hadi Ikukwa n.k ni barabara muhimu kwa uchumi wa nchi hii lakini nani wakuzikumbuka Ikiwa mbunge hata kuzizungumzia bungeni hatusikii,!!

Chondechonde Serikali, ikumbukeni mbeya kwa barabara maana Hali sio nzuri kabisa. Hali ya barabara mkoa wa Mbeya ni mbaya ikizingatiwa mbeya ni lango la nchi za SADDC na ndio lango la kuingia border kubwa kuliko zote Tanzania yaani Tunduma.

Mfikishieni Salam Rais, waziri wa fedha, waziri wa ujenzi, spika wa bunge na wadau wote wa maendeleo. Mzee Kinana alipita hapa Jana awe Balozi mzuri maana yeye ni shuhuda.

Ni hayo machache
Ndimi
Mwanshinga Jr
Serikali ikome kutufanya watu wa Mbeya na Nyanda za Juu kafara wao..

Hii Barabara yote ni hatarishi,magari yanaongezeka kuanzia malori hadi magari binafsi na Yale ya IT..

Wabunge wa Mbeya bajeti ijayi msikubali upumbavu wa Serikali wa sijui tunamalizia upembuzi sijui upuuzi gani,mkatae..

Serikali ianze mara moja kujenga Mbeya bypass na kupanua hiyo barabara maana upande wa Inyala ni Majanga,upande wabalizi ni Majanga..
 
Wabunge wa Mkoa wa Mbeya na Songwe mwaka ujao msikubali msibukali upuuzi wowote wa serikali na blaa blaa za hiyo barabara..

Malori yameongezeka kadiri uchumi wa Nchi na Nchi jirani unavyokua,magari binafsi kuanzia IT hadi ya watu binafsi nayo hivyo hivyo,barabara inazidi kusongamana..

Lazima hiyo barabarani ipanuliwe haraka,na Mbeya bypass ijengwe maana Hapo Uyole kwenda Inyala ni Majanga,Meta kwenda Mbalizi kote ni Majanga,hivyo hivyo ukienda hadi Tunduma.
 
ukiwa mtumiaji wa barabara na unapaswa kujua kitu kinaitwa Defensive driving...

Hapo ambapo eneo ni finyu madereva wanapaswa kwenda mwendo mdogo na kuwa na tahadhari na kuacha uzembe....
 
Serikali ikome kutufanya watu wa Mbeya na Nyanda za Juu kafara wao..

Hii Barabara yote ni hatarishi,magari yanaongezeka kuanzia malori hadi magari binafsi na Yale ya IT..

Wabunge wa Mbeya bajeti ijayi msikubali upumbavu wa Serikali wa sijui tunamalizia upembuzi sijui upuuzi gani,mkatae..

Serikali ianze mara moja kujenga Mbeya bypass na kupanua hiyo barabara maana upande wa Inyala ni Majanga,upande wabalizi ni Majanga..
Hakika, yaani ni kama wameamua watumiaji wa hii barabara hasa wenyeji wa Mbeya kuwa Mbuzi wa kafara .

Yaani umeongea points sana maana barabara ni ndogo afu Ina mzigo wa magari ya IT, malori maelfu, mabasi na magari madogo na ya kawaida . Kibaya zaidi barabara ni ndogo na ni mbovu .

Kuanzia Shamwengo Hadi Mlima nyoka ni Kama machinjio pananuka damu za walipa Kodi wanaokomolewa makusudi.

Nilishauri hii barabara waihanishie kule chini malori yajitenge maana ni mengi na ndio yanayokata breki na kuua watu Kila Wakati.

Yaani ni mengi yakusema ila ukweli inatisha sana, mbunge wetu mwenyewe ni bubu tu maana mlima Iwambi na Inyala kote ni kwake Sasa sijui haoni .


Au kwakuwa wao hupita kwa ulinzi na ving'ora.!!!!
 
Hawana habari kila siku kusifia utendaji wa rais pumbavuu kabisa huku raia wakifa kila siku

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Lakini nadhani Kuna kitu wanaficha, hivi kipi kigumu kumueleza ukweli rais au waziri mkuu ??!

Pili naamini rais anajua huu ukweli wa hii barabara maana spika ni mwenyeji hapa .

Kiukweli sijui naweza pata wapi namba ya raisi nimfowardie hiki Kilio maana it's too much .

Leo watu wamekufa hatujui nani anafuata maana sote tunaitumia hii barabara
 
Mkuu, tujitahidi kuandika machache yanayo eleweka, mengi mno.
Nimekuelewa sana ndugu japokuwa niliandika ombi , pendekezo na ushauri kwa kuwa ni mwenyeji wa haya Maeneo ndio maana nimeandika kuwa wajitahidi kuhamisha malori kwa kuyajengea njia Yao kule chini itengane na hii ya njia ya Sasa.

Lkni nimekuelewa sana
 
Nimepita hapo siku si nyingi, hiko kipande cha Ilongo mpaka Uyole na Kedeghe mpaka Mbalizi ni hatari mno.

Barabara nyembamba na miteremko ni mikali. ?Malori makubwa, ma-bus yaendayo kasi, gaei ndogo, bajaji na pikipiki vyote humohumo.

MUNGU tu huwa anatuepusha. Serikali ifanye jambo pale, tena mapema.
 
Kila ajali inayotokea lazima umhusishe kinana, kuwa makini na maneno yako ndugu traffic, watakukamata wakusweke ndani 😅
 
Nayasema haya sababu Huwa haziishi siku mbili bila Lori kupoteza mwelekeo barabara ya Mlima nyoka Hadi Shamwengo ambapo ndipo penye milima na miteremko mikali sana . Hata ajali ya mwezi huu iliyoua zaidi ya watu 20 pale Inyala akiwemo mwalimu Iddy Mwandete ilisababishwa na Lori kuvamia Costa na vibanda sababu ya kufail breki kwenye mteremko wa Itewe kwenda Inyala.
Kinatokea kijitu kinasema askari warudi barabarani kumbe ni kipiga deal ya rushwa kumbe ajali nyingi ni ubovu wa miundombinu

 
ukiwa mtumiaji wa barabara na unapaswa kujua kitu kinaitwa Defensive driving...

Hapo ambapo eneo ni finyu madereva wanapaswa kwenda mwendo mdogo na kuwa na tahadhari na kuacha uzembe....
Tatizo la hili eneo sio Mwendo. Tatizo ni mteremko na Mlima kuwa mkali pia ufinyu wa Barabara, barabara kuwa mbovu na zaidi barabara Ina magari mengi kuliko uwezo wake .

Inahudumia magari ya Kila namna, makubwa kwa madogo ya mizigo na ya abiria .

Yaani kwa ujumla panatakiwa hatua za haraka sana maana Hali ni mbaya
 
Back
Top Bottom