Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Ni pamoja na barabara zetu kutokuwa za kiwango cha Kimataifa, ubovu wa magari, madreva kutozijua sheria za barabarani.

Kwani ni Ajali zote huwa zinasababishwa na mwendokasi?? Vipi kuhusu umakini wa dereva barabarani??

Ku-overtake kwenye kona au mlima, ku-overtake magari zaidi ya mawili kwa mpigo tena yote yakiwa kwenye mwendokasi, service za mabasi yenyewe lakini pia wakati mwingine ni uzembe tu wa madereva wengine kwa mfano ile ajali iliyosababishwa na Passo hivi majuzi..
 
Jawabu ni Smart phone

Huawei Ascend Y530,download application iitwayo "My tracks"- controller akae siti yoyote ya BASI,safari ianze.
Speed,umbali, vyoote vitaonyeshwa na muda uliotumika kituo hadi kituo!

Mahitaji:-
1)smartphone kama iliyotajwa hapo juu au iliyo bora zaidi.

2)mtu(operator) wa simu hiyo
3)power bank(chargers)

4)My track(application) haihitaji mtandao wa simu ila smartphone iwe na line ya sim(sim card)


Utaratibu

Smartphone ikaguliwe na RTO au wakala wake!
Dereva asini kuwa smartphone yenye IMME 12345678... Ndiyo itakayo record mwendo wa basi lake kwa siku hiyo!

Kama una mawazo bora zaidi changia

asante kwa ujuzi huu wa tekenolojia nadhani pia wahusika wamekusoma na wataitumia ili kudhibiti ajali zitokanazo na mwendo kasi ingawa si kila ajali inasababishwa na mwendo kasi
 
Dereva asaini kuwa simu inatrack mwendo? Dereva gani akubali
 
Hayo ndio mambo muhimu ya kupewa kipaumbele kwanza.. Hii habari ya mwendokasi hatutaweza kupambana nayo kwa haraka hivi..

Ni pamoja na barabara zetu kutokuwa za kiwango cha Kimataifa, ubovu wa magari, madreva kutozijua sheria za barabarani.
 
Naunga mkono hoja. Hao wanaotetea ni miononi mwa wanaofikiri ari ni kishada
 
''Kutokana na ajali za barabarani ambazo watalawa kama vile wameshindwa kusimamia au kuchukua hatua za dharura kunusuru maisha ya watu ambayo yanapotea kila siku; Ningekuwa kiongozi ningesema haya yafuatayo:

''Sitaki kusikia ajali zinatokea, hivyo basi kamanda wa usalaama barabani wa eneo usika (eneo la ajali), mkuu wa wilaya wa eneo n.k , barua zao ziko tayari kufukuzwa kazi kama hayo yatatokea katika eneo lao ikiambatana na kutunga sheria ya kufungwa kwa miaka 3 jela kushindwa kuweka mikakati ya kuzuia ajali''

MATOKEO:Wakuu hao wataweka mitakati ya kudhibiti ajari, hutasikia ajari za hovyo ovyo.

2.Kama wauzaji wa madawa ya kuleya wamewekewa sheria kali,kwa nini madereva na wamiliki wa kampuni ya usafirishaji yasiwekewe sheria kali.

Mfano🙁a)ikithibitika ni uzembe wa dereva;Dereva akisababisha ajari atalipa fidia ya sh TZS 10 billion Na kifungo cha maisha jela
(b) Wamiliki wa mabasi hayo pia watalipa fidia ya TZS 10 billion na kufungiwa kufanya shughuli za usafirishaji kwa miaka isiopungua 5

3.Serikali kufuta vyuo vya mitaani ambavyo havina sifa za kufundisha udereva.

Je kama haya yakisimamiwa kutakuwa na ajari barabari


WADAU TUJADILI

Dah natamani umpokee pr dr kwa miezi michache iliyobaki ili utimize
 
Watanzania inabidi tuwe analytical zaidi ya kuwa na majibu mepesi kama suluhisho la ajali barabarani. Usalama bararani ni idara kama zilivyo idara zingine za serikali kwa hiyo haitatarajiwi iwe bora yenyewe tu kama kisiwa, Kwani idara ipi Tanzania inayofanya vizuri zaidi ya hii? Je ni afya? yawezekana watu wanaokufa mahospitalini kwa uzembe,kukosa dawa au pesa za kulipia matibabu ikawa kubwa kuliko wa ajali za barabara.Vilevile wangapi wanadhulumiwa ardhi?angalia migogoro ya wafugaji na wakulima,wangapi wako magereza au polisi bila makosa?Escrow, EPA na mengine.Wazembe sio madereva tu wako kila sekta tofauti ni impact tu zingine hazionekani kwa haraka ila ni mbaya sana kuliko hata za madereva. Ajali ni matokeo ya corrupt system.
 
''Kutokana na ajali za barabarani ambazo watalawa kama vile wameshindwa kusimamia au kuchukua hatua za dharura kunusuru maisha ya watu ambayo yanapotea kila siku; Ningekuwa kiongozi ningesema haya yafuatayo:

''Sitaki kusikia ajali zinatokea, hivyo basi kamanda wa usalaama barabani wa eneo usika (eneo la ajali), mkuu wa wilaya wa eneo n.k , barua zao ziko tayari kufukuzwa kazi kama hayo yatatokea katika eneo lao ikiambatana na kutunga sheria ya kufungwa kwa miaka 3 jela kushindwa kuweka mikakati ya kuzuia ajali''

MATOKEO:Wakuu hao wataweka mitakati ya kudhibiti ajari, hutasikia ajari za hovyo ovyo.

2.Kama wauzaji wa madawa ya kuleya wamewekewa sheria kali,kwa nini madereva na wamiliki wa kampuni ya usafirishaji yasiwekewe sheria kali.

Mfano🙁a)ikithibitika ni uzembe wa dereva;Dereva akisababisha ajari atalipa fidia ya sh TZS 10 billion Na kifungo cha maisha jela
(b) Wamiliki wa mabasi hayo pia watalipa fidia ya TZS 10 billion na kufungiwa kufanya shughuli za usafirishaji kwa miaka isiopungua 5

3.Serikali kufuta vyuo vya mitaani ambavyo havina sifa za kufundisha udereva.

Je kama haya yakisimamiwa kutakuwa na ajari barabari


WADAU TUJADILI

Kuwafukuza kazi watu usalama barabarani utakua umetumia nguvu badala ya akili, hata kuwalipisha na kuwafunga jela madereva utawaonea maana vyanzo vya ajari hata serikali inahusika kwa sababu kuna barabara nyingi sana mbovu
 
Kwani ni Ajali zote huwa zinasababishwa na mwendokasi?? Vipi kuhusu umakini wa dereva barabarani??

Ku-overtake kwenye kona au mlima, ku-overtake magari zaidi ya mawili kwa mpigo tena yote yakiwa kwenye mwendokasi, service za mabasi yenyewe lakini pia wakati mwingine ni uzembe tu wa madereva wengine kwa mfano ile ajali iliyosababishwa na Passo hivi majuzi..

Hapo kwenye red umeongea mkuu......umesahau na hili la ufinyu wa barabara, na mwendo kasi kwenye kona...
 
Jawabu ni Smart phone

Huawei Ascend Y530,download application iitwayo "My tracks"- controller akae siti yoyote ya BASI,safari ianze.
Speed,umbali, vyoote vitaonyeshwa na muda uliotumika kituo hadi kituo!

Mahitaji:-
1)smartphone kama iliyotajwa hapo juu au iliyo bora zaidi.

2)mtu(operator) wa simu hiyo
3)power bank(chargers)

4)My track(application) haihitaji mtandao wa simu ila smartphone iwe na line ya sim(sim card)


Utaratibu

Smartphone ikaguliwe na RTO au wakala wake!
Dereva asini kuwa smartphone yenye IMME 12345678... Ndiyo itakayo record mwendo wa basi lake kwa siku hiyo!

Kama una mawazo bora zaidi changia

Mkuu' hizo ndio simu utakazosikia zinaongoza kwa kuharibika na kuishiwa charge' waanzishe tu hako kamchezo mafundi simu wengi watafahamiana sana na madereva wa mabasi
 
Tufanye sasa tayari sheria ulizoziainisha zimepitishwa halafu mimi ndo kamanda usalama barabarani mathalani Dodoma.

1.Ikibainika dereva wa basi alikuwa speed inayozidi 40km/hr abiria mtaumia aisee mtakula bakora za kutosha na dereva ananyang'anywa leseni.Dar-Mza siku mbili.

2.Dereva akibainika amelewa,anaswekwa lupango miaka mitano(hakuna msamaha wa rais) na kufanyishwa kazi ngumu.

3.Ikitokea ajali na watu wakapoteza maisha,mmiliki wa hicho chombo atapaswa kuwalipa fidia(actually kifuta machozi) 80mil kila marehemu na 200mil kwa majeruhi wenye ulemavu wa kudumu kama kisababishi cha ajali ni ubovu wa chombo au uzembe.

4.Kama chanzo cha ajali ni ubovu wa chombo basi dereva,makenika,mmiliki watakuwa answerable NB hizi kesi haziendi mahakamani ni kitengo kinakuwepo maalumu kwa ajili ya ajali.

5.Mabasi yote na malori ya usafirishaji hayataruhusiwa kuwa barabarani yakitembea 300,000km

6.Madereva wa malori na mabasi wawe na elimu ya kidato cha sita na kuendelea na lazima awe na uzoefu wa 10yrs bila ajali ndo akabidhiwe gari kwengine.

7.Bodaboda akipata ajali kama abiria hajafa basi anapewa yeye hiyo pikipiki na unamlipa fidia na bakora unakula.

8.Basi likifika stendi kabla ya mda uliopangwa abiria mnatoa maelezo na bakora juu.

Nitaendelea.......
 
Ndugu wanaJF, Salam.
Takribani mwezi mmoja sasa, ajali za barabarani zimeongezeka kwa kasi kubwa na zinasababisha vifo na vilema vya kudumu kwa watanzania wenzetu.

Ongezeko hili linaacha maswali mengi kiasi cha kushindwa kuyapatia majawabu stahiki.
Mfano; (a). Ongezeko hili ni kutokana na kuingizwa kwa magari mabovu barabarani?.
(b). Ongezeko hili ni kutokana na kuajiliwa kwa madereva wasio na uzoefu?.
(c). Ongezeko hili ni kutokana na mivutano ya kimasirahi(mikataba & posho) kati yadereva na boss wake?.
(d). Ongezeko hili ni matokeo ya ongezeko la askari wa usalama barabarni?.

Kwa jumla, ni vigumu kupata majawabu stahiki. Kwa sababu hiyo, naombeni michango yenu, nini kifanyike kunusuru maisha ya watanzania?.

Mod, uzi huu ni mhimu kwa maisha ya watanzania. Please, naomba msiufute ama kuunganisha na zingine hapa JF.
 
Back
Top Bottom