Ajali yaua watu wanne wa familia moja Morogoro

Vigari vya mjapani miaka hii ni kama karatasi tuu
 
Usalama wa viongozi ni first priority. Gari zao lazima ziwe na stability ya kutosha kuhimili miundombinu ya nchi yetu.
Ndiyo wanunue gari la milioni 500??? Hivi ukienda Uholanzi hujaona PM anaenda ofisini na baiskeli?
 
Mkuu elewa kuwa hiyo ni ajali.

Kwani mpaka mtu aingie barabarani kuendesha gari anakuwa hajui kukwepa gari inayokuja mbele yake?

Kuna kitu kinaitwa "mzuka" ni wazimu flani ambao huwapanda madereva karibia wote wawapo barabarani!

Madereva siku zote tunaambiwa, tuliza akili unapoovertake, uwe unaona umbali wa kutosha na pasiwe na kona.

Usikimbie mwendo kasi kama uendako siyo mzoefu wa njia hiyo, pia kama kuna mvua ama ukungu unaokuzuia kuona sawa sawa!

Lakini yote hayo kwa madereva ni ngonjera zisizokuwa na maana yoyote.

Njiani kuna rough za kila aina bila kujali kuwa gari unayoiendesha dereva, una dhamana nayo pia ulinzi na uhai wa maisha ya wenzako muda huo upo mikononi mwako.

Pole zao majeruhi na kwa marehemu pamoja na wafiwa.

Tunawaombea kwa Mungu awakinge na adhabu ya kaburi, wapumzike kwa amani na majeruhi wapone kwa haraka.
 
Barabara zetu zimekuwa na shida ya maroli yanayotembea taratibu sana na hasa inapotokea ni kamlima marolinhayo hutembea taratibu sana na kufanya kuwe na foleni ya malori mengine, wenye magari madogo wengi huwa na haraka na hasa anapoona msururu wa maroli, maana kutoka kutembea 100km/h mpaka 10km/h ambayo pengine utatembea kwa dakika 10 au 15, mtu anaona ajilipue tu, ndio kinatokea kama kilichotokea kwambe, nawaza tu kwa sauti
 
Wote waliokufa Ni masoja wa kambi flani pale mjini morogoro. Nawajua hao wawili wadada. Kati ya waliokufa watoto Ni wawili mmoja miezi 9 mmoja miaka mitano.
Aliyepona Ni dada yao walikua wametoka Dodoma hospitali kumtibia but huko ikashindikana so walikuwa wakiekekea Dar siku 2 hizi.
Nb.
Kila kifo Ni funzo jipya juu ya ukufi wa maisha ya binadam lazima tujiulize kila Mara ikiwa mtoto wa miezi 9, mtoto miaka 5 wanakufa iwe Mimi mwenye 42, 25, nk?
 
Moro-Dumila highway inakunywa damu si mchezo
 
Nadhani tutapoteza familia sio ukinunua gari tuu na udereva unaweza kisa Leseni umeletewa pana haja kuwa makini ukishindwa kodi dereva awapeleke kijijini kuliko kujaza familia kwa Leseni ya Duka...gari ndogo inapepea inakua nyepesi pale inapopishana na gari kubwa nimeona madereva wengi hawapunguzi mwendo wanapopishana yeye akiamini yupo site yake kumbe katikati ya Tela na horse pale panakua na upepo unaoweza kutoa gari ndogo nje ya bara bara kama utaipita au kupishana na Truck kwa kasi sana...
 
Hivi mtu kuwa mtakatifu anakuwaje?
 
Sio kwamba gari ikijaza abiria full (kama hao watu sita ndani ya Spacio) inakua nzito... Stable?
 
Mbeya Moro singida mikoa ya kafara za barabarani haipiti mwezi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…