Ajali ya Magari 13 Msafara wa Makonda; Tusome Alama za Nyakati

Duu hasara kubwa sana
 
Kwani hizo garama ni za kwako ama za chama waswahili mbona mnajiaibisha hivi..akina mbowe wakifanya ziara na mahelkopta wanatumiaga makaratasi sio.
Gharama ni walipa kodi ukiwemo wewe na mimi. Haihitaji certificate kubaini hili, lakini pia ni kielelezo cha uduni wa elimu yetu.
Mbali na CCM kuwa ndio chama chenye serikali hivyo kinayo mamlaka ya kwenda mahali popote na watendaji wa serikali ili kutatua kero mbona uulizi gari za umma zinafata nin kweny misafara ya akina mbowe ama hizo gari za polisi ni gari zako
Sidhani kama unaelewa unazungumzia nini. Naomba nikusalimu tu, habari za asubuhi. Maisha yaendelee
 
Mkuu, hii inasikitisha na kutia hasira sana, yaani unashindwa kuelewa anayeyabariki haya yote ana nia gani haswa.

Wengi wanadhani ni tatizo la DAB, hapana! hili ni tatizo la uongozi wa nchi.

Huu ufujaji na upotevu wa pesa za Umma ni sawa na zile zilizopotea kwenye taarifa ya CAG n.k.

Watumishi wa Umma wana mfumo unaowasimamia , DAB hayupo katika wasimamizi hao.
Magari ya Umma kwa kutumia rasilimali za Umma kwa shughuli za Chama si sahihi, ni makosa.

Magari zaidi ya 10 ya Umma yaliyoharibika hayatengenezwi au kununuliwa na Chama. Ni kodi za Watu wote.
Kuharibu magari 10 halafu tuagize kwa gharama za Tsh 400 Milioni kwa gari moja ni ufujaji uliokithiri.

Huyo Mwenezi hana , narudia tena hana uwezo wa kumwajibisha hata mfagizi wa Ofisi kwa kanuni za utumishi.
Bashite hana tofuati na Ali Kamwe au Ahme Ally wa Yanga na Simba.
Leo msafara wa magari ya umma unamhusu vipi.

Yeye si tatizo kwasababu atafanya tu anavyoona. Wanowajibika kwa hili ni Mh Rais , Mh Makamu wake na Mh Waziri mkuu wanaoruhusu ufujaji na upotevu wa pesa wakati kuna maeneo yanahitaji rasilimali.

JokaKuu Pascal Mayalla
 
Mtu mwenye akili timamu na mwenye fika huru zisizo na ushabiki wa kivyama hawezi kuikubali ccm na serikali yao. Watanzania wanatakiwa kujua kwamba mchawi wa maendeleo yao ni ccm. Chama kinatumia magari ya serikali na hapo hapo kinapewa ruzuku.

Kama viongozi wa chama na serikali wanaona hayo na wanayafumbia macho ni wazi kwamba wanafurahia wananchi kuendelea kuumia.

Ccm ni hasara kwa watanzania.
 
Yote yamepata baraka za mwenyekiti wa chama taifa, tangu mashindsno haya ya Tanzania Makonda Rally yaanze ni mwezi sasa na CCM imekuwa ikifurahia kuona kasi ya magari hayo huko mikoani kuwa ni ushindi dhidi ya upinzani, CCM ndicho chama kinachohujumu uchumi wa Tanzania.
 
Chama tawala chatakiwa kuonyesha mfano wa namna bora ya kutatua matatizo nchini.

Pia chapaswa kuonyesha kwamba kipo makini kwenye matumizi ya fedha za umma na chasimamia uchumi wa nchi ipasavyo.

Moja ya njia bora kabisa na iso na gharama ni kuwatumia wabunge, wakuu wa wilaya au wakuu wa mikoa kutatua kero na matatizo ya maeneo waliyopo.

Na hata hivyo hao ni watu wa juu kabisa maana chini wapo wakurugenzi wa maendeleo na maofisa wengine wadogo.

Shida ingine kubwa kabisa kwa wabunge wa Tanzania ni kukosa ofisi maalum majimboni jambo ambalo CCM na Chadema wamefanya iwe hivyo kwa makusudi.

Pili, si upinzani wala CCM wenye haki ya kuonyesha matumizi mabaya ya fedha, kwani wakati wa kufanya kampeni rasmi haujafika na hali ni hiyo je, ukifika wakati wa kampeni wa 2025 gharama zake mwatoa wapi?

Hivi hamuoni hata haya kwa kufanya ujinga huu wa kiwango cha juu, kuchezea fedha za walipa kodi na fedha za kukopa nje na vyanzo vingine?
 
Inashangaza sana Kwa kweli...

Mimi nimewahi kushuhudia msafara wa Daniel Chongolo wakati huo akiwa Katibu Mkuu - CCM ukiwa na magari yasiyozidi 10 tu na mengine yakiwa ya watu binafsi...

Kwa Daud Albert Bashite (Makonda), mtu anaweza kujiuliza hivi inawezekana vipi kiongozi wa kaidara kadogo tu ndani ya CCM awe na masafara wa magari karibu 70 tena mali ya idara mbalimbali za serikali yanayopaswa kuwa huko kuhudumia wananchi lakini yanalazimishwa kutumika kufanyia propaganda za kijinga na kipuuzi za huyu bwana asiyestahili kupewa uongozi wowote hapa nchini?

Kuna shida gani huko CCM? Hivi inawezekana wanatumia nguvu hii kubwa kwa kutumia rasrilimali za umma wote kwa shughuli za chama ili kulazimisha watu waone kuwa CCM ipo wakati haipo na imekufa kabisa?
 
Uharibifu huo unanonyesha kuwa kulikuwa na impact ya nguvu sana, yaani magari yalikuwa yanakwenda kasi sana kwenye barabara hiyo nyembaba tena ya vumbi. Uendeshaji mbovu sana huo. <Mara nyingi madereva wa serikali hudhani kuwa kwenda kasi sana ndiyo usalama lakini ni ujinga mtupu. Utakuta gari linatoka benki kuchukua hela linakwenda klasi hovyo hovyo baila kufuata sheria za usalama barabarani
 
Umenena kweli tupu ndugu,baadhi akili zao zinawaza kila lenye kutokea ni ushirikina tu, utadhani walisoma darasani kwa kufundishwa na waalimu washirikina.
 

[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] eti "ZeroBrain" daaah
 
Hamnaga hoja upinzani sijui mnashida ipi?...Ziara hazina tija mbona wew ndio zero brain sas.Mtu kabaini utendaji mmbovu wa DED huko tanga unakuja kusema ziara haina tija
Huo utendaji mbovu wa DED wa CHADEMA!!??
Huyo DED anapaswa kusimamiwa na CHADEMA!!?
Wananchi kila siku wakilalamika juu ya utendaji wa serikali kwa ujumla,hiyo serikali ni ya chama gani!!??

Kichwa kitupu cha kufugia nywele ni mzigo kwa kiwiliwili.
 
Daaaaah!!!
Ngoja niishie hapa.

R.I.P Edward Ngoyai Lowassa mzee wa
Elimu
Elimu
Elimu.
 
Kwani serikali inaongizwa na Chama gani!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…