Ajali ya Gari Karatu Arusha: Coaster yaua Wanafunzi na walimu wa Lucky Vincent (karibu wote)

Ajali ya Gari Karatu Arusha: Coaster yaua Wanafunzi na walimu wa Lucky Vincent (karibu wote)

Waziri Mkuu Mstaafu, Edward
Lowassa ametuma salamu za rambi
rambi kutokana na tukio la watu 32
kufariki dunia katika ajali ya basi.
Waliofariki katika ajali hiyo iliyotokea leo asubuhi Karatu, ni wanafunzi 29, walimu wawili, pamoja na dereva wa gari hilo.


“Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya ajali hiyo, ni ajali mbaya ambayo inaifanya siku hii kuwa mbaya katika
historia ya nchi yetu,”alisema Miongoni mwa wanafunzi waliofariki ni pamoja na wanaume 11 na wasichana 18.

Kadhalika maiti 32 zikiwamo za walimu wawili, dereva mmoja na wanafunzi 29 zimepokelewa sasa hivi katika Hospitali ya Lutheran Karatu.

Chanzo: Mwananchi.
Mbona hajaenda??? Si yupo Jirani tu hapo! Au uchaguzi ukikaribia ndio anaendaga misibani kwa msafara na kula kwa mama ntilie Tandale!
 
Inasikitisha sana lakini ndio mipango ya Mungu hatuna namna yatupasa kukubali matokeo!

Mwenyezi Mungu azipokee roho za wapendwa wetu waliotutangulia kupitia ajali hii!
 
Mkuu unafeli sana ku'report habari za watoto waliofariki kama hivi, ingekua upo jela watu kama nyie dawa yenu ni kuliwa tu. Kuwa na adabu.
Si mpaka awe jela, huyu analiwa huku huku uraiani.
 
RIP.

Huu ni ukweli usiopingika magari mengi ya shule hayapitii tanuri kali la ukaguzi wa usalama kwa ile dhana ya sijui tuite ni "kujali"? Au "huruma" kuwa hayo ni ya wanafunzi.

Asilimia kubwa ya mabasi ya shule ni yale ambayo yamechoka kazi za kuhudumia usafiri wa uma yamepakwa rangi za mabasi ya shule lakini hayahudumiwi ipasavyo. Ni bahati nzuri tu haya ya mjini hayendi safari za mbali.

Maelezo yaliyotolewa na mmoja wa manusura wa ajali kwamba basi hilo Coaster lilikata breki yanasadifu kabisa mwonekano wa basi hilo maana inaelekea baada ya kupaa lilienda kuangukia pua "nose diving" hivyo impact ya kugongana vichwa au kugonga kichwa ilikuwa kubwa kwa wahanga wa ajali na inawezekana ni kwa nini hakukuwa na damu nyingi iliyomwagika eneo la tukio

Hatua zichukuliwe sasa kudhibiti usalama wa mabasi ya wanafunzi.
tuseme ukweli school bus ya bei ndogo ni TATA ambalo linauzwa 100m shule ngapi zinamudu kununua? ukizingatia huyu bwana mkubwa ana negative altitude na sekta binafsi. Wamiliki wa shule hawafanyi biashara wanatoa huduma, serikali lazima itie mkono wake, hizi shule zipewe ruzuku basi zipewe sawa na shule za serikali zinavyopewa angalau.

Mafao watudhulumu, vyeti wavichane, makato ya helsb yaongezwe, pesa za nhif wakajengee majengo udom na hayo majengo wakae wao kwa kisingizio cha kuhamia dodoma na wanetu waachwe wajifie kwenye school bus mbovu, hapana hili hatukubaliani nalo.
 
Sis kwema. Umekuwa kimya kumbe ushabadilisha hata avatar yangu. Safari hii sikulalamikii lakini baada ya muda nitaanza kuipigania ile ya mwanzo. Nimesoma soma kidogo kumhusu huyu malkia. She was tough!

Watoto hawa masikini. Basi hilo utakuta pengine lilikuwa choka mbaya balaa...
Nipo bro, nilikuwa kwenye ban flani hivi hahahaha, lesson learned! Indeed ISIS ni Goddess wa magical powers!
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] Duu jamaa hiyo heading umenifanya nicheke kwa sauti, lakini ndio hivyo ukweli mchungu.
 
Nikiskia ajari ya gari siku yangu huwa mbaya.wazazi poleni sana .Mungu azipokee roho zao.Amen
 
Mungu azipumzishe roho za hawa watoto mahali pema
Poleni sana wazazi waliondokewa na watoto wao na kwa wengi kwa kweli huu ni msiba mzito sana sana
Upo shemeji.......ni msiba mzito kwakweli. Mungu awape faraja wafiwa wote
 
Ni habari mbaya sana kwa jumamosi ya leo, tumbo la uzazi limenikata..........RIP watoto na walimu, poleni ndugu jamaa na marafiki mlioguswa na huu msiba
 
Dah,yako mambo mengi sana yaliyofichika kwa mwanadamu ndomana huwa tunatoaga ushauri mwingi sana baada ya matukio,lkn jumla ya mambo yote hayo ni mapepo tu na wala co yote ni mipango ya Mungu
Ninacho shangaa idadi ni kubwa lakin basi bado zima nyuma inamananwatoto hawakusimamiwa kufunga mikanda au kitu gani hapo!!?? Maana ukiliona basi lilivyo na idadi ya walio tutangulia inachanganya hapa ,
 
Back
Top Bottom