Ajali ya Gari Karatu Arusha: Coaster yaua Wanafunzi na walimu wa Lucky Vincent (karibu wote)

Ajali ya Gari Karatu Arusha: Coaster yaua Wanafunzi na walimu wa Lucky Vincent (karibu wote)

dah ndio maana mimi watoto wakinambiaga maswala ya kwenda ziara nawakataliaga kwa sabab ya vitu kama hivi ila kwakuwa wao hawajui waniita mkoloni yan inafikia hatua wakiwa wananiulizia wanasema"mama,mzee mkuda yupo ndani au bado hajaludi"........dah maumiv ya kupoteza mtoto ni mazito jaman mi yashanikuta !

yan mimi watoto wakinambiaga haya mambo ya ziara nawauliza mchango ni tsh ngap wakishanambia nawapa hiyo pesa nawawambia nendeni mkatembee kuna siku mtoto alijibu jibu flan sitasahau,alinijibu"baba wewe sio mzee ila mbona una mambo ya kikoloni hivo,ungekuwa unatukataza bila kutupa hizi pesa ambazo zingekuwa ghalama ya trip tungehisi m'bahili"
Mkuu pole sana kwa kuyajua maumivu hayo,maelezo yako yamenitoa machozi kwa kweli,tunahangaika sana na hawa watoto wao hawajui tu,wakienda trip huna amani wala furaha hadi watakaporudi salama,natamani kuwakataza wakiniambiaga,lakini huzuni wanayokuwa wanananionyesha na wanajua ninauwezo wakuwalipia,huwa naumia sana,nikiwaruhusu hawajui maumivu ninayokuwa nayo mm hadi warudi
Wakuu habari za leo,

Muda huu kuna ajali mbaya imetokea maeneo ya karatu basi la shule limeanguka kabla ya kuingia karatu mjini na kuua watoto wengi ambao idadi yake bado haijafahamika. Wanafunzi hao wanaokadiriwa kuwa wa darasa la 7 inasemekana ni wa shule inayoitwa Lucky Vicent ya Arusha ambao walikua wanaenda karatu kufanya mitihani ya mashindano na shule za karatu. Kwa mujibu wa shuhuda basi hilo lilikua limebeba watoto zaidi ya 40 na wengi wao (zaidi ya nusu) inasemekana wamepoteza maisha akiwemo dereva na walimu.

Ntawapa updates soon nipo jirani na eneo la tukio na mvua inanyesha sana nimeshindwa kutoka kufika eneo la tukio.
Tuendelee kuwaombea
 
Habari mbaya sana, poleni wazazi mm ni mmoja wa wazazi ambaye sipendi kabisa vi trip vya pamoja iwe ni kwa watu wazima au watoto i prefer private transport
Hata private, ikifika imefika japo public ni kizunguzungu
 
Asbh yangu imekuwa mbaya..Ee MUNGU wapokee watoto hawa kwenye ufalme wako na uwape wazazi na ndugu moyo mkuu!
 
Nimepata habari isiyo na shaka kuwa gari aina ya coaster limeua watoto karibu wote waliokuwa wanaelekea mjini Karatu kwa ziara ya kimasomo, taarifa zinasema wamebaki watoto wawili tu wengine wamefariki, shule inaitwa Lucky Vincent Nursery & Primary School ipo Arusha ni medium schools,kwa wenye updates tunaomba mtupe

Picha: Soon ntaziapload ni ajali ya mda huu
Mungu awalaze mahali pema peponi
----------------------

UPDATE: Coaster ina jumla ya abiria 58 na wote wanasadikiwa wamefariki,maiti zimepelekwa hospitalini na watu wameondoka eneo la tukio,mvua inanyesha

UPDATE: Picha zinakuja soon ripota yuko eneo la tukio..

19a4fcd1c935e4c031670cd880a46bc5.jpg

.........................
UPDATES:Magari ya polisi yametanda kila kona na maiti zimebebwa na magari ya polisi
Tayari kuhifadhiwa
...................
UPDATES:Ni watoto wanne(4) wanasadikiwa wako hai ila wako mahututi kabisa na kuna wasi wasi vifo vikaongezeka
UPDATES:Lucky vincent nursery school bus
62d62ef75dec257e496254f5cfb2808e.jpg

UPDATES:Shughuli za uokozi
a198eaa3cab45eec73b51943888b0a63.jpg
Ni nadra binadam wooote wakafariki lazima wawili watatu Mungu anaweza kuwanusuru.
 
Inasikitisha sana..

Ingawa ajali haina kinga... Na kifo hakina hakina hodi... Ni ni shida sana kusafiria magari mabovu...

Shule nyingi kwenye ziara za kusafiri eneo moja kwenda jingine, wanakodisha magari ambayo yapo tayari kwa safari za mbali...


Cc: mahondaw
 
Innocent lives lost!!!!Inahuzunisha ,Inasikitisha ,Utakuta walitoka shuleni wakiwa wanafuraha,bashasha wakifurahikia wanapokwenda!Ooh maskini wamepoteza maisha!Gone too soon!
 
Innalilahi wainaillahi rajiuni!l can imagine how their parents are feeling now!mama zao sasa hivi wanamumivu wanatamani wangekufa wao,baba zao wanatamani wangeweza kupambana na hicho kifo!dah,Allah wape waja wako subra waikubali kwa wepesi kazi yako uliyofanya wewe!
 
Maskini. Poor little angels..... poleni sana sana wazazi na familia za waliofariki.
 
Hii hali ukiwa kama mzazi unajiuliza umetenda kosa gani mpaka uyapitie haya? Ni wakati mgumu na inaumiza sana..

Mwenyenzi Mungu awape faraja wahusika
 
Back
Top Bottom